Ni Siri Kuu - The Great Mystery

Ni Siri Kuu - The Great Mystery
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.

Jumamosi, 4 Novemba 2017

ZAWADI KWA ALIYEOKOKA

 SIKU MUHIMU KATIKA MAISHA YAKO
ziko siku pengine nyingi zilizo za Muhimu sana kwa mwanadamu katika kuwepo kwake hapa Duniani. Siku muhimu ya kwanza ni siku uliyozaliwa, na siku ya pili ambayo ni kubwa kuliko zote tangu kuzaliwa ni siku hii/hiyo uliyo okoka, na siku ya tatu muhimu ni siku utakapopumzika katika Kristo Yesu.

PONGGEZI KUU KWAKO
Hakika, unastahili pongezi kuu kwa uamzi ulioufikia sasa, uamzi wa kumwamini na kumkiri Yesu kuwa BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO, ni uamuzi wa maana na hatua kubwa kuliko hatua yoyote katika maisha. Hii ni kwa sababu pia watu wengi hawapati neema ambayo wewe umeipata, hivyo Huduma ya (Ni Siri Kuu, kupitia Mwl. Goodluck Kazili) na waamini wote pamoja na walioko mbinguni tunakupongeza kwa uamuzi wako. Ni wazi umuhimu wake unaweza usionekane haraka, lakini thamani yake ni kubwa kuliko mambo yote kwako hapa Duniani.

THAMANI ULIYOIPATA
Uko ufalme wa nuru (MUNGU), tena uko ufalme wa giza, hivyo wewe siyo tena wa ufalme wa giza bali ni wa ufalme wa nuru yaani wa MUNGU mwenyewe aliyeumba mbingu  na  nchi katika Kristo Yesu Pamoja na Roho Mtakatifu. Thamani kubwa kwanza uliyoipata ni ile ya kuondolewa kaitka    ufalme wa giza   shetani na kuingizwa katika ufalme wa Mungu. Na      apa inathibitishwa hivi
“Naye alituokoa kutoka katika nguvu za giza akatuhamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake, ambaye katika Yeye tuna ukombozi, yaani msamaha wa dhambi (Wakolosa 3:13-14)”
Thamani hii imetokana na upendo wa Yesu, ambaye aliitoa Damu yake kusudi kwa hiyo uweze kutakaswa, hapa anasema, “Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu kwa damu yake. (Ufunuo 1:5b)”
Hata hivyo jua kuwa ulipokuwa haujaokoka/ haujazaliwa mara ya pili kwa roho haukuwa na thamani katika ufalme wa Mungu, na usingeweza kuuona wala kuuingia kwa hakika, maana Yesu mwenyewe anasema Lakini wewe sasa kwa njia ya Roho, umezaliwa mara ya pili, hivyo umepata sifa ya kuuona na kuuingia ufalme wa Mungu. Sasa wewe ni wa thamani sana mbinguni na Duniani.

UMUHIMU WA KUOKOKA/WOKOVU
Kuokoka au kupata wokovu si suala la dini, wala suala la kanisa fulani, wala haki ya dhehebu fulani, bali ni mpango mahususi tena kamili wa Mungu kumuokoa na kumkomboa mwanadamu kwa njia ya imani, maana hapa maandiko husema “kwa sababu ukimkiri Yesu Kristo kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako  ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. (Warumi 10:9-10)” na si jambo jema hata kidogo kufikiri kuwa wokovu ni wa watu wa dhehebu fulani. Bali ni baraka tena ni haki tena ni faradhi kufikiri na kujua kwa hakika kuwa wokovu ni mpango wa Mungu wa kumuokoa kila mwanadamu. Ni vibaya sana dhehebu kujimilikisha wokovu, na ni vibaya sana dhehebu kuukataa wokovu na kuona kuwa ni kitu cha watu fulani.
Ni kweli na hakika kuwa mtu asiyeokoka, hawezi kuuona wala kuuingia ufalme wa mbinguni. Hapa Yesu anasema “amini amini nawaambieni mtu asipozaliwa mara ya pili hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. (Yohana 3:3). lakini maneno haya kwa wengine yalionekana kuwa magumu, kwa kujiuliza inawezekanaje mtu kurudi tumboni mwa mama yake na kuzaliwa tena mara ya pili? Katika fahamu zetu kama wanadamu haiwezekani kabisa, lakini hapa Yesu anabainisha tena kwa msisitizo zaidi kwa kusema ““amini, amini, nakuambia mtu asipozaliwa kwa Maji na kwa Roho hawezi kuuingia ufalme wa Mungu (Yohana 3:5)” Katika mafafanuzi ya usemi huu, anasema “kilichoza; liwa na mwili ni mwili nakilichozaliwa kwa roho ni roho”, hapa alimaanisha kuwa unapozaliwa mara ya kwanza unazaliwa katika tumbo la mama yako, hapo wewe ni mwili kabisa, lakini mwili hautaurithi ufalme wa mungu. Hivyo kama umezaliwa na mama yako ambaye ni mwili, basi hata wewe ni mwili, na kwa sababu hiyo usipozaliwa katika roho huwezi uuona wala kuuingia ufalme wa Mungu. Kuzaliwa katika roho ni kwa njia ya imani ya kumwamini Kristo Yesu, na kutiwa muhuri yaani kubatizwa. Lakini hapo kinachohitajika tena ni ile kukiri hicho unachokiamini, yaani huyo Kristo unayemwamini moyoni mwako kumkri, ambapo kukirki huko kunakufanya uokoke, kunakufanya upate wokovu. awaye yeyote asikudanganye wala kukuhubiri injili yoyote inayokanusha habari hizi, maana huo ndio uzima wako, wala jambo liwalo lolote lisikutoe katika kuamini huko kunakotajwa maana thamani          yake ni zaidi ya chochote. Hapa Yesu ananena “kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? (Mathayo 16:26)”. Hakuna uwezacho kutoa na kuwa fidia ya nafsi yako, bali wokovu pekee ndio jibu na uzima wa nafsi.
WOKOVU NI MCHAKATO
Suala la wokovu huanza siku moja, lakini halikamiliki ndani ya siku moja hiyo hiyo, maana ni mchakato ambao unamhitaji mtu mwenyewe kuhusika kikamilifu kwa msaada wa huyo Roho Mtakatifu. Ndiyo maana kati ya vitu muhimu ambavyo mtu anavihitaji mara anapo okoka, ni kumpokea Roho Mtakatifu.
Kuokoka na kutokuwa na roho mtakatifu ni sawa na kumvua samaki wa kufuga kisha ukamwacha bila maji, lazima tu atakufa, ndivyo alivyo mtu anayeokoka na kuendelea kuishi bila ujazo wa Roho Mtakatifu. Ama ni kama mtu anunuaye gali na kuiendesha bila kuwa na oili, gali hiyo lazima itanoki injini na itakufa kabisa.
Ndugu uliyeokoka, unahitaji Roho Mtakatifu sasa, ili uingie katika hatua nyingine ambayo sasa utaanza kumjua Mungu. Maana ni kweli kuwa hatupati uzima wa milele ile tu kuokoka, bali kuokoka ni hatua ya msingi wa kutupeleka kwenye hatua  za kumjua Mungu ambao ndio uzima wa milele. “kama vile ulivyompa mamlaka juu ya wote wenye mwili, kusudi wote uliompa awape uzima wa milele. Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe Mungu wa pekee, wa kweli na Yesu kristo uliyemtuma. (Yohana 17:2-3)”. Wokovu unafikia hatua ya utimilifu mara unapofika kiwango cha kumjua Mungu katika kweli. Hatua hii huwezi kuiingia bila kuwa na Roho Mtakatifu       
 Maa     na hakuna ajuaye mambo ya Mungu ila Roho Wa Mungu. Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ua binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho wa Mungu. (1Wokorintho 2:11)”
Hivyo hakuna awezaye kumjua Mungu asipojulishwa na Yesu kwa njia ya Roho Mtakatifu. Na ndiyo sababu Yesu aliwasisitiza sana wanafunzi, kuwa ni muhimu sana Yeye aondoke ili kusudi Roho Mtakatifu naye aje ambae atawafundisha kumjua Baba yaani Mungu kwa huyo Roho ambaye watampokea mara baada ya Yesu kuondoka. “lakini mimi nawaambia iliyo kweli; yawafaa ninyi mimi niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu, nitampeleka kwenu. Naye akisha kuja huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu. (Yohana 16:7-8)”
Hivyo maadamu umeokoka, kwa maana ya kumpokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa maisha yako, hapo umestahili kumpokea Roho Mtakatifu. Ambaye Yesu anampeleka kwako makusudi tu akufunulie kumjua Mungu. “Akasema, nimekabidhiwa vyote na baba yangu; wala hakuna amjuaye Mwana, ila baba; wala hakuna amjuaye Baba ila Mwana, na yeyote ambaye Mwana apenda kumfunulia. (Mathayo 11:27)”
Kwa ufafanuzi huo, wokovu huanza na Imani moyoni, kisha kukiri kile ulichokiamini. Huo tunaita kuokoka, lakini mara baada ya kuokoka, sasa unapaswa kumpokea/kujazwa Roho Mtakatifu, ili akufikishe mahali unapotakiwa kufika yaani kumjua Mungu.
Si wewe tu ambaye umeokoka na inawezekana ukawa huna Roho Mtakatifu, bali wako wengine. Tena kwenye maandiko wanatajwa watu ambao walikuwa wameokoka lakini hawajui hata kama kuna kitu kinaitwa Roho Mtakatifu maana hata kusikia tu hawakuwahi kusikia.
“Paulo akiisha kupita kati ya nchi za juu, akafika Efeso; akakutana na wanafunzi kadha wa kadha huko; akawauliza, je! Mlimpokea Roho Mtakatifu mlipoamini? Wakamjibu, la, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia. (Mdo 19:1-2)”
Lakini haikuwa haki kwao kuokoka na kuishi bila kuwa na Roho Mtakatifu. Hapo sasa ndipo walipoamini upya kwa kubatizwa kisha wakampokea Roho Mtakatifu wote kwa idadi yao. “Na Paulo alipokwisha kuweka mikono yake juu yao, Roho Mtakatifu akaja juu yao; wakaanza kunena kwa lugha, na kutabiri. Na jumla yao walipata wanaume kumi na wawili. (Mdo 19:6-7)”


Mwl. Goodluck Kazili
(NI SIRI KUU/THE GREAT MYSTERY)
Hakiuzwi/ kimeamuliwa na Mungu kama Sadaka

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni


Kunihusu

Picha yangu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Tafuta katika Blogu Hii