Ni Siri Kuu - The Great Mystery

Ni Siri Kuu - The Great Mystery
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.

Alhamisi, 7 Aprili 2016

UJUMBE MAALUMU KWAKO

Mwl; Goodluck Kazili

Tumia muda wako japo mfupi kusoma haya, na kuyatia katika fahamu zako, maana huendayakakufaa ikiwa Roho wa Mungu atakusaidia kuyafahumu vema.
 
Unafkiri vipi ukifanya kitu kwa lengo flani kisha kile kitu ulichokifanya wewe kikakataa au kushindwa kufanya vile utakavyo, hapo utajisikiaje? Na je! utafanya nini? Hivi unajua kwa nini dunia iliumbwa! Na kwa nini wewe uliumbwa! na aliyeiumba hii dunia alikusudia nini! na aliyekuumba wewe alikusudia nini!. Ukimuuliza mama yako na baba yako kama wako hai watakwambia kwa nini waliamua kukubali wewe uwepo kwenye dunia hii! Lakini ikiwa wao tu wasioweza kukufanya wewe, ila tu walitumiwa kukuleta, ikiwa ni kweli walikuwa na malengo na ujio wako, vipi aliyekufanya kabisa, aliyekupa uhai ndani yako, akili ya kufikri na kutambua, nafasi yake kwako ni ipi?. Ni sawa kuwa Yeye ni Mungu, lakini kuwa Mungu, na wewe kumtambua kuwa Mungu haifanyi kitu kikubwa, isipokuwa kikubwa ni yale malengo ya aliyekufanya yanapokuwa yametekelezwa.

Hayo unayoyafanya, kabisa ni moja ya malengo ya Mungu, kwamba uyafanye, mbali na yale yasiyokubalika ambayo unaweza kuwa unayafanya kimakosa. Hivyo mbali na hayo mabaya, hayo mema ambayo unayafanya na kuyapata, ni sehemu halisi ya malengo ya Mungu kukuweka kwamba upate kuyafanya. Lakini hayo yanakuridhisha na kukufurahisha wewe, je unafkri kitu gani ambacho kwa dhahili wewe ukikifanya chaweza kumpendeza huyo aliyibeba dhamana yako na aliyekuleta kwa malengo makuu kabisa, ambaye anahuzunika kila siku kwa sababu tu wakati mwingi humfanyii kila anachotamani kutoka kwako?. 
Ijapokuwa huchoki kumuomba na kuhitaji msaada kwake, lakini je! kwa kuwa wajibidisha katika kumuomba ndilo jambo linalompendeza, au je ni mzazi gani ambaye anaweza kumfurahia mtoto wake kwa kuwa anamuomba tu kila siku ikiwa mtoto huyo hafanyi mengine yanaupendeza moyo wa huyo mzazi?. 
Je wewe utafurahishwa na mtoto atakayekuomba na kukulilia kila siku umsaidie katika mahitaji yake tu? Au hata kama ungekuwa na rafiki ambaye Yeye ni kukuomba tu, wala hafanyi jambo lolote linaloupendeza moyo wako, hivi kweli utapendezwa na huyo mtu?  Ikiwa hautapendezwa ndivyo ambayo Yeye aliyekuumba hapendezwi na Wewe kumuomba tu usiku na mchana kwa ajili ya mahitaji yako, bali ingefaa sana kama ungeomba pamoja kufanya kile ambacho kinaupendeza moyo wake
 Mungu kabla hajakufanya wewe, alikufanyia kwanza mahitaji utakayoyatumia, wakati wote utakaokuwepo, alipoiumba dunia na vitu vyote vilivyomo, hivi aliviumba kwa ajili ya matumizi yako. Na wa sababu hiyo kila kitu unachokiona ni kweli kuwa kipo kwa ajili ya matumizi yako, iwe vitu vya mbingu, anga na nchi vyote alivifanya kwa ajili ya matumzi yako.
Ikiwa Yeye alifanya hayo kabla ya wewe kuletwa hapo kwanza, humaanishwa kuwa, anajua mahitaji yako kuliko wewe unavyojua. Na kuna mengnie aliyoyaweka ambayo bado hujui matumizi yake lakini nayo aliyaweka kwa ajili ya wewe kuyatumia. Na kwa sababu hiyo, kila iitwapo leo kinagunduliwa kitu kipya ambacho alikifanya kwa ajili ya matumizi. 
Na mengine hadi sasa hayajagunduliwa lakini yapo, na aliyaweka kwa ajili ya matumizi yako. Ikiwa Yeye aliyajua vema mahitaji yako na akayatanguliza kwanza kabla hata ya wewe kuja, imekuwaje sasa kujisumbua sana kwa ajili ya hayo, hata kumsahau Yeye?
 Imekuwaje kutumia muda mwingi kupita kawaida kwa ajili ya kuyatafuta hayo mahitaji aliyokuwekea kuliko hata kumtafuta Yeye, au hata kumpendeza Yeye ambaye ni vyote katika vyote?
Swali hilo, ni la ufahamu tu wa kawaida, ambalo unapaswa kujiuliza, maana ikiwa Yeye aliyeingia gharama ya kufanyia hayo yote, lakini leo unajisumbua kwa ajili ya hayo aliyoyafanya tena kwa ajjili yako, lakin leo unakaa mbali naye kwa kuyatafuta na kuyasumbukia hayo, ni lazima utafakari sawasawa je! unajitendea haki? 
Tena je! Unamtendea haki? Kwa nini uwe kama mtu anayemuonea, je! Itahesabika kuwa wamuonea Yeye? Maana ijapokuwa kwa sasa itaonekana hivyo, lakini Yeye hata tahayarika kamwe, maana ameiweka siku moja tu ambayo kila jambo litafunuliwa wazi, na makusudi yake yatawekwa bayana na hapo, utajichukia wewe na hayo uliyojidhatiti kuyafanya na utayaona kuwa hayakufaa kitu ni heri ungeyaacha hata kumtafuta Yeye usiku na machana. 
Maana ijapokuwa  kwa sasa yanaonekana mbele ya macho ya watu wote kuwa yanafaa, lakini yatakuwa batili mbele ya macho ya watu wote. Maana si kwa shauli lake jinsi unavyoishi bali kwa ushupavu wa matakwa yako, tena kwa mfumo wa dunia ambao unawashurutisha wote kuenenda kwa namna hiyo.
Lakini Yeye aliyekufanya hatanyamanza kusema nawe hata wakati atakapokutwaa kwa malipo ya njia zako. Maana ijapokuwa ugumu umeonekana katikati ya watu wote lakini hataacha kuyathibitisha Maneno yake na shauli lake atalisimamisha mahali pa juu ili kila mtu atie ufahamu na ambaye hatatia ufahamu atalipwa katika hayo.
Ni vema kama leo, utaketi chini na kuyatafakari haya, maana ni kwa salama yako kuyatia katika ufahamu, na kuyapatia ufumbuzi, maana ni hakika kuwa Yeye hana furaha na Wewe katika mwenendo wa Mambo mengi, hasa kwa kutokufanya lile ambalo laufurahisha moyo wake. Lakini je ikiwa hauko hivyo, ujumbe huu wakusu wewe? Hapana wamuhusu huyo asiyefanya jambo hili kwa hakika.
Furaha ya Bwana, ni kupokea anachostahili kwa uradhi wa moyo wake, alipoumba minguni alikusudia kitu, na hicho kimefunuliwa wazi hata kwetu. Kadhalika alipoumba dunia, alikusudia kitu cha pekee, kitu hicho kilifunuliwa wazi majira na nyakati alipoichukua Nafsi aliyoifanya hapo kwanza, na ku uumba  mwili na k uiambia nafsi “kaa ndani ya huu mwili ili utawale hii dunia na vyote kwa ajili yangu”
Na kama aliiweka hiyo nafsi katika mwili ili itawale dunia kwa ajili yake aliye mfalme mkuu katika falme zote, basi hii nafsi ilipewa heshima ambayo hata malaika na wote walioko mbinguni hawakupewa. Maana malaika na jeshi lote la mbinguni humwabudu Yeye na Yeye ndiye mtawala, lakini kwa nafsi hii ya mwanadam/ya kwako aliipa heshima ya kumwabudu Yeye na kutawala dunia kwa ajili yake.
 Hata hivyo, nafsi iliasi na kujifanyia utaratibu wa kwake, na kutawala kwa ajili ya kujifurahisha katika vitu hivyo alivyovifanya kwa ajili ya nafsi ambavyo ingevitumia vema na kumletea Yeye aliyevifanya utukufu. Nafsi hii, katika uasi huo na upotofu huo kwa madaganyo makuu, ilipotoka hata kumuacha Yeye aliyeituma, ikaamua kujitia katika ubatili wa kujifurahisha kwa vitu hivi na kumpa nafasi yeye aliyeasi hapo kwanza yaani ibilisi.

Ni kweli, suruhu ya haya ilikuwa kuufuta utawala huo na hizo nafsi alizozifanya na kuzipa heshima ya kutawala kwa ajili yake. Lakini kwa jinsi alivyoipenda hiyo nafsi kupita kikomo, alivumilia na kutaka kuikomboa, akiingia gharama kila iitwapo leo ili kuirejesha katika makusudi yake. 
Lakini nafsi hii, ifananishwe na nini? Maana kama ni upotofu ulioiingia basi umeifungia mbali na makusudi ya Mungu, kwa kuwa katika kuwaza kwake, huwazi tu kujifurahisha na siyo kujifurahisha katika kumfurahisha Yeye aliyeifanya. Nafsi hii yautumia mwili uliopewa kuutumia kwa ajili ya Mungu, yautumia katika ubatili na kumsukumia mbali Mungu, kwa madanganyo na upotofu mkuu.

Lakini ingekuwa heri sana, kama utayatia moyoni haya, na kujua kuwa, Mungu anataka nini leo? Je! Si kujinyenyekesha mbele zake, kumpa sifa na heshima na utukufu anaostahili, kumfanyia ibada ya kicho cha moyo, kwa kutenga kwanza muda wa kujisongeza mbele zake, ili Yeye naye ahusiane na hii nafsi aliyoifanya? Tena ajiburudishe moyo wake kwa hiyo nafsi kwa kurejea mbele zake kila wakati, maana ikiwa aliipenda kiasi cha kuingia gharama kubwa ya ukombozi, si furaha yake sana aionapo hiyo nafsi ikijihudhulisha mbele zake, kwa kumpa utukufu kwa kuwa ndio ijala ya kazi yake na makusudi ya hayo.

Basi sasa, nakusihi katika pendo lake, uyatie haya katika fahamu zako, na nafsi yako isipotoshwe na mwili wala mfumo wa dunia hii, bali ugeuke na kurejea nyumbani katika shauli na kusudi lake, yaani kutenga muda wa kujihudhulisha mbele zake, ukiwa binafsi na katika wengi, kwa kumpa utukufu na ile tu kukaa mbele zake. 
Jambo hilo ndilo jambo analolifurahia, na hilo analitaka sana kutoka kwako! Na kwa kufanya hivyo, atakuwa Mungu kwako katika uhalisia, nawe utakuwa mtu wake, naye ataisimamia nafasi yake vema, kwa kuwa nawe uatakuwa umejidhihilisha kwake katika uhalisi. Hapo ndipo utakapovikwa utukufu kama utukufu ule wa mwanzo aliokukusudia ambao ni mkuu kuliko ule wa malaika.
Heshima yako itazidishwa katikati ya mbingu na nchi, na vitu vya mbinguni vitamtukuza Yeye kwa ajili yako, kwa kuwa alikufanya kwa ajili ya huo utukufu uletwao mbele zake uwe mkuu sana.
Jitafakari tena na uyapambanue hayo, ili angalau kwa muda udumuo, ufanye jambo la kufaa, kwa ajili yako na kulitimiza shauli la kuwepo kwako.
Mwisho:
Ikiwa utahitaji msaada wa mafafanuzi zaidi, nitumie ujumbe au nipigie, nami nitamuomba huyu aliyetia haya ndani yangu, akupe ufafanuzi huo wa kukufaa zaidi

UTUKUFU UMRUDIE YEYE ALIYETUFANYA SOTE NA VYOTE

(Ni Siri Kuu)

Mwl; Goodluck Kazili
Phone:  0765129960
Email:   gkazili@yahoo.com

JIJENGEE MTAZAMO SAHIHI ULIYE MKRISTO WA SASA


Mwl; Goodluck Kazili

KUMUHUSU MUNGU
Ni kweli kuwa kila mtu ana mtazamo wake kumhusu Mungu, tena kila mtu kuna jinsi anavyoamini juu ya Mungu kuhusu mambo mbalimbali ya kimaisha. Na hili ndilo jambo kuu ambalo unapaswa kulitazama kwa upya, mtazamo ulio nao juu ya Mungu kuhusu maisha.
Ni kweli kuwa kila mtu kuna maisha aliyoandikiwa tena aliyokusudiwa kuishi, maana kwa vyovyote vile lazima aliyekuumba kuna maisha aliyokukusudia, na hayo maisha kwako ni ya muhimu kuliko hata yale unayoyatamani.
Swali rahisi la kujiuliza ni hili, kama wewe ingekuwa ndiye uliyeumba, na hivyo ulivyoviumba vyote umevipangia maisha , je ungeviacha viishi hayo vinayoyataka au ungevilazimisha viishi yale unayoyataka?. Kama hiyo haitoshi, vipi kama yale maisha vinayoyataka haviwezi kuyapata, kisha vinakuja mbele yako kukuomba ambako ni kama kukulazimisha uvipe maisha vinayotaka mbali na yale wewe uliyoyataka viishi, je! utavijibu na kuvipa hayo maisha vinayotaka au utanyamanza ili vikose yote?
Hii ndiyo hali ambayo Mungu wetu anakutana nayo; maana kwa hakika alituumba/alikuumba na kwa namna yoyote ile kuna maisha aliyoyakusudia wewe uyaishi, lakini sisi/wewe kuna maisha ambayo unayataka kuyaishi ambayo kwa namna flani si yale ambayo Yeye anataka uishi. Na uzuri ni kuwa wewe huwezi kujifanikisha kuishi hayo maisha unayoyataka, ambapo inakulazimu kuomba msaada kwake ili akusaidie uishi maisha hayo unayoyataka na siyo yale ambayo Yeye anataka na amekupangia.
Ugumu huo umempata Mungu, kwa miaka mingi, tangu hapo mwanzo alipomuumba mtu wa kwanza, ijapokuwa wako waliotafuta maisha ambayo anapenda na anataka waishi, lakini wengi wao waliishi yale ambayo wao wanataka na wanaona yanafaa. Hivyo aliwaangamiza kwa hasira kwa kuwa asema “Nafsi yangu haitashinda na mtu kamwe”.
Jifikri kidogo maisha unayoyataka, je! Ndiyo ambayo Mungu wako anayataka uishi?, na je ndiyo yatakayoupendeza moyo wake?, maana hakukufanya ili ahuzunike bali akufurahie kwa kuishi maisha yenye heshima na utukufu kwake. Lakini hakuna anayefikri hayo, kila mtu amegeukia njia zake za maisha, na ikiwa haitoshi humuomba kila siku awafanikishe katika maisha hayo wayatakayo. Na kwa sababu hiyo, naye ameamua kunyamanza na kuwaacha kila mtu aiendee njia yake aionaye inafaa  katika maisha.
Ni wazi kuwa Mungu hajawasukumia mbali watu wake, lakini pia hayuko karibu na watu wake, kwa kuwa haiwezekanai kuwa karibu nao wasipoishi maisha anayoyataka wayaishi.
Lakini pia hawasukumii mabali kwa kuwa anawapenda ijapokuwa wanajipotosha nafsi zao kwa kuziendea njia zao wenyewe.
Ni wazi kuwa shauku ya Mungu kwetu, ni kila jambo, kila kitu, kipitachao katika maisha yetu kimletee heshima na utukufu Yeye. Na kwa maana hiyo, aliifanya nafsi iliyo kwa namna yake na kuipa uwezo wa kutawala, ili katika kutawala huko Yeye ajipatie heshima. Lakini kinyume chake amehuzunishwa sana  na hizo nafsi alizozifanya, kwa kuwa tu hazitimizi ile adhima yake aliyoikusudia katika kuzifanya kwake.
Ndugu katika Kristo Yesu, Bwana anakutaka leo ufikri jambo hili, je! Hayo maisha ulionayo, na unayoyatafuta na kumuomba kila wakati ndiyo maisha aliyoyakusudia na anayoyataka kutoka kwako?, tafakari vema uone utakalofanya, maana ijapokuwa hatakujibu katika hayo unayomuuomba lakini pia atajilipa kwa wakati aliouamru, kwa hivyo, ni heri kwako kama leo utajifkri upya juu ya Mungu wako kuhusu maisha yako.
Si kwamba anashindwa kukupa maisha hayo unayotaka , maana wote twajua kuwa kila kitu ni kazi ya neno lake tena ni kazi ya mikono yake, na vyote vimetiishwa jini ya mbingu zake na ameifunga amri ya kuihusu hii inchi katika mbingu hizo, na lolote analoamuru ndilo linalokuwa, sasa je ! kashindwa kukufanikisha kuhusu hayo unayomuuomba kila siku?, au liko tatizo gani hadi asikufanikishe? Hakika yake nayashuhudia haya katika Roho Wake Mtakaifu, kuwa ni kwa kuwa hayo unayoyaomba mengi yake siyo yale aliyoyapanga wala anayoyakusudia kwako, maana yako maisha anayoyatamani kutoka kwako, na aliyo yapanga. Hivyo hawezi kukupa yale unayoyataka wewe ikiwa wewe hutaki kutafuta yale ya kwake ambayo ameyakusudia na anayataka wewe uyaishi.
Hivyo, unao uchaguzi pia, wa kuendelea kujibidisha katika hayo yaliyo ya shauku yako, au kujifikri upya na kubainisha iliyo kweli yake kwako, na kujitia katika kujua anayoyataka kwako, na kuanza kuyaishi na kumuomba katika hayo kwanza, ili ukishafanya na kuishi hayo ayatakayo, katika hali hiyo nawe waweza kumuomba yale uyatakayo, kama ni ya kufaa, hakika yake atakupa na kukuzidisha zaidi ya hayo utakayoomba.
Lakini ikiwa utajibidisha katika hayo unayoyatamani, basi hakika yake utayakosa yote, maana Mungu si dharimu wala habahatishi, kiasi cha kufanya jambo lisilo maana, kwa kuwa kila kitu amekifanya kwa kusudi, tena katika kila kazi aliyoifanya aliikusudia imletee heshima na utukufu, hivyo kusudi hilo haliendi bure. Ikiwa wewe uliyemhusika hutataka kulitimiza, basi hakika yake ni kuwa hata wewe hautafanikiwa katika hayo unayoyatafuta na kumuomba kila siku, tena ijapokuwa aweza kukuacha ukafanikiwa katika hayo lakini bado atakukondesha roho/nafsi yako, na haitakuwa na raha, tena atakuhukumu kwa siku ile aliyoiweka kuzihukumu nafsi zote za wanadamu.
Ndugu nakuhimiza na kukusihi katika Kristo, kuona kuwa imetosha, kumtia Mungu wetu katika hali ya kutokutufurahia, maana asema “ nafsi yangu ingezimia kwa hizo nafsi nilizozifanya” kwa nini kumtia Mungu wetu katika uchungu kwa nafsi zetu. Je! gharama aliyoingia ya kutukomboa katika uteka ambao tusingeweza kujitoa haitoshi sisi kufkri? Tena ikiwa hiyo haitoshi ya kutukombao akatupa nguvu na kutupa urithi wa yale tuliyokuwa hatusitahili tena kuyarithi kwa jinsi tulivyokuwa tumeasi, lakini kwa pendo na neeama tena na rehema zake akatukirimia nafasi hiyo tena.  Je! Si ingekuwa heri leo kama ukiyatia haya katika moyo wako na kuyafkri kwa kina,  tena kuchukua hatua ya kumwendee Yeye na kutaka kwake kujua maisha anayoyataka kwako, ili sasa upate kuyaishi na kuifurahisha Nafsi yake?. Maana hakuna jambo lililo kubwa kwake zaidi ya nafsi yako kuhudhulia mbele zake na kumfanyia ibada.
Lakini je! nafsi ya mtu ikiwa yasema yampenda Mungu, na huku wajibidisha katika mambo yako na yale uyatakayo na kuyaona kuwa yanafaa,
 je! Mungu ataifurahia nafsi hiyo, maana nafsi ya Mtu ndicho kitu pekee kinachoweza kumfurahisha Mungu, ikiwa tu kitahudhulia mbele yake na kumuabudu na kumpa utukufu.
 Kadhalika kitu pekee kinachoweza kumkasirisha Mungu sana ni nfasi ya mtu kutokuhudhulia mbele yake na kufanya ibada, tena kutokumpa utukufu Yeye anayestahili ambaye aliiumba nafsi ili ifanye hayo.
Ni kweli kuwa maisha pia yana namna ya mwili, ambayo ina uhitaji mkubwa tu wa vitu mbalimbali, ambavyo hivyo vyatukimbiza sana. Je! kwani aliyeumba hakujua kuwa hayo yote tunayahitaji, au ni nani aliyeyaweka hayo?  je! kuna mtu aliyejiamuru kula, kuna mtu aliyefanya hitaji lolote katika mwili wake, si Mungu aliyeyaweka yote? Na ikiwa Yeye ndiye aliyeyaweka yote, basi kwa hakika kwa kila maisha aliyoyapanga basi ameweka pia mahitaji hayo katika utimilifu wake. Maana dunia nzima iliumbbwa kwa ajili ya matumizi ya huo mwili, maana alipoipanda bustani ya edeni hayo yalikuwa mahitaji ya mwili, tena alimuwekea uzuri wa kila namna maana Yeye kama Muumbaji alijua tena anajua mahitaji ya hicho alichokiumba kwa kuwa kila lionekanalo kuwa hitaji Yeye ndiye aliyeliweka ndani ya huyo mtu.
Kwa kuwa huo ndio ukweli ulio halisi, je! Ni sawa kujisumbua katika hayo hadi kumsahau Yeye? Na hata tunapomukumbuka, tunamukumbuka kwa kutaka atusaidie na kufanya hayo ambayo tunayataka?. Ikiwa iko hivyo, maana na tafsiri ya hayo, ni kuwa tunamlazimisha afanye, maana ikiwa Yeye ametutaka tuishi maisha flani, nasi twataka mengine na kuenda kwake kwa kuomba afanye vile tutakavyo, hilo humaanisha kuwa twamlazimisha. Na kwa jinsi mashauri yake yasivyopingika, twajikosesha wenyewe na kujilemea, maana ni afadhali yetu kama tungejitia chini ya kongwa lake na kuyataka hayo maisha ayatakayo sisi tuishi, ingekuwa salama na amani kwetu.
Maana tujapojibidisha katika hayo, hakika hatutayapata, na hata kama tutayapata hakika tutaangamia. Ya nini kuyakosa yote, tena ya nini kuangamia katika mambo ambayo tulipewa lakini tu twashinda kufuata utaratibu wa Yeye aliyetufanya na kuviumba vitu vyote.
Katika hayo yote, ujumbe huu hauwezi kwenda bure! Maana ikiwa Roho wake ajibidisha kututia katika kweli yote, ili kusudi nasi tulio kuwa tumesukumiwa mbali, tena watu tusiomjua Mungu, wala kuwa na ushirika nae, kwa nini nafasi hii tusiyoitafuta, tusiitumie vizuri? Maana ijapokuwa twaubatilisha ukweli, lakini iko wazi kuwa sisi tu watu tu, tuliopata neema maana hapo kwanza hatukusitahili, hata kumkaribia Mungu, wala hakuna maisha yaliyoamriwa kwetu dhahili ambayo tungeweza hata kujibidisha na kuyapata. Lakini kwa jinsi wema wake na pendo lilivyokuwa kuu kwetu, lilimbidisha hata kujitoa nafsi yake kuyakabili mauti naam mauti ya msalaba ili tulio mbali tuletwe karibu, tena tusioweza kukaribia mahali pake tukaribie ili tumletee heshima na utukufu anaostahili kwa hiyo kazi yake.
Twajikosesha sana, kutokujibidihsa katika mapenzi yake, na hayo maisha anayoyataka kwetu, maana haya tuyatafutayo ni ubatili, tena usiofaa kitu katika ulimwengu huu wala ule ujao. Inafaa nini tena, katika haya maisha yako, je! Si kujisogeza kwake kila wakati na kumpa heshima na utukufu, kwa kuimimina nafsi yako mbele zake na kumuandama Yeye katika mambo yote. Maana asemapo “nami nitawapa raha nafsini mwenu”, ni hakika kuwa ni kwa kujibidisha katika kumtafuta Yeye ili nafsi yako ipate hiyo raha.
Haizuiliwi kutafuta mahitaji yako katika mwili, lakini haifai kuyatafuta yale yaliyo nje ya mapenzi yake, yale yaliyo nje ya anayoyataka kwako. Maana ni hakika kuwa Yeye apenda ufanikiwe sana, lakini si nje ya yale ayatakayo kwako. Ikiwa unaweza kuyajua hayo ayatakayo basi wewe utakuwa aliyefanikiwa sana, maana ijapokuwa tunahitaji sana, lakini tusiyoyajua kuwa tunayahitaji ni mengi tena ndiyo yenye maana sana kuliko hayo.
Mwenyewe amebainisha wazi kuwa “ mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?” tena “itamfaidia nini mtu akiupata ulimwengu na mambo yake yote lakini akapata hasara ya nafsi yake?” yafkri hayo kwa undani ujue hakika yake, maana ikiwa nafsi yako haitaokoka mpaka mwisho, basi ni heri usingelizaliwa.
Maana ijapokuwa haiwezekani kuupata ulimwengu wote na mamabo yake yote, lakini asema hata kama ingekuwa hivyo, bado thamani yake hailingani na nafsi yako. Je ikiwa hayo yangetiwa moyoni mwako leo, utaendelea kujibidisha sana katika mambo hayo ya ulimwengu ikiwa hujajihakiki nafsi yako kuwa salama? Maana kuangamia kwa nafsi ni ile kutokuwa na uhusiano mwema na Mungu, tena kutokutimiza Yale ambayo nafsi hiyo imeaandikiwa.
Pamoja na mambo yote, haitafaa lolote kama nafsi yako haitafika mwisho mzuri, maana ijapokuwa mbingu na nchi zitatoweshwa lakini nafsi yako haitapita kamwe, hata itakapotelemshwa kwenye mauti au kuingizwa katika mbingu mpya na nchi mpya. Maana twajua hakika kuwa, nafsi ya mtu haitapata kifo hiki tukijuacho katika mwili, maana kinachokufa ni mwili na siyo nafsi. Maana kipo kifo ambacho hicho huuhusu mwili, lakini pia yako mauti ambayo hayo huihusu nafsi. Maana kuna tofauti kati ya mauti na kifo, kwa kuwa kifo ni kwa ajili ya mwili na mauti ni kwa ajili ya nafsi. Mauti ni mateso na maumivu, wakati kifo huhusu mwisho wa uhai.
Yafikri haya sawasawa, maana ikiwa Roho Mtakatifu amekushirikisha wewe,  hailengi mwili wako hata kidogo, maana mwili unaweza kuyadharau wala usione kuwa kitu cah kufaa, lakini mambo haya yanailenga nafsi yako ambayo ndiyo yenye thamani kuliko vitu vyote, maana katika haya nafsi yako, itafunguka, na kujua uhalisia wake.
Maana asema “ nia ya mwili ni mauti lakini nia ya roho/nafsi ni uzima na amani”, je! Mwili huo utayafikri haya na kuyabaini au utayaona kuwa kitu? Ingekuwa heri kama nafsi yako itapambazuka na kuyafikri haya, ili kujitia ufahamu katika Roho Mtakatifu, uliyeshirikishwa.
Hata hivyo, Mungu ni mwaminifu kwa watu wake, maana walio wake awajua, na tena waisikia sauti yake, hao ndio walioitwa na Yeye katika wito wa msalaba, akawakaribisha kwake kwa kuwa walipoitwa waliitika, nao walitamani kukombolewa kwa kuwa walichoshwa na uteka waliokuwa nao. Ikiwa Mungu wa mbinguni amekupa neema hiyo, ni hakika kuwa haya utayatia katika moyo wako na kuyaamua vema kwa ajili ya utukufu wake Mwenyewe, ila kwa njia hiyo upate kujibidisha katika kuhudhulia mbele zake, ili ayamimine mapenzi yake ndani ya nafsi yako na upate kufanana naye na kumfaa zaidi kwa kila neno, tendo na uwazalo.
Katika yote, Roho wake Mtakatifu, ajifunue wazi, na kuyathibitisha yaliyo mapenzi ya Baba, katika Mwana, ili nasi tulio nafsi zake, tupate kuyapokea na kujitia katika kweli yake yote.
Hata hivyo yafaa sana ukiyafikri na kuyabaaini haya, ambayo kwa hakika yanafaa sana, na ni kweli itokayo kwa Mungu ambayo kwa Neema ya Kristo, Roho wake Mtakatifu ametushirikisha. Kama alivyoyamimina ndani yangu, nami nayapokea kutoka kwake, na kumlilia sana anisaidie niweze kuyatia katika fahamu zangu na kuyatekeleza bila upungufu wowote. Mambo haya ni matamu sana, tena yanatia uchungu sana kwa kuwa, kwa hakika huyo Mungu wetu ni wa ajabu sana, tujapomfikri katika hayo hakika hatutamuelewa wazi jinsi alivyotufadhili na kutupenda.

Mwl; Goodluck Kazili
0765 129 960
kazili.blogspot.com

Ijumaa, 4 Machi 2016

MTAZAMO CHANYA UNAOZALISHA (POSTIVE AND REPRODUCTIVE VIEW)

MTAZAMO CHANYA UNAOZAA

Maswali 2 muhimu ya kujiuliza

1. Una nini ( what do you have) swali hilo aliulizwa Musa
2. unaona nini (waha do you see) swali hilo aliulizwa Yeremia

unachoona ndio hatua ya kwanza ya mafanikio yoyote, maana huwezi kufanikiwa nje ya kile unachoona

ulichonacho, ni nyenzo ya kufikia maono, unacho ili kikusukume kukupeleka kwenye maono yako

kutambua ulichonacho nia matokeo ya mahitaji ya maono. maono yakiwa ndani yako hudai, na yanapodai ndipo nyenzo iliyoko ndani yako inapojiibua ili kuyafanya hayo maono yafikiwe

Nikuache na changamoto hii

Unaona nini (what do you see)
Una nini ( what do you see)


Jumatatu, 29 Februari 2016

THAMANI YA MTU WA NDANI (NAFSI)

SK-Siri Kuu
 

THAMANI YA MTU WA NDANI (NAFSI)

Na Mwl; Goodluck Kazili

"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?. (Mathayo 16:26)
Hakuna kitu chenye thamani katika ulimwengu huu, kama nafsi ya mtu. Nafsi yako ndicho kitu chenye thamani kuliko chochote unachokijua katika ulimwengu huu, ndiyo sababu Yesu aliuliza au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?. Je! ulimwengu mzima thamani yake inalingana na thamani ya nafsi yako? hapana haiwezi kufikia. Na hivyo hakuna chenye thamani kuliko nafsi yako.

Hata hivyo ajabu ni kwamba, mtu mwenyewe haithamani hiyo nafsi yake bali anathamini vitu ambavyo nafsi ilipewa ili kuvitumia. mfano mtu hataki kuokoka kwa madai kuwa atashindwa kuifaidi dunia na raha yake. Mtu kama huyu, tatzo lake ni ufahamu tu wa kutokujua thamani ya kila kimoja na matumizi yake na sababu ya kuwekwa hivyo vitu.

Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa kuna utu wa ndani na utu wa nje. tena utu wa nje uliumbwa kwa ajili ya utu wa ndani, kama tu nyenzo ambayo mtu wa ndani anapewa ili atumie kwa matumizi yake.


NI SIRI KUU

Na Mwl; Goodluck Kazili

"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)


"A work shop of Holy Sprit in man is mind"

"A work shop of devel in man is mind"

"A work shop of mind in man is brain"

If you fail to protect and control you're mind, you can not be you, you will be one of someone,

Jumatano, 24 Februari 2016

POWER OF VISION (NGUVU YA MAONO)


SK-Siri Kuu


 


POWER OF VISION (NGUVU YA MAONO)
Na Mwl; Goodluck Kazili 
“Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na chi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba, kwa kuwa ndivyoilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Dondoo muhimu za kujifunza kuhusu Maono (kwa ufupi)
Ø  Tafsiri ya maono
Ø  Maono kuhusu maisha
Ø  Nvugu ya maono
Ø  Namna ya kuwa na maono
Ø  Funguo za maono
Ø  Kiapo katika maono
Ø  Mipango ya maono
Ø  mwisho
TAFSIRI YA MAONO
Maono ni picha ya mbele kuhusu jambo/ kitu/hali/ inayopigwa na kudhihilishwa kabla, ili kutengeneza mazingra ya kufanikiwa kwake
Maono yanaeleza jambo lisilokuwapo bado kwa wakati uliopo sasa lakini lipo mbele, hivyo ile picha inayopigwa na kuletwa kwa mtu ili afanye jambo kwa ajili ya kufanikiwa kwake.
Hata hivyo maono yapo ya aina nyingi, lakini maana hiyo inagusa maono karibu ya namna zote. Katika somo hili, maono yanayolengwa ni yale yanayohusu maisha ya mtu.
MAONO KUHUSU MAISHA
Kila mtu katika maisha ana viengele 4 vinavyogusa maisha yake, vitu hivyo ni Yeye kuhusiana na Mungu, uchumi, afya na familia.
Hivyo, mtu analazimika kuwa na maono yanayogusa mambo hayo manne . kwa ulazima huo, binafsi ni lazima uwe na:-
1.       Maono ya Kiutumishi (spritual Vision)
2.       Maono ya kiuchumi (economical vision)
3.       Maono ya kifamilia (family vision)
4.       Maono ya kiafya (health vision)

Hata hivyo, haiwezekani hayo yote kuwa maono halisi ndani yako kisha ukayafanikisha vema. Unapaswa kuwa na maono makuu, ambayo huwa ni moja.  Unakuwa na maono ambayo ni makuu (main vision), kisha unakuwa una maono yaliyo chini ya maono makuu (sub vision).
Mfano mimi Goodluck Kazili maono yangu ni haya “Kumtumikia Mungu kwa kiwango cha juu cha kwanza, katika yote, kwa vyote, sawa na mapenzi yake” (to serve the LORD GOD to the best level of all, with all in His will). Kwangu haya ndiyo maono makuu (main vision), lakini chini yake nina maono mbali mbali ya kiuchumi, ya kiafya, na ya kifamilia. Mfano katika maono ya uchumi, nina picha (maono) ya kuwa na shule pamoja na chuo, tena nina picha (maono) ya kuwa na miradi kadhaa ya fedha, n.k.
Hivyo ninachofanya ni lazima haya maono yawe chini ya maono makuu ambayo ni ya kumtumikia Mungu. Hivyo, pamoja na kuwa nitamiliki chuo, shule, miradi, bado itakuwa sehemu ya utumishi wangu kwa Mungu ili kuwa wa juu na wa kwanza kwa vyote na katika vyote sawa na mapenzi yake Mungu.
NGUVU YA MAONO
Huwezi kufanikiwa vema katika jambo lolote kubwa usipokuwa na maono nalo. Maono yenyewe kama yalivyo ni nguvu, tena ni imani, tena ni ulinzi, tena kichocheo (catalyst), ni Zaidi ya jitihada unazoweza kuzifanya katika jambo lolote. Maano yanaelezea na yanalihakiki jambo kuanzia mwisho wake kuja mwanzo wake, hivyo unaona unakoenda na jinsi unavyofanikiwa hata kabla hujafanikiwa wala kufikia.
Ni muhimu kufahamu kuwa kazi ya akili ni kuutumia ubongo kutekeleza wazo au adhimio lolote lililo ndani ya mtu liwe baya au jema. Akili inatengeneza mbinu mbalimbali kwa kuutumia ubongo ili kufanikisha adhima yoyote ile iliyoadhimiwa na mtu. Hivyo ukiwa na maono, yale maono mbali na kuhifadhiwa sehemu nyingine kama moyoni, pia hukaa kwenye akili, hivyo akili wakati wote hutumia ubongo kufanya namna mbali mbali ili kutekeleza hilo ambalo ndiyo maono.
Pia kinyume chake ni kuwa kama hauna maono, unaifanya akili yako itekeleze kila jambo linalokuja ndani yake karibu kila siku. Mfano mtu akikusema vibaya, kama huna maono na kama hayana nguvu ndani yako, unaifanya akili yako kutwa nzima ishinde inatafuta namna ya kufanya ili kutekeleza hilo la huyo aliyekusema. Kama ni jambo ambalo akili itashindwa kupata suruhu, ina maana akili haitaridhika na itapelekea kuliwaza kila wakati na kukwama katika mambo mengine.
NAMNA YA KUWA NA MAONO
Huwezi kuwa na maono nje yako, hata Mungu hawezi kukuletea maono nje yako, ikimaanishwa kuwa ni lazima yawe maono ambayo kwa kweli ndiyo wewe, na ndivyo ulivyo. Kuna maono ya kuletewa na kuna maono ya kutengeneza wewe mwenyewe, na mara nyingi ukitengeneza maono wewe mwenyewe kwa namna ya kawaida utayaacha na huwa yatabadilika.
Mbali na yale ya kuletewa, wewe unaweza kuwa na maono ambayo yanazaliwa ndani yako. Hilo si jambo la kufikri ila linazaliwa kama wewe ulivyozaliwa. Maana kila mtu ndani yake kuna maono, ambayo mara mnyingi hayako wazi kwake, hivyo ni kazi ya kuyatambua na kuyajua.  Hii ni hatua ambayo mtu anaingia kwa makusudi na kwa dhamili hatua hii ni hatua ya ufunuo, Kimungu yaani unafunuliwa kilichoko ndani yako, hivyo unakitambua na kukielewa. (vision recognition and understanding)
Ili kutambua maono, ni lazima uwejifahamishe wewe mwenyewe kukuhusu, maana maono yako ndiyo wewe mwenyewe. Hivyo ukishaweza kujijua vema ulivyo, undani wako usiobadilika ambao ndiyo asili yenyewe hapo unaweza kutambua maono yaliyoko ndani yako. Na kwa kuwa tumetofautiana uwezo wa utambuzi, unweza kuomba usaidizi ili kutambua maono yako, ikiwa ni wewe mwenyewe kwa Mungu au mtu kukusaidia.
FUNGUO ZA MAONO          
Hapo kwenye maono, kuna vitu ambavyo vinashika hayo maono ambavyo ni lazima vijulikane na tena uwe navyo wakati wote ili viwe kwenye akili itumie ubongo wakati wote kuvitekeleza.
Nitumie mfano wangu:
Maono yangu ni “kumtumikia Mungu, kwa kiwango cha juu, cha kwanza, katika vyote na kwa vyote sawa na mapenzi yake” kwa kingereza “to serve the LORD GOD, to the best level of all with all to His will”
Katika maono haya, funguo zake ziko 5
1. Kumtumika Mungu (serving Lord God)
2. Kiwango cha juu na cha kwanza (best level)
3. Katika yote (of all)
4. Kwa vyote (with all)
5. Mapenzi yake (His will)
Kwa hiyo, huu unakuwa ndio msingi wangu wa maonowa vitu ninavyo paswa kuvitekeleza wakti wote

KIAPO/ COMMITMENT
Ili uweze kufanikiwa katika maono yako ni lazima uwe na kiapo juu yako mwenyewe.  Mfano mimi ili kufikia maono yangu kwa jinsi yalivyo na funguo zake, nimejiapia kuwa “Goodluck Kazili katika kila jambo ni lazima nimtumikie Mungu, tena kwa kiwango cha juu na cha kwanza, tena sawa na mapenzi yake”
Kama unavyojua kiapo ni kitu ambacho kikishakuwa ndani yako, huna uhuru wa kuchagua kutekeleza au kutokutekeleza. Hivyo kila wakati utajikuta unakumbuka ufanyapo jambo na kuliangalia kama liko sawa na maono yako tena kama linaongeza jambo kwenye maono yako
MPANGO MKAKATI (STRATEGIC PLAN)
Hii ni mipango tofautitofauti inayohusu maono na inayopaswa kutekelezwa ambayo kufanikiwa kwake ndio kufikiwa kwa maono. Hapa ndipo akili inapofanya kazi zaidi kufikia maono ambayo yako ndani yako.

MWISHO
Wakati wote kumbuka kuwa , kama huna maono utatumikia maono ya watu wenginge. Na ukweli ni kuwa hukuzaliwa ili utumikie maono ya watu wengine, lakini kama huna lazima utumikie tu, aidha kwa kujua au kwa kutokujua.
Pia maono yanakua, hivyo upana wa maono yako kwa sasa au ya kipindi flani hayatabaki na ukubwa au upana uleule. Maana kwa kadri wewe unavyokua ndivyo na Yeneyewe yanavyokua.
Maono makuu yanapaswa kuwa ya kumtumikia Mungu, na mengine yote kuwa madogo.
Mungu wa mbinguni akujalie kuwa na maono yanayoujenga ufalme wake.

Mwl. Goodluck kazili
Email: gkazili@yahoo.com
Phone: 0765 129 960
Blog:  Kazili.blogspot.com





Kunihusu

Picha yangu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Tafuta katika Blogu Hii