KUMUHUSU
MUNGU
Ni
kweli kuwa kila mtu ana mtazamo wake kumhusu Mungu, tena kila mtu kuna jinsi
anavyoamini juu ya Mungu kuhusu mambo mbalimbali ya kimaisha. Na hili ndilo
jambo kuu ambalo unapaswa kulitazama kwa upya, mtazamo ulio nao juu ya Mungu
kuhusu maisha.
Ni
kweli kuwa kila mtu kuna maisha aliyoandikiwa tena aliyokusudiwa kuishi, maana
kwa vyovyote vile lazima aliyekuumba kuna maisha aliyokukusudia, na hayo maisha
kwako ni ya muhimu kuliko hata yale unayoyatamani.
Swali
rahisi la kujiuliza ni hili, kama wewe ingekuwa ndiye uliyeumba, na hivyo
ulivyoviumba vyote umevipangia maisha , je ungeviacha viishi hayo vinayoyataka
au ungevilazimisha viishi yale unayoyataka?. Kama hiyo haitoshi, vipi kama yale
maisha vinayoyataka haviwezi kuyapata, kisha vinakuja mbele yako kukuomba
ambako ni kama kukulazimisha uvipe maisha vinayotaka mbali na yale wewe
uliyoyataka viishi, je! utavijibu na kuvipa hayo maisha vinayotaka au
utanyamanza ili vikose yote?
Hii
ndiyo hali ambayo Mungu wetu anakutana nayo; maana kwa hakika
alituumba/alikuumba na kwa namna yoyote ile kuna maisha aliyoyakusudia wewe
uyaishi, lakini sisi/wewe kuna maisha ambayo unayataka kuyaishi ambayo kwa
namna flani si yale ambayo Yeye anataka uishi. Na uzuri ni kuwa wewe huwezi
kujifanikisha kuishi hayo maisha unayoyataka, ambapo inakulazimu kuomba msaada
kwake ili akusaidie uishi maisha hayo unayoyataka na siyo yale ambayo Yeye
anataka na amekupangia.
Ugumu
huo umempata Mungu, kwa miaka mingi, tangu hapo mwanzo alipomuumba mtu wa
kwanza, ijapokuwa wako waliotafuta maisha ambayo anapenda na anataka waishi,
lakini wengi wao waliishi yale ambayo wao wanataka na wanaona yanafaa. Hivyo
aliwaangamiza kwa hasira kwa kuwa asema “Nafsi yangu haitashinda na mtu kamwe”.
Jifikri
kidogo maisha unayoyataka, je! Ndiyo ambayo Mungu wako anayataka uishi?, na je
ndiyo yatakayoupendeza moyo wake?, maana hakukufanya ili ahuzunike bali
akufurahie kwa kuishi maisha yenye heshima na utukufu kwake. Lakini hakuna
anayefikri hayo, kila mtu amegeukia njia zake za maisha, na ikiwa haitoshi
humuomba kila siku awafanikishe katika maisha hayo wayatakayo. Na kwa sababu
hiyo, naye ameamua kunyamanza na kuwaacha kila mtu aiendee njia yake aionaye
inafaa katika maisha.
Ni
wazi kuwa Mungu hajawasukumia mbali watu wake, lakini pia hayuko karibu na watu
wake, kwa kuwa haiwezekanai kuwa karibu nao wasipoishi maisha anayoyataka
wayaishi.
Lakini
pia hawasukumii mabali kwa kuwa anawapenda ijapokuwa wanajipotosha nafsi zao
kwa kuziendea njia zao wenyewe.
Ni
wazi kuwa shauku ya Mungu kwetu, ni kila jambo, kila kitu, kipitachao katika
maisha yetu kimletee heshima na utukufu Yeye. Na kwa maana hiyo, aliifanya
nafsi iliyo kwa namna yake na kuipa uwezo wa kutawala, ili katika kutawala huko
Yeye ajipatie heshima. Lakini kinyume chake amehuzunishwa sana na hizo nafsi alizozifanya, kwa kuwa tu
hazitimizi ile adhima yake aliyoikusudia katika kuzifanya kwake.
Ndugu katika Kristo Yesu, Bwana
anakutaka leo ufikri jambo hili, je! Hayo maisha ulionayo, na unayoyatafuta na
kumuomba kila wakati ndiyo maisha aliyoyakusudia na anayoyataka kutoka kwako?,
tafakari vema uone utakalofanya, maana ijapokuwa hatakujibu katika hayo
unayomuuomba lakini pia atajilipa kwa wakati aliouamru, kwa hivyo, ni heri
kwako kama leo utajifkri upya juu ya Mungu wako kuhusu maisha yako.
Si kwamba anashindwa kukupa
maisha hayo unayotaka , maana wote twajua kuwa kila kitu ni kazi ya neno lake
tena ni kazi ya mikono yake, na vyote vimetiishwa jini ya mbingu zake na
ameifunga amri ya kuihusu hii inchi katika mbingu hizo, na lolote analoamuru
ndilo linalokuwa, sasa je ! kashindwa kukufanikisha kuhusu hayo unayomuuomba
kila siku?, au liko tatizo gani hadi asikufanikishe? Hakika yake nayashuhudia
haya katika Roho Wake Mtakaifu, kuwa ni kwa kuwa hayo unayoyaomba mengi yake
siyo yale aliyoyapanga wala anayoyakusudia kwako, maana yako maisha
anayoyatamani kutoka kwako, na aliyo yapanga. Hivyo hawezi kukupa yale
unayoyataka wewe ikiwa wewe hutaki kutafuta yale ya kwake ambayo ameyakusudia
na anayataka wewe uyaishi.
Hivyo, unao uchaguzi pia, wa
kuendelea kujibidisha katika hayo yaliyo ya shauku yako, au kujifikri upya na
kubainisha iliyo kweli yake kwako, na kujitia katika kujua anayoyataka kwako,
na kuanza kuyaishi na kumuomba katika hayo kwanza, ili ukishafanya na kuishi
hayo ayatakayo, katika hali hiyo nawe waweza kumuomba yale uyatakayo, kama ni
ya kufaa, hakika yake atakupa na kukuzidisha zaidi ya hayo utakayoomba.
Lakini ikiwa utajibidisha
katika hayo unayoyatamani, basi hakika yake utayakosa yote, maana Mungu si dharimu
wala habahatishi, kiasi cha kufanya jambo lisilo maana, kwa kuwa kila kitu amekifanya
kwa kusudi, tena katika kila kazi aliyoifanya aliikusudia imletee heshima na
utukufu, hivyo kusudi hilo haliendi bure. Ikiwa wewe uliyemhusika hutataka
kulitimiza, basi hakika yake ni kuwa hata wewe hautafanikiwa katika hayo
unayoyatafuta na kumuomba kila siku, tena ijapokuwa aweza kukuacha ukafanikiwa
katika hayo lakini bado atakukondesha roho/nafsi yako, na haitakuwa na raha,
tena atakuhukumu kwa siku ile aliyoiweka kuzihukumu nafsi zote za wanadamu.
Ndugu nakuhimiza na kukusihi
katika Kristo, kuona kuwa imetosha, kumtia Mungu wetu katika hali ya
kutokutufurahia, maana asema “ nafsi yangu ingezimia kwa hizo nafsi nilizozifanya”
kwa nini kumtia Mungu wetu katika uchungu kwa nafsi zetu. Je! gharama
aliyoingia ya kutukomboa katika uteka ambao tusingeweza kujitoa haitoshi sisi
kufkri? Tena ikiwa hiyo haitoshi ya kutukombao akatupa nguvu na kutupa urithi
wa yale tuliyokuwa hatusitahili tena kuyarithi kwa jinsi tulivyokuwa tumeasi,
lakini kwa pendo na neeama tena na rehema zake akatukirimia nafasi hiyo tena. Je! Si ingekuwa heri leo kama ukiyatia haya
katika moyo wako na kuyafkri kwa kina,
tena kuchukua hatua ya kumwendee Yeye na kutaka kwake kujua maisha
anayoyataka kwako, ili sasa upate kuyaishi na kuifurahisha Nafsi yake?. Maana
hakuna jambo lililo kubwa kwake zaidi ya nafsi yako kuhudhulia mbele zake na
kumfanyia ibada.
Lakini je! nafsi ya mtu ikiwa
yasema yampenda Mungu, na huku wajibidisha katika mambo yako na yale uyatakayo
na kuyaona kuwa yanafaa,
je! Mungu ataifurahia nafsi hiyo, maana nafsi
ya Mtu ndicho kitu pekee kinachoweza kumfurahisha Mungu, ikiwa tu kitahudhulia
mbele yake na kumuabudu na kumpa utukufu.
Kadhalika kitu pekee kinachoweza kumkasirisha
Mungu sana ni nfasi ya mtu kutokuhudhulia mbele yake na kufanya ibada, tena
kutokumpa utukufu Yeye anayestahili ambaye aliiumba nafsi ili ifanye hayo.
Ni kweli kuwa maisha pia yana
namna ya mwili, ambayo ina uhitaji mkubwa tu wa vitu mbalimbali, ambavyo hivyo
vyatukimbiza sana. Je! kwani aliyeumba hakujua kuwa hayo yote tunayahitaji, au
ni nani aliyeyaweka hayo? je! kuna mtu
aliyejiamuru kula, kuna mtu aliyefanya hitaji lolote katika mwili wake, si
Mungu aliyeyaweka yote? Na ikiwa Yeye ndiye aliyeyaweka yote, basi kwa hakika
kwa kila maisha aliyoyapanga basi ameweka pia mahitaji hayo katika utimilifu
wake. Maana dunia nzima iliumbbwa kwa ajili ya matumizi ya huo mwili, maana alipoipanda
bustani ya edeni hayo yalikuwa mahitaji ya mwili, tena alimuwekea uzuri wa kila
namna maana Yeye kama Muumbaji alijua tena anajua mahitaji ya hicho
alichokiumba kwa kuwa kila lionekanalo kuwa hitaji Yeye ndiye aliyeliweka ndani
ya huyo mtu.
Kwa kuwa huo ndio ukweli ulio
halisi, je! Ni sawa kujisumbua katika hayo hadi kumsahau Yeye? Na hata
tunapomukumbuka, tunamukumbuka kwa kutaka atusaidie na kufanya hayo ambayo
tunayataka?. Ikiwa iko hivyo, maana na tafsiri ya hayo, ni kuwa tunamlazimisha
afanye, maana ikiwa Yeye ametutaka tuishi maisha flani, nasi twataka mengine na
kuenda kwake kwa kuomba afanye vile tutakavyo, hilo humaanisha kuwa twamlazimisha.
Na kwa jinsi mashauri yake yasivyopingika, twajikosesha wenyewe na kujilemea,
maana ni afadhali yetu kama tungejitia chini ya kongwa lake na kuyataka hayo
maisha ayatakayo sisi tuishi, ingekuwa salama na amani kwetu.
Maana tujapojibidisha katika
hayo, hakika hatutayapata, na hata kama tutayapata hakika tutaangamia. Ya nini
kuyakosa yote, tena ya nini kuangamia katika mambo ambayo tulipewa lakini tu
twashinda kufuata utaratibu wa Yeye aliyetufanya na kuviumba vitu vyote.
Katika hayo yote, ujumbe huu
hauwezi kwenda bure! Maana ikiwa Roho wake ajibidisha kututia katika kweli
yote, ili kusudi nasi tulio kuwa tumesukumiwa mbali, tena watu tusiomjua Mungu,
wala kuwa na ushirika nae, kwa nini nafasi hii tusiyoitafuta, tusiitumie
vizuri? Maana ijapokuwa twaubatilisha ukweli, lakini iko wazi kuwa sisi tu watu
tu, tuliopata neema maana hapo kwanza hatukusitahili, hata kumkaribia Mungu,
wala hakuna maisha yaliyoamriwa kwetu dhahili ambayo tungeweza hata kujibidisha
na kuyapata. Lakini kwa jinsi wema wake na pendo lilivyokuwa kuu kwetu,
lilimbidisha hata kujitoa nafsi yake kuyakabili mauti naam mauti ya msalaba ili
tulio mbali tuletwe karibu, tena tusioweza kukaribia mahali pake tukaribie ili
tumletee heshima na utukufu anaostahili kwa hiyo kazi yake.
Twajikosesha sana,
kutokujibidihsa katika mapenzi yake, na hayo maisha anayoyataka kwetu, maana
haya tuyatafutayo ni ubatili, tena usiofaa kitu katika ulimwengu huu wala ule
ujao. Inafaa nini tena, katika haya maisha yako, je! Si kujisogeza kwake kila
wakati na kumpa heshima na utukufu, kwa kuimimina nafsi yako mbele zake na
kumuandama Yeye katika mambo yote. Maana asemapo “nami nitawapa raha nafsini
mwenu”, ni hakika kuwa ni kwa kujibidisha katika kumtafuta Yeye ili nafsi yako
ipate hiyo raha.
Haizuiliwi kutafuta mahitaji
yako katika mwili, lakini haifai kuyatafuta yale yaliyo nje ya mapenzi yake,
yale yaliyo nje ya anayoyataka kwako. Maana ni hakika kuwa Yeye apenda
ufanikiwe sana, lakini si nje ya yale ayatakayo kwako. Ikiwa unaweza kuyajua
hayo ayatakayo basi wewe utakuwa aliyefanikiwa sana, maana ijapokuwa tunahitaji
sana, lakini tusiyoyajua kuwa tunayahitaji ni mengi tena ndiyo yenye maana sana
kuliko hayo.
Mwenyewe amebainisha wazi kuwa
“ mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?” tena “itamfaidia nini mtu akiupata
ulimwengu na mambo yake yote lakini akapata hasara ya nafsi yake?” yafkri hayo
kwa undani ujue hakika yake, maana ikiwa nafsi yako haitaokoka mpaka mwisho,
basi ni heri usingelizaliwa.
Maana ijapokuwa haiwezekani
kuupata ulimwengu wote na mamabo yake yote, lakini asema hata kama ingekuwa
hivyo, bado thamani yake hailingani na nafsi yako. Je ikiwa hayo yangetiwa
moyoni mwako leo, utaendelea kujibidisha sana katika mambo hayo ya ulimwengu
ikiwa hujajihakiki nafsi yako kuwa salama? Maana kuangamia kwa nafsi ni ile
kutokuwa na uhusiano mwema na Mungu, tena kutokutimiza Yale ambayo nafsi hiyo
imeaandikiwa.
Pamoja na mambo yote, haitafaa
lolote kama nafsi yako haitafika mwisho mzuri, maana ijapokuwa mbingu na nchi
zitatoweshwa lakini nafsi yako haitapita kamwe, hata itakapotelemshwa kwenye
mauti au kuingizwa katika mbingu mpya na nchi mpya. Maana twajua hakika kuwa,
nafsi ya mtu haitapata kifo hiki tukijuacho katika mwili, maana kinachokufa ni
mwili na siyo nafsi. Maana kipo kifo ambacho hicho huuhusu mwili, lakini pia
yako mauti ambayo hayo huihusu nafsi. Maana kuna tofauti kati ya mauti na kifo,
kwa kuwa kifo ni kwa ajili ya mwili na mauti ni kwa ajili ya nafsi. Mauti ni
mateso na maumivu, wakati kifo huhusu mwisho wa uhai.
Yafikri haya sawasawa, maana
ikiwa Roho Mtakatifu amekushirikisha wewe,
hailengi mwili wako hata kidogo, maana mwili unaweza kuyadharau wala
usione kuwa kitu cah kufaa, lakini mambo haya yanailenga nafsi yako ambayo
ndiyo yenye thamani kuliko vitu vyote, maana katika haya nafsi yako,
itafunguka, na kujua uhalisia wake.
Maana asema “ nia ya mwili ni
mauti lakini nia ya roho/nafsi ni uzima na amani”, je! Mwili huo utayafikri
haya na kuyabaini au utayaona kuwa kitu? Ingekuwa heri kama nafsi yako
itapambazuka na kuyafikri haya, ili kujitia ufahamu katika Roho Mtakatifu,
uliyeshirikishwa.
Hata hivyo, Mungu ni mwaminifu
kwa watu wake, maana walio wake awajua, na tena waisikia sauti yake, hao ndio
walioitwa na Yeye katika wito wa msalaba, akawakaribisha kwake kwa kuwa
walipoitwa waliitika, nao walitamani kukombolewa kwa kuwa walichoshwa na uteka
waliokuwa nao. Ikiwa Mungu wa mbinguni amekupa neema hiyo, ni hakika kuwa haya
utayatia katika moyo wako na kuyaamua vema kwa ajili ya utukufu wake Mwenyewe,
ila kwa njia hiyo upate kujibidisha katika kuhudhulia mbele zake, ili ayamimine
mapenzi yake ndani ya nafsi yako na upate kufanana naye na kumfaa zaidi kwa
kila neno, tendo na uwazalo.
Katika yote, Roho wake
Mtakatifu, ajifunue wazi, na kuyathibitisha yaliyo mapenzi ya Baba, katika
Mwana, ili nasi tulio nafsi zake, tupate kuyapokea na kujitia katika kweli yake
yote.
Hata hivyo yafaa sana ukiyafikri
na kuyabaaini haya, ambayo kwa hakika yanafaa sana, na ni kweli itokayo kwa
Mungu ambayo kwa Neema ya Kristo, Roho wake Mtakatifu ametushirikisha. Kama
alivyoyamimina ndani yangu, nami nayapokea kutoka kwake, na kumlilia sana anisaidie
niweze kuyatia katika fahamu zangu na kuyatekeleza bila upungufu wowote. Mambo
haya ni matamu sana, tena yanatia uchungu sana kwa kuwa, kwa hakika huyo Mungu
wetu ni wa ajabu sana, tujapomfikri katika hayo hakika hatutamuelewa wazi jinsi
alivyotufadhili na kutupenda.
Mwl; Goodluck Kazili
0765 129 960
kazili.blogspot.com
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni