UTATU
MTAKATIFU NA KUSUDI KWA MTU
(MUNGU BABA, MUNGU MWANA, MUNGU ROHO MTAKATIFU)
DONDOO:
UTANGULIZI
SEHEMU YA KWANZA
Ø NAFASI
YA MUNGU BABA KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
Ø NAFASI
YA MUNGU MWANA KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
Ø NAFASI
YA ROHO MTAKATIFU KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
SEHEMU YA PILI
NYAKATIA TATU MHIMU
Ø KUUMBWA
ULIMWENGU
Ø BAADA
YA UUMBAJI AGANO JIPYA
Ø UJIO
WA KRISTO: AGANO JIPYA
SEHEMU YA TATU
UGAWAJI WA MADALAKA
Ø KUTOKA
KWA MUNGU HADI KWA YESU KRISTO
Ø KUTOKA
KWA YESU KRISTO HADI KWA ROHO MTAKATIFU
SEHEMU YA NNE
MAMLAKA NA UHUSIANO BAADA YA UGAWAJI MADALAKA
Ø MAMLAKA
YA MUNGU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAMU
Ø MAMLAKA
YA YESU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAUMU
Ø MAMLKA
YA ROHO MTAKATIFU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAMU
SEHEMU YA TANO
UMHIMU NA ULAZIMA WA KUJUA NA KUFUATA UTARATIBU HUU
Ø KUSUDI
LA MUNGU KWA MWANADAMU
Ø UTILIMILIVU
WA KUSUDI
Ø HITIMISHO
SEHEMU YA NNE
MAMLAKA NA UHUSIANO BAADA YA
UGAWAJI MADALAKA
Ni mhimu kufahamu kuwa utendaji
kazi wa Mungu umebadilika sana kulingana na vipindi ambavyo vimepita. Hali hiyo
inapelekea mfumo pia wa mwanadamu kutakiwa kubadilika katika uhusiano wake na
Mungu. Kitu kilichowakwamisha wayahudi hadi leo wengi wao wasimwamini Kreisto
ni kutokujua mabadiliko ya utendaji kazi wa Mungu na uhusiano wake na wanadamu.
Japo maandiko yalikuwa yametangulia kueleza wazi kuwa kutakuwa na mabadiliko:
Yeremia 31:3
Hakika Mungu ni mmoja lakini
mwenye nafsi tatu za utendaji kazi, kusema mwenye nafsi tatu ni mhimu kuelewa
kazi ya nafsi ni kupambanua na kufanya maamuzi. Hivyo kwa ufupi na tafsiri ya
karibu tunaweza kusema kuwa Mungu anapambanua na kufanya maamuzi katika maeneo
matatu au kwa namana tatu. Hivyo kwetu wanadamu husema yuko Mungu Baba, Mungu
mwanaNeno, na Mugnu Roho Mtakatifu: kwa maana wako watatu washuhudia[mbinfuni, Baba, na Neno,
na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. Kisha wako watatu washuhudiao
duniani], Roho, na maji, na damu na watatu hawa hupatana kwa habari moja,
(1Yohana 5:8-9a)
Hata hivyo ni mhimu kujua kuwa,
utenfaji kazi huo, ambao umebadilika katika vipindi maalumu ambavyo vina maana
kubwa kwetu.
Ukisoma kwenye maandiko
matakatifu utakutana na wakati ambao Mungu alikasilishwa na akaamua kumupa
mamlaka malaika ya kuwaongoza wana wa Israel; kutoka
32: 34: basi sasa uende ukawaongaze watu
hawa mpaka mahali paloe ambapo nimekwambia habari zake; tazama Malaika wangu
atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kawa ajili ya
dhambi yao.
Hata hivyo tuna wakati wa
kujiuliza kwa nini Mungu hakuwapa Mwana ndiye awaongoze; hakika yake ni kuwa muda wa
Mungu kujifunua kupia Mwana ilikuwa bado, pia ni wazi kuwa nafasi ya taifa moja
hakukuwa na ulazima wa kujifunua kupitia mwana wakati ulimwengu mzima ulikuwa
na shida, hivyo kwao malaika alitosha, hata hivyo ukiendelea kusoma unaona kuwa
Musa alikataa kwenda na malaika.
Na jambo hili ndilo ambalo
limefanyika kwa wayahudi japo si kwa kukataa kwenda na Yesu ila kwa kutokujua
kuwa utendaji kazi katika dunia hauko tena chini ya nafsi ya Mungu Baba bali
Mungu mwana.
Ilipofika kipindi Fulani cha
wakati kama unabii ulivyokuwa umeonyesha Mungu alihamisha mamlaka yake ya
kuisimamia dunia na kuweka chini ya Nafsi yake iliyo mwana yaani nafsi ya pili
ya utendaji kazi ambayo ni Mwana;
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa Tumepewa motto
mwanamume na uweza wa kifalme utakuwa bagani mwake; naye ataitwa jina lake,
Msahuri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani (Isaya
9:6). Pia kaitka Mathayo 1:21Naye atazaa
mwana , nawe utamwita jina lake Yesu, maana ndiye atakayewaokoa watu wake na
dhambi zao, Hayo yamekuwa ili litimie neon lililonenwa na Bwna kwa ujumbe wa
nabii akisema, Tazama bikra atachukua mimba naye atazaa mwana; Nao watamwita
jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.
Ugawaji wa mamlaka hii ulikuwa na
maana kubwa sana, hasa kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu, kwa maana ya kuwa
Mungu aliamua aitoe nafsi yake ambayo ni mwana ili aifanye kuwa upatanisho kwa
dhambi kati ya wanadamu na Mungu. Hii humaanisha kuwa Mungu hatamtazama
mwanadamu tena moja kwa moja isipokuwa ataitazama nafsi yake/mwana kisha ndani
yake atamuona mwanadamu. Na kwa kuwa katika nafsi hiyo ilitolewa damu ambayo
huwasafisha dhambi zao, hivyo Mungu hataiona dhambi kwa kuwa watakuwa
wametakaswa.
Haikutosha tu kuzaliwa kwa Yesu
na kuwapa msingi wa namana ya kuishi maisha mpya yaani ya Kikristo, bali
walitakiwa wakae nae ili kupata msaada zaidi wa kuendelea kuufahamisha
ulimwengu hiyo namna mpya na ukombaozi ulioletwa na Mungu kwa wanadamu kupitia
nafsi Yake. Na kwa kuwa kazi ya nafsi ya pili yaani mwana ilikuwa kutoa damu na
maji kwa ajili ya ukombozi na utakaso wa dhambi, kazi ya kuendelea kushuhudia
ukombozi hou haikuwa ndani ya nafsi mwana balili ilikuwa ndani ya uwezo wa
nafsi Roho Mtakatifu; hivyo baada ya nafsi Mwana kumaliza kazi yake ilikuwa ni
lazima nafsi nyingine ije kwa ajili ya ukamilisho.
Hapa huwa kuna changamoto kubwa
kwa kuwa watu wengi wanaishia kwenye nafsi ya pili yaani mwana; wakijua kuwa
baada ya kuokoka, kubatizwa na kutakaswa kwa damu ya Yesu hudhani kuwa mambo
tayari, na wakati mwingine hufikri wanaweza kuyaishi hayo maisha ya utakatifu
walioupata kupitia kwa mwana. Kumbe ni lazima kumalizia na hatu nyingine mhimu
sana ya nafsi ya tatu yaani Roho Mtakatifu kwa kuwa huyo nidye kila kitu baada
ya mtu kuokoka, kubatizwa na kutakaswa.
Maandiko yameweka wazi mambo haya
japo watu hawayazingatii, na ndio maana wanakwama sana katika huduma zao, imani
yao, na hata katika kutunza wokovu hou walioupata.
Ukisoma habari za Yesu ni baada
tu ya kubatizwa alichukuliwa na Roho kwenda kujaribiwa nyikani. Kwa hali ya
kawaida kulikuwa na haja gani ya Yesu kuchukuliwa na Roho Mtakatifu; (Math
4:1). Baada ya Yesu kukaribia kuyondoka
kwenda mbinguni aliwaambia wanafunzi/ mitume; Lakini mtapokea nguvu, akisha kuwajilia juu
yenu Roho Mtakatifu;nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika
Uyahudi wote, na Samaria na hata mwisho wa nchi, (matendo 1:8)
Hawa hawakuwa na sifa ya kuwa
mashahidi wa Yesu kabla Roho mtakatifu hajawajilia, ni mhimu kujiuliza vema
maana hawa wanafunzi walikuwa wamekaa na Yesu mda wa miaka mitatu na nusu
akiwafundisha tena wakitembea naye na wakihubiri
na kufanya ishara na maajabu mengi, lakini bado kuondoka kwa Yesu
walikuwa hawana sifa za kuwa mashahidi wake hadi Roho mtakatifu atakapowajilia.
Ukijiuliza unagundua kuwa kazi hiyo
haikuwa ya Yesu/Mwana bali ilikuwa imewekwa ndani ya Roho Mtakatifu.
Kwa uelewa zaidi kuna wakati
wanafunzi wa Yesu hawakuwa wanapendezwa na taarifa za kuwa Yesu ataondoka,
kisha Yesu akawaambia; Lakini mimi nawaambia iliyokweli; yawafaa ninyi mimi
niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo msaidizi hatakuja kwenu, bali mimi
nikienda zangu, nitampeleka kwenu,(Yohana 16:8). Hapa unaona kuwa
kumbew Roho Mtakatifu yupo, lakini hajapewa hiyo kazi, na Yesu anasema
nitampeleka kwenu halafu ukiendelea kusoma zinatajwa kazi atakazozifanya ambazo
amepewa mamlaka haimaanishi ndizo kazi anazoziweza tu ila kwa duniani amekuja
kufanya hizo; Naye
akisha kuja huyo natauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki,
na hukumu, (Yh 16:9).
Ukipendezwa na somo hili na unahitaji mwenelezo wake tuma email gkazili@yahoo.com au tuma ujumbe no ya simu 0752165609 au 0716050663.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni