SK-Siri Kuu
THAMANI YA MTU WA NDANI (NAFSI)
Na Mwl; Goodluck Kazili
"Wakati ule Yesu
akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo
haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba
, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata
ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? au mtu atatoa nini badala ya
nafsi yake?. (Mathayo 16:26)
Hakuna kitu chenye thamani katika
ulimwengu huu, kama nafsi ya mtu. Nafsi yako ndicho kitu chenye thamani kuliko
chochote unachokijua katika ulimwengu huu, ndiyo sababu Yesu aliuliza au mtu
atatoa nini badala ya nafsi yake?. Je! ulimwengu mzima thamani yake inalingana
na thamani ya nafsi yako? hapana haiwezi kufikia. Na hivyo hakuna chenye
thamani kuliko nafsi yako.
Hata hivyo ajabu ni kwamba, mtu
mwenyewe haithamani hiyo nafsi yake bali anathamini vitu ambavyo nafsi ilipewa
ili kuvitumia. mfano mtu hataki kuokoka kwa madai kuwa atashindwa kuifaidi
dunia na raha yake. Mtu kama huyu, tatzo lake ni ufahamu tu wa kutokujua
thamani ya kila kimoja na matumizi yake na sababu ya kuwekwa hivyo vitu.
Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa
kuna utu wa ndani na utu wa nje. tena utu wa nje uliumbwa kwa ajili ya utu wa
ndani, kama tu nyenzo ambayo mtu wa ndani anapewa ili atumie kwa matumizi yake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni