Ni Siri Kuu - The Great Mystery

Ni Siri Kuu - The Great Mystery
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.

Jumapili, 5 Novemba 2017

Tarehe 5, Jumapili ya NI SIRI KUU

Juma pili, ni siku maarufu kuliko siku yoyote kote ulimwenguni, ni siku ambayo haifanani na siku yoyote. Siku ya jumapili moja, umaarufu wake unalinganishwa na siku zote za wiki.  Pia thamani ya jumapili moja, inalinganishwa na sikukuu ya Krismasi au Pasaka au mwaka mpya ambayo imefanyika siku za kawaida. Siku nyingine zote huitwa siku za kawaida, lakini siku ya jumapili haiitwi siku ya kawaida.

Katika ulimwengu wa sasa, siku ya jumapili, ndiyo inayojulikana sana kuwa siku ya mapumuziko, hata katika nchi yetu siku hiyo kiselikali na katika taasisi karibu zote ni siku ya mapumuziko. Siku hii imewalazimisha hata wale ambao kwao isingewafaa kupumuzika, kupumuzika, kwa kuwa iko kisheria kuwa siku ya mapumuziko. 

Siku hii huitwa siku ya kuabudu, tena huitwa siku ya mapumuziko, tena huitwa siku ya mwisho wa wiki, japo wengine huiita mwanzo wa wiki.
Waadventist/wasabato, wanaona kitendo hiki cha kuifanya siku ya jumapili kuwa siku ya mapumuziko siyo sawa, tena siyo sawa kabisa kuifanya siku ya kuabudu. Hivyo ukienda maaeneo ambayo wanapatikana wengi, kama ni kijijini, siku ya jumapili wakati hawa wakitembea kwenda kanisani, wao utakutana nao wakiwa wameweka jembe begani wakielekea shamba. Kama ambavyo, na hawa wengine jana juma mosi walibeba jembe kwenda shamba.

Ukiangalia katika torati, suala la kushika sabato ni moja ya Amri kuu. Ambapo mtu aliyeivunja hukumu yake ilikuwa kifo.  Mfano mwanamke mmoja anatajwa katika maandiko aliyeokota kuni siku ya sabato, na kwa kuwa huyo alikuwa wa kwanza kufanya kitendo hicho tangu amri zilipotoka, basi wengi walingoja kuona nini atafanywa mtu yule. Lakini kama ilivyokuwa imeandikwa, mwanamke yule aliuawa na hakuna aliyejaribu kufanya kazi tena siku ya sabato.
Mambo ni tofauti zama hizi, siku hii ya jumapili, hata kwa hao wanaoiita sabato yao, yaani pumziko lao bado huwa wanafanya kazi. Mbali na ile kwamba siku imebadilishwa kutoka juma mosi na kuwa jumapili, lakini bado pia jumapili hii, haitendewi haki.
Kabla ya kuzungumuzia kuhusu mabadiliko ya kuibadilisha sabato kutoka juma mosi na kuwa jumapili tuitazame jumapili kama sabato japo tutazungumzia mabadiliko hayo kwa kina.

JUMAPILI
Jumapili siku ya kupumuzika/sabato, je ni kweli Wewe huwa unapumuzika? Juma pili siku ya kuabudu je wewe unakusanyika pamoja wenzako kuabudu?. Maana hata baada ya Israeli kutoka Misri waliamuliwa kukusanyika sikua ya kwanza na ya saba. Na kusanyiko hilo liliitwa Takatifu. “siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yoyote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu. (Kutoka 12:16)”
Maana ya sabato  ni pumuziko, kama kweli juma pili ni sabato kwa nini haupumuziki, mbona ndiyo siku ya kufanya biashara, mbona ndiyo siku ya kufua, mbona ndiyo siku ya kusoma, mbona ndiyo siku ambayo wengine hata kazini huenda. Usabato wa siku ya jumapili uko wapi? Hilo ni swali lako, ujiulize.
Nina hakika kuwa, hakuna anayefanya hivyo ambaye ana ushahidi unaomruhusu kufanya hivyo.  Najua wengi tutatumia agano jipya kuweka utetezi na hasa ile Yesu aliyomponya siku ya sabato. Ni kweli, kama wewe daktari basi nenda kafanye huduma maana yafaa sana, Kama unatoa huduma ya uokozi basi fanya hivyo maana yafaa sana na ni haki. Lakini kama unaenda kufanya biashara, umegeuza kuwa siku ya kufua, umegeuza uwa siku ya kusoma na hasa mitihani ikikaribia, tena umegeuza kama siku ya kumalizia kazi zako zilizobaki, tena umeigeuza kama siku ya kusafiri, tena ofisi wanakulazimisha kwenda kazini nawe umekubali, huitendei haki hata kidogo siku hii ya jumapili, tena humtendee haki Yeye aliyeamuru mapumuziko na ibada kwa siku hiyo.

Sasa nitaeleza kitu hapa nawe utajishauri. Mwaka 2009/, Mungu alisema nami, kuwaambia wanafunzi ambao walikuwa wakienda kujisomea siku ya jumapili waache na badala yake wapumuzike na kuitumia siku hiyo kumtafakari Mungu na kujisomea Neno la Mungu, Lakini hawakusikia. Nakumbuka sana wakati huo, nilikuwa kiongozi wa maombi, wapendwa hawa walikuwa na kawaida hii, Walikuwa wanaamuka asubuhi wanaenda kwenye ibada ya kwanza, ikifika saa 3 asubuhi wanakuwa wametoka kwenye ibada tayari, kisha wanachukua vitabu na kwenda shule kujisomea hadi jioni.

Tena walitengeneza mtandao wa kuombea mitihani yao miezi 3 hivi kabla ya mtihani kufika, wanafunzi hao walikuwa kitado cha sita. Niliposema nao kuhusu hilo, hawakunielewa, basi nikawaacha. Walipoendelea na kazi hiyo ya kusoma, basi nikiwa njiani naelekea kanisani kwenye kipindi nikifika karibu na uwanja wa ndege pale Dodoma, Sauti ikanijia kusema, watu hawa hawajaniheshimu, kwa sababu hiyo, hawatafanikiwa kama wanavyotazamia sitawafanikisha ijapokuwa wananiomba kwa bidii. Tulipkutana kwenye kipindi, nilisema maana nilitajiwa na matokeo ambayo wangeyapata. Nakumbuka sana wakati huo walikuwa wameshamaliza mtihani wa mock. Na walikuwa wamefaulu sana, hivyo nilipowaambia matokeo watakayopata kwa sababu wameshindwa kufuata maelekezo ya kuiheshimu siku ya jumapili/sabato kwa kupumuzika, lakini ni kama walibeza na kuona kama mtu nichezae na jambo lisilowezekana.

Basi tuliendelea katika hali hiyo, yuko mtu mmoja ambaye alitii na kuacha ambaye alikuja kuniambai kama ushuhuda. Matokeo yalipotoka, wale wapendwa hawakuamini kilichotokea, na kwa ushahidi yule mmoja aliyeacha akafaulu kwa daraja la kwanza na hakutegemewa hata kidogo. Wakati huo waliofaulu vizuri walikuwa 2 miongoni mwetu tuliokuwa katika kundi lile, japo mimi nikiwa kidato cha tano.  Wako walioelewa kilichotekea na wengine hawakuelewa mpaka leo. Mungu hakuwafanikisha vile alivyokusudia, japo baadhi walifaulu kwa arama za kuwawezesha kuendelea na vyou lakini si kiwango kizuri kilichokusudiwa na walichotazamia.

Jumapili ni siku ya mapumuziko, mwanafunzi usisome, mfanya biashara usifanye biashara, mfanya kazi usifanye kazi kama si kazi iliyoainishwa yaani hizo za huduma ya uokozi, mama na Dada nyumbani usiitumie kufua nguo, usiitumie kumalizia kazi zako au kupunguza, usiitumie kujipa kazi. Sote tusiitumie kusafiri. Siku ya jumapili itumie kupumuzika kwa kumwabudu Mungu, kumtafakari, kujifunza Neno, kumsifu, kuwatia moyo wengine, kuwafariji wengine, kuwahubiria wengine nakwa ujumla kuujenga mwili wa kristo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni


Kunihusu

Picha yangu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Tafuta katika Blogu Hii