Ni Siri Kuu; Ni huduma inayosimamiwa na Mwl; Goodluck Kazili. Inabeba pia; Kuhani Gospel Team (KGT), Akiba Zalishi (AZ). KGT; Ni timu ya Huduma za Kiroho, Yenye watumishi mbalimbali walioitwa kutumika katika kusudi la Mungu. AZ; Ni mfumo unaowezesha mtu/watu/taasisi/shirika/kampuni kuwa na kukuza mitaji, uzalishaji na uwekezaji. Wasiliana nasi:- Email: gkazili@yahoo.com, Phone: +225 (0) 765 129 960, Fb: Ni Siri kuu.
Jumatatu, 24 Novemba 2014
Goodluck Kazili (KGT-TANZANIA) HEAVEN KINGDOM TEACHING
Labels:
SK-Siri Kuu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Alhamisi, 28 Agosti 2014
WAJUA KUWA WE NI MFALME NA KUHANI!
kongamano la Maombi ya Shule na Masomo
Na Goodluck Kazili
Na Goodluck Kazili
UMENUNULIWA NA KUFANYWA KUWA UFALME NA KUHANI KWA MUNGU KATIKA NCHI
Si hadithi wala simulizi, bali ni kweli na hakika kuwa Kristo alichinjwa akawanunua watu wa kila kabila , lugha, jamaa, na taifa na akawafanya kuwa ufalme na makuhani wanamiliki juu ya nchi.
Si tu bahati kupata nafasi ya kusoma na kusikia habari hii, bali pia ni neema ya MUNGU kwako, hivyo nakusihi kwa upendo wake Yeye aliyetuumba uzitafakali habari hizi kwa kina nazo zitakufaa na kukusaidia kwa wakati wake.
Kwa msaada wa Roho Mtakatifu nalipenda nikushirikishe habari za nafasi yako kwa MUNGU, katika kanisa, katika nchi/taifa au jamii na familia yako. Si rahisi kujua nafasi yako, lakini imekupasa kuifikiria kwa kuwa hakuna atakayefikri kwa ajiri yako bali ni wewe mwenyewe.
Iko nafasi mhimu na kubwa mbele za MUNGU uliyo nayo, hivyohivyo ulivyo, japo nyumbani wanaweza wakawa wanakudharau na kukuona kuwa si lolote. Lakini mimi leo kama sauti ya MUNGU kwako jijue kuwa una nafasi kubwa na ya heshima mbele za MUNGU. Na nafasi hiyo ni ya mhimu sana kwako . haijalishi una maisha ya dhambi kiasi gani, lakini bado MUNGU ni m,wema kwako, maana maandiko yanasema “Tena zitokazo kwa Yesu Kristo shahidi aliye mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa na mkuu wa wafalme wa dunia. "Yeye atupendaye na kutuosha dhambi zetu katika damu yake. Na kutufanya kuwa ufalme na makuhani wa MUNGU, naye ni Baba yake ; utukufu na ukuu una Yeye hata milele na milele amina”. (ufunuo 1:5-6)
Mpendwa katika Kiristo Yesu, nakusihi kwa neema hii; basi ujitahidi kumpenda MUNGU na kutafuta sana kumjua Yeye ili kwa msaada wake maisha yaweze kukamilika. Maana hakuna maana ya maisha pasipo MUNGU mwenye kuyafanya maisha. Na kwa kuwa sisi tuliompokea Kristo tulifanyika kuwa watoto wa MUNGU, basi imetupasa kuyatambua haya ya kuwa yapo kwa ajiri yetu.
Ni mhimu kukumbuka kuwa, jambo lililo jema huja kwa wakati wake, basi hakika hili ni jambo jema. Kwa kuwa kama ungelijua tangu hapo kuwa wewe ni kuhani juu ya nchi katika ufalme wa MUNGU, basi pengine ungekuwa na hatua kubwa. Hata hivyo nakukumbusha kuwa hakuna wakati utakao kuwa mwema kwako zaidi ya wakati huu.
Hivyo nakusihi ufikiri kama mtu mhimu, ambaye anategemewa sehemu nyingi na watu wengi. Tena maneno haya usiyasahau, elimu ipo ili kukupa maarifa, na kwa kuwa kuna namna mbili, basi ni mhimu kuwa na maarifa ya pande zote, kwa kuwa unaishi pande zote. Ni hatari sana kutokuwa na maarifa juu ya nmna hizi mbili.
Kwa hakika yapo maarifa ya roho na yapo maarifa ya mwili. Maarifa haya yote ni mhimu sana kwako, japo maarifa ya roho yanaonekana kuwa na thamani kubwa. Yanaonekana ya thamani kwa kuwa si wengi wanaobahatika kuyapata, kwa sababu hawayatafuti. Sasa sikushauri wewe ujaribu kutoyatafuta, itakuwa hatari sana. Tafuta maairfa ya roho na haya ya mwili kwa kuwa yote yatakusaidia katika maisha yako yote ya sasa na ya badae, hata baada ya kufa.
Ningeweza kukuandikia mengi, lakini kwa ufupi huu, naomba utafakari sana jinsi unavyowaza na unavyoenenda, je namna hiyo itakusaidia kufika hapo alipokukusudia MUNGU? Ikiwa ni ndiyo MUNGU akutie nguvu katika juhudi hizo, na ikiwa siyo basi MUNGU akusaidie ili ujitahidi kwa dhati kuubadili mwenendo na mawazo yako. Uyatambue haya kuwa yamekujia kwa wakati sahihi wa wewe kubadilika na kuanza kufikri sawasawa na makusudi ya MUNGU aliyekuumba. Usipoteze muda ni wakati wako maana “ Nao waimba wimbo mpya wakisema wastahili kukitwaa hicho kitabu na kuzifungua mhuri zake,kwa kuwa ulichinjwa ukamnunulia MUNGU kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa, ukawafanya kuwa ufalme na makuhani kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi” ufunuo 5:9-10
Haya ndiyo nalipenda nikushirikishe japo kwa ufupi, MUNGU akubariki .
Goodluck Kazili 0765-129960
Labels:
SK-Siri Kuu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
SIRAHA MOJA MHIMU YA VITA YA KIROHO
KUHANI GOSPEL TEAM (KGT)TANZANIA)
SIRAHA MHIMU ZA UFALME WA MUNGU
Linapotajwa
Neno siraha, kuna kitu kinajengeka ndani yako, na wakati mwingine utapata picha
fulani. Hata hivyo suala la siraha lipo ikiwa tu kuna vita au ulinzi au
uharibifu. Kama ilivyo katika mwili pia katika
ulimwengu wa roho zipo siraha, na
zinamatumizi mbalimbali.
Mpendwa
katika Kristo, ni wazi kuwa, siraha hizi za ufalme wa Mungu, ni mhimu kuzijua
zote pamoja na matumizi yake, lakini pia umhimu wake.
Waefeso
6:10, inaeleza kuwa tuzidi kuwa hodari katika uweza wa Mungu na nguvu zake,
lakini anasema uhodari wetu upo kwa kuzivaa siraha zote za MUNGU. Hapa
unagundua kuwa zipo siraha nyingi za MUNGU, na ikiwa zipo nyingi zaidi ya moja kama maandiko yanavyothibitisha, basi ni hakika kuwa,
zinatofautiana katika matumizi pia.
MUNGU
alipotengeneza siraha tofauti tofauti, alikuwa na maana kubwa, na siraha hizo
hutumika kwa wanadamu tu na zipo zitumikazo kwa malaika, ila hatutazungumzia
hizo za malaika ila tutazungumzia zilizowekwa kutumiwa na wanadamu au duniani. Kama nilivyoeleza kuwa siraha hizo zinatofautiana kwa
namna nyingi.
Mtumiaji wa
siraha
Huyu
ni mtu mhimu sana kwa kuwa siraha za Mungu zilizotengenezwa kwa ajili ya wana
wa ufalme wa MUNGU hapa duniani, haziwezi fanya kazi hadi awepo mtumiaji, na
kama mtumiaji atakosa maarifa basi siraha hizo zitafanya kazi kwa kiwango cha
maarifa alichonacho mtumiaji.
AINA ZA
SIRAHA ZA UFALME WA MUNGU
SIRAHA YA IMANI
Hii
ni siraha ya kwanza, si kwa ukubwa ila inayobeba siraha nyingine pia. Kwa mjibu
wa waebrania 11:1 imani ni kuwa na hakika), si kitu cha kubahatisha, ila ni
uhakika ambao mtu anakuwa nao juu ya jambo Fulani, tena jambo hilo lisiwe la wakati huo ila liwe la wakati
ujao na lazima liwe halionekani. Ukisikia kitu kisichoonekana ina maana kuwa
kitu hicho ni cha kiroho.
Kwa
maana nyingine tunaweza kusema, imani ni namna ya roho inayosimama kama nguvu, siraha, mamlaka, uwezo, uhakika na kuamini,
inayotarajia kutekeleza au kutekelezwa kwa jambo fulani. Kwa msingi huo imani
si kuamini tu kuwa Mungu anaweza ila ni zaidi ya kumwamini MUNGU. Mwili una kawaida ya kutokuamini vitu vya
rohoni, hivyo wakati mwingine mwili unaweza kukutia moyo kuwa Mungu anaweza
kila kitu ila ikifika kwenye tatizo mwili utakuambia hili siyo la kawaida.
Lengo la kukuambia hivyo ni ili kukuondoa kwenye imani halisi ya utendaji
ambayo ndiyo kubwa.
Kuna
imani ya kumwamini Mungu kuwa anaweza, lakini pia kuna imani zaidi ya kumwamini
Mungu kuwa anaweza. Ukweli ni kuwa kitendo cha kumwamini Mungu kuwa anaweza ni
hatua ya kwanza ya imani, kuishia hapo hakuwezi kusaidia kitu zaidi ya kuwa na
tumaini tu, lakini ukitaka kuiona, imani ikifanya kazi yake, lazima kuamini
huko ukufanye kuwa kitendo.
Mfano
mama hana mtoto, na ameomba na kuhitaji sana kupata mtoto na hajapata, kwa hakika
ni kuwa mama huyo anaweza akawa anamwamini Mungu lakini kumwamini Mungu huko
hakuwezi kumsaidia asilimia nyingi kupata mtoto, isipokuwa kinachoweza
kumsaidia ni pale anapoweza kubadili ile hali ya kuamini, iwe tendo.
Mfano
mama anaweza kuamua na kusema, kwa kuwa imani ni kuwa na hakika ya mambo
yatarajiwayo na ni yale mambo yasiyoonekana, hivyo basi itampasa kuwa na
uhakika ndani kuwa, mwakani atakuwa na mtoto na inampasa kufanya
maandalizi kwa kuanza kununua vifaa
vyote vya mtoto atakayemzaa, na wakati huo pengine hata mimbabado. Mungu akiiona imani hiyo hakika lazima
amfanyie mama huyo hata kama mpango haukuwepo.
Ukisoma
maandiko matakatifu, unagundua kuwa wakati Yesu alipokuwa akiendelea na huduma
kati ya vitu alivyokuwa anaangalia ilikuwa imani ya mtu, wakati mwingine hata kama mtu alikuwa hasitahili kutendewa lakini kwa imani
yake ilimulazimu Yesu kumfanyia haja yake.
Nakuomba
usome kwa umakini mistari hii uione imani jinsi ilivyo na hapa ndipo Roho
alipokusudia kukufundishia suala la imani
“(Mathayo
15:22-28), Natazama, mwanamke mkananayo wa mipaka ile akatokea, akampazia
sauti akisema, unirehemu, Bwana, mwana wa Daud; binti yangu amepagawa sana na mapepo. 23 Wala Yeye hakumjibu neno. nao wanafunzi
wake wakamwendea, wakamwomba, wakisema
mwache aende zake; maana anapiga kelele nyuma yetu. 24 Akajibu, akasema, sikutumwa ila kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli. 25 Naye akaja akamsujudia, akasema Bwana, unisaidie.
26 Akajibu, akasema, si vema kukitwaa
chakula cha watoto na kuwatupia mbwa. 27 Akasema, Ndiyo, Bwana, lakini hata mbwa
hula makombo yaangukayo mezani pa bwana zao. 28 Ndipo Yesu akajibu,
akamwambia, mama imani yako ni kubwa; na
iwe kwako kama utakavyo. Akapona binti
yake tangu saa ile”
Sijui
umepata kitu gani, lakini kwa kweli huwezi kuielewa imani vema hadi umeyapima
mazingira na mazungumzo ya huyu mama na Yesu. Maneno yaliyolazwa ni kauli za
mama mkananyo, maneno yaliyokolezwa na hayajalazwa ni ya Yesu mwenyewe na
mengine walisema wanafunzi.
Kama
umefuatilia kwa nia ya kuijua imani sawasawa ni kuwa umegundua, yule mama
alikuwa na mambo mawili makubwa, kwanza alikuwa na msimamo pili alikuwa na uhakika
na anachokiomba majibu yake yapo. Uhakika ulimpa msimamo na msimamo
ulimsaidia kulinda imani na kupata alichokuwa anakihitaji.
Jambo
la ajabu, ni majibu ya Yesu, mstari wa 26 aliposema kuwa chakula alichonacho ni
kwa ajili ya watoto wake na siyo kwa ajili ya mbwa, kwa lugha nyingine alimuita
yule mama kuwa ni kama mbwa kwake. Hivi mfano wewe ukamwendea Yesu na kumsihi
ukimuomba, halafu akakujibu kuwa ana majibu ya maombi ya watoto wake tu na siyo
mbwa; unaweza ukafanyaje. kwa haraka haraka, inaweza ikawa ndio mwanzo na
mwisho habari zako na Yesu, maana kama umemwendea kwa kumsihi na ukitegemea
atakusaidia halafu bado ni Mungu, lakini anakupa majibu ambayo hata mpagani
mwanadamu asingekupa kama umemwendea kwa unyenyekevu kiasi hicho.
Lakini
hebu mtazame mama yule kwa unyenyekevu anamkaribia Yesu na kusema “ndiyo Bwana”
kisha akajenga hoja asiyoitegemea Yesu, ni kweli mimi ni mubwa na pengine
sistahili kula chakula ulichoandalia watoto wako, “ lakini hata mbwa hula
makombo yaangukayo mezani pa bwana zao” Yesu alishangaa sana, maneno ya mama
huyo yalikuwa na maana hii; kwa kuwa sistahili kula chakula ulichowaandalia
watoto wako kwa sababu mimi ni mbwa wako
na siyo mtoto wako, basi uniruhusu tu nile makombo yaliyoanguka mezani pako
maana hiyo ni haki yangu kama mbwa wako.
Hii
ndiyo imani halisi inayotakiwa kwa watu wa MUNGU, ni wazi kuwa hujawahi
kujibiwa kama huyu mama alivyojibiwa na alivyokatishwa tamaa na Yesu mwenyewe,
lakini kwa imani yake alisimama akasema nina hakika na ninatarajia kupokea kwa
namna yeyote. Na alipojenga msimamo huo Yesu akamtazama akasema Mama imani yako
ni kubwa, na iwe kwako kama utakavyo, akapona
binti yake tangu saa ile.
Ukisoma
kwa kutafakari, na kwa undani unagundua kuwa, Yesu hakumuombea Yule mama juu ya
mtoto wake, ila alimwambia iwe kwako kama
utakavyo. Hebu fikri kama yule mama angekuwa
anataka awe tajiri mimi nakuambia saa ile ile yule mama angekuwa tajiri. Si kwa
maombi sana kuwa alipata alichotaka ila kwa imani yake, maana kama ni kuomba
aliomba vizuri tena kwa unyenyekevu mkubwa; kama umesoma vema yale maombi ya
yule mama yalikuwa ya unyenyekevu sana kuliko ya kwako unayoyaomba, hebu
yatazame “akampazia sauti akisema,
unirehemu maana yake unihurumie Bwana, mwana wa Daudi, lakini Yesu
hakumjibu neno. Wanafunzi walipomtazama yule mama wakamhurumia na wao
wakamwendea Yesu wakamsaidia kuomba wakasema mwache aende zake, maana yake
mtendee ili aende zake maana anaendelea kupaza sauti. Bado Yesu hakujali maombi
ya mama yule hata kwa kubembelezwa na wanafunzi wake, na badala yake akwaambia
hakuja kwa ajili ya yule mama ila kwa wana wa Israeli waliopotea. Mama hakurudi
nyuma japo kwa maneno hayo ilimtosha kuishi hapohapo, ila ajabu kuu aliendelea
pamoja na kwamba Yeye hata kujibiwa hakujibiwa, ila wanafunzi walimsaidia ili
angalau ajibiwe, bado anajibiwa kuwa Yesu hakuja kwa ajili yake. kwa hiyo
ilimaanisha kuwa asitegemee kuwa anaweza kutendewa chochote kama anavyoomba, kama ni kuondoka aondoke tu. Yule mama baada ya kuambiwa
hivyo akasogea akamsujudu, kuonesha kuwa hata kama
hukuja kwa ajili yangu ila mimi nakuamini, alipomsujudu akaomba tena akisema,
Bwana unisaidie. Baada ya Yesu kuona huyu mama anang’ang’ania akasema maneno
magumu sana ambayo sasa yule mama kama si imani kubwa aliyokuwa nayo angekufulu palepale.
Swali
langu kwako ni hili; huyu mama ana utofauti gani na wewe? Je Yeye hakuwa
mwanadamu kama wewe? Je Yeye hakuwa na haja kama wewe ulivyo na haja? Na je umewahi kuomba
ukakatishwa taamaa angalau robo ya huyu mama? Umewahi kujibiwa majibu kama alivyojibiwa huyu mama?. kwa kujiuliza hivyo,
angalia imani yako, utagundua huna imani, na ndicho chanzo cha kutokupata kile
unachotakana kuomba.
Hebu
ngoja nikuambie jambo moja hapa la ajabu ili uone imani inavyofanya kazi kwa
mhitaji lakini pia kwa yule anayeombea. Mathayo 17:14-16 inaeleza kisa kimoja, “Nao
walipoufikia mkutano, mtu mmoja akamjia, akampigia magoti akisema. Bwana
umurehemu mwanangu, kwa kuwa anakifafa, na kuteswa vibaya; maana mara nyingi
huanguka motoni, na mara nyingi majini. Nikamlete kwa wanafunzi wako, wasiweze
kumponya.” Ukiendelea kusoma unaona Yesu akichukia kwa ajili ya yule
mtu, na juu ya wanafunzi wa Yesu kwa kuwa hawakuwa na imani. Ila alipomaliza
kuwasema aliamuru wamlete kwake kisha akakemea yule pepo akamtoka yule mtoto. Wanafunzi wake walipoona hivyo, hawakulidhika
wakamwendea mstari wa 19 “kisha wale wanafunzi wakamwende Yesu kwa
faragha wakasema mbona sisi hatukuweza kumtoa? 20 Yesu akawaambia, kwa sababu
ya upungufu wa imani yenu, kwa maana, amini, nawaambia, mkiwa na imani kiasi
cha punje ya haradali, mtauambia mlima huu, ondoka hapa uende kule, nao
utaondoka; wala hakutakuwa neno lisilowezekana kwenu”
Naamini
umeona kazi ya imani na jinsi imani ilivyo, ila ukisoma sehemu nyingine
wanafunzi walipoambiwa hivyo waliomba waongezewe imani ndipo Yesu akawaambi
mngelikuwa na imani hata chembe ya haradali , kwa maana kuwa hawakuwa na imani
hata ndogo japo walikuwa ni wanafunzi wa Yesu na walikuwa wanamwamini Yesu.
Hapo unagundua kuwa imani ni zaidi ya kumwamini Yesu, lakini pia amesema hakutakuwa na neno lisilowezekana kwenu.
Unafikri kwa nini mambo mengi hayawezekani kwako, ni kwa sababu huna imani japo
unamwamini Mungu. Ni wazi kuwa ungekuwa unaweza ungeniuliza swali sasa hiyo
imani ya zaidi ya kumwamini Mungu iko je? na ndio unafanya je?. Roho mtakatifu
alijua kuwa utahitaji kujua na ameweka majibu ya maswali yako hapa chini. Ila
nakusihi sana
isiwe tu kusoma na kuelewa bali iwe kusoma na kutenda hicho unachogundua na
kukielewa.
Ukisoma
hapo kwenye mathayo 17 lakini mstari wa 21 umetoa majibu. “ lakini namna hii
haitoki ila kwa kusali na kuomba” hapo humaanisha kuwa namana hiyo ya imani
inayoweza kutoa nguvu za namna hiyo haiwezekani isipokuwa kwa kufunga na
kuomba. Maana yake ni kuwa kuna kiwango cha imani unachoweza kukipata kwa kuamini
na kufanya kile unachokiamini kiwe hakika na kutenda vile unavyoaamini, lakini
kiwango halisi cha imani hupatikana kwa kufunga na kuomba.
Hii
ni kwa sababu mwanadamu ana namna ya mwili sana kuliko namna ya roho na kwa
kweli hakuna mahali popota ambapo mwili unakubali na kumruhusu mtu kuwa na
imani hasa ya utendaji, hivyo kufunga maana yake ni kuutiisha mwili ili
kupandisha ile nafasi ya roho, hivyo kumfanya mtu kuwa na hali ya roho kuliko
ya mwili. Pia kufunga huko kunaudhoofisha mwili ambako kudhoofika huko huifanya
roho kuwa na nguvu.
Pia
kuomba hutifua au hunyanyu hali ya roho, au hunyanyua hali ya kimungu ndani ya
mtu, na hupunguza kasi ya mwili kufikri kimwili na kuifanya akili ikae kwa
namna ya roho ambapo ni rahisi sana kuwa na imani na kuona kuwa kila kitu kinawezekana
kwa Mungu, na kwa kuwa unakuwa kwa namna ya roho zaidi utasikia msukumo ambao
unakusukuma kufanya kile unachokiamini na unapofanya kwa kuwa unafanya kwa
uhakika lazima kitokee.
Mpendwa
katika Kristo, siraha ya imani ni siraha kubwa sana,
na wakati mwingine imekupasa kufanya mazoezi ya imani, hata pale ambapo watu
wote wanaona ni ngumu, wewe unawaambia inawezekana, pale akili yako
inapokuambia hapa ni ngumu unalazimisha ikubali kuwa inawezekana hata kama kwa jinsi ya kawaida haiwezekani.
Kikubwa
jitahidi kuamini, na kufanya kile unachokiamini kiwe kweli, yaani kama unaamini
Mungu anaweza katika jambo Fulani weka uhakika, na kisha lifanye ikiwa unomba
uambiwe omba ukijua nikimaliza kuomba nitakuwa nimepokea, na ukimaliza hata kama hujaona majibu anza kujiaminisha kuwa umepokea
taratibu taratibu utaanza kusikia amani moyoni na kuona lile jambo
likikamilika.
Mungu
wa mbinguni akujalie kujua vema siraha za ufalme wake ili uwe askari mwema na
mtetezi wa wokovu wako na kuujenga mwili wa Kristo. Hata hivyo ujue kuwa ziko
siraha nyingine kama siraha ya Neno, Siraha ya
Maombi, Siraha ya Wokovu. Hizo ndizo siraha kuu za ufalme wa Mungu. Na hata
siraha hiyo ya imani imeelezwa kwa ufupi hivyo endelea kusoma kwenye maanidiko
juu ya imani na vitabu vya Neno la Mungu, semina, mikutano, na zaidi shuhuda
mbalimbali. Maana imani chanzo chake ni kusikia ambako huja kwa Neno la Kristo.
Mungu wa mbinguni akujalie mema yote.
“mjue sana
Mungu ili uwe na amani”
Mwl: Goodluck Kazili
Labels:
SK-Siri Kuu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Ijumaa, 4 Julai 2014
KARIBU UTUMIKE NASI- KUHANI GOSPEL TEAM (KGT)
Karibu Katika Huduma ya KGT (Kuhani Gospel Team) Tanzania.
Labels:
SK-Siri Kuu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Ijumaa, 2 Mei 2014
SOMO LA KUJUA MISING YA NCHI NA NAMNA YA KUOMBA
KONGAMANO
LA 8 LA MAOMBI YA TAIFA TANZANIA 2013
MADA: KUOMBA
TOBA NA UPATANISHO KWA AJIRI YA SELIKARI ILI KUPATA
KIBARI NA KUWA NA UHUSIANO
WA KUDUMU MBELE ZA MUNGU
Daniel 9:1-27
MUHIMU KUHUSU MADA ILIYOTANGULIA:
Mada ilikuwa: "KUJENGA NAFASI HALISI
YA KANISA KATIKA NCHI"
Katika mada hii, tuliangalia na
kuomba juu ya lango la kanisa kuwa imara katika nchi. Tuliomba toba juu ya
kuhusuriwa Kwa lango hilo, tukaomba kuimarishwa kwa lango hilo, tukaomba
kutumiwa vema na Mungu ili kufanya mapenzi yake, tukaomba juu ya kuchukua
wajibu wake wa kuiongoza selikali katika njia bora ya kiMungu. Tulikuwa na
mfululizo wa makongamano 3 ya kuombea kanisa, ambapo tulianza terehe 10/4/2012
na kukamilisha 15/12/2012.
Wakati huu tumepewa “kuomba
toba na upatanisho kwa ajiri ya selikari ili kupata kibari na kuwa na uhusiano
wa kudumu mbele za mungu”. eneo hili tutajifunza yale ambayo Mungu anataka
tuyajue juu ya nafasi Yake katika selikali, pamoja na nafasi ya selikali mbele
za Mungu, na wajibu wa kanisa katika selikali.
DONDOO
Nafasi ya
selikari mbele za Mungu
Nafasi ya Mungu katika selikari
Wajibu wa
kanisa katika selikali mbele za Mungu
UTANGULIZI:
Ni jambo la mhimu sana katika
nchi, kuwa na mtazamo chanya juu ya misingi ya nchi na uwepo wake katika dunia
inayoonekana na ile isiyoonekana yaani ulimwengu wa roho. Imani yangu ni kuwa
unajua “kushindana kwetu sisi si juu ya damu na
nyama, bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya
majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho, Waefeso 6:13”. Misingi ya nchi yoyote hujengwa katika
ulimwengu wa roho kwanza kabla ya kujengwa upande wa mwili. Ni wazi kuwa, kwa
kuwa kuna falme, mamlaka na jeshi la pepo wabaya katika maeneo haya haya ya
dunia, swali la kujiuliza ni hili, je huo ufalme, mamlaka na jeshi la pepo
linafanya kazi juu ya nani au jeshi hilo linamrinda nani na lipo kwa ajili ya
kupigana na nani?
Ni hakika kuwa ulimwengu huu ni
mwendelezo wa ulimwengu wa roho, ambapo mfumo na namna unavyoongozwa inafanana
kwa sehemu kubwa na ile ya ulimwengu wa roho, ndio maana huwa kuna kuathiliana
kati ya watu wa dunia yaani wa mwili na wale wa roho. Hata hivyo tunajua kuwa
yako madaraja kadhaa yanayoikamilisha dunia kwa upande wa watu. Kwa mfano kuna
mtu, familia, ukoo,kijiji,kata, tarafa,wilaya, mkoa, kanda, taifa, bara,dunia.
Madaraja haya huadhili au kuathiliwa kuanzia mtu hadi dunia. Athali haiwezi
kutokea ambayo chanzo chake itakuwa nchi, bali kwa mtu au familia/kundi dogo
linaweza kuvuluga hali ya nchi, pia mtu au familia/kundi dogo linaweza kuiweka
nchi katika hali njema, hata maandiko yanathibitisha “ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu,
watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya;
nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao, 2
Nyakati 7:14”.
Karibu Usome na Kujifunza, Roho Mtakatifu yuko tayari kukusadia vema; Amina
UFAHAMU JUU YA NCHI/TAIFA LA TANZANIA
Hadi sasa Tanzania ina miaka 51,
lakini Tanganyika ina kadiliwa kuwa na miaka 10,000 tangu watu waanze kuishi,
kwa ushahidi wa kiakilojia. Hatuwezi kutazama hali ya nchi kwa kuitazama miaka
hiyo 51, bali tunatakiwa kutazama tangu kuwepo kwa aridhi ya Tanzania, na pale
watu walipoanza kuishi.
Japo ni vigumu sana kupata histori,
lakini kujua ukweli kwa namna ya roho inawezekana kwa kuwa kisichokuwepo ni
ushahidi wa kimwili, ila ushahidi wa mambo ya roho upo, “kwa maana twajua torati asili yake ni ya
rohoni-Warumi 7:14a”.
Wakati Mungu anaiumba dunia,
Tanganyika iliyozaa Tanzania aliiumba, na kusudi lile lile tunalolisoma kwenye Maandiko la Mungu kuiumba dunia ndilo kusudi la Mungu kuiweka Tanganyika-Tanzania,
(tunatumia Tanganyika kwa kuwa ndiyo asili, kwa kuwa Tanzania imepatikana
kisiasa, yaani baada ya kuungana na Zanzibar). Na kwa kuwa kila jambo
analolifanya Mungu huwa na maana kubwa, basi uwepo wa Tanganyika una maana sana
kwetu tuliowatanganyika na wazanzibari,
kwanza mbele yetu wenyewe, mataifa mengine na mbele za Mungu mwenyewe
aliyetuweka.
Nchi yetu iliumbwa kwa ajiri ya
Mungu, nasi tukawekwa ili kutawala, nchi hii ni mali ya Mungu, kwa kuwa dunia
na vyote viijazavyo ni mali ya Mungu. Hata hivyo sisi tunaoishi humu, tumepewa
kazi moja kuu, kuitawala nchi na kila kilicho ndani na juu ya nchi kwa maana ya
kilicho aridhini na kilichoko juu ya aridhi “Mwanzo 1:26-31”.
Hivyo ni mhimu kukumbuka kuwa
kusudi la Mungu juu ya Tanzania halijakuwepo kuanzia mwaka 1961-64, bali
lilikuwepo tangu ilipowekwa misingi ya dunia. Na kwa kuwa kusudi la Mungu
ilikuwa kuwa na utawala mwingine wa namna ya mwili huku duniani, na ikampendeza
kuiweka Tanganyika, basi ni mhimu kulitazama kusudi hilo ili kuijua Tanzania na
mstakabali wake katika misingi ya roho na mwili.
Tanganyika iliumbwa kama nchi na
wala siyo taifa, kwa kuwa hakuna mahali palipoumbwa kama taifa, na tukishataja
suala la nchi basi tunagusa lasiri mali, kwa kuwa nchi ni aridhi. Na kusudi la
Mungu haliko kwa watu wa Tanzania, bali kwa nchi ya Tanzania, kwa kuwa angeweza
kuzaliwa yeyote Tanzania, na kama kusudi lingekuwa kwa watu, basi
tusingetawaliwa na kuongozwa kwa muda wa miaka zaidi ya 85,(wakati wa ukoloni)
ambao ni umri unaoizidi Tanzania, lakini bado mambo yaliyofanyika yana maana
kubwa katika kukamilisha kusudi la Mungu juu ya nchi.
Nchi hukamilika inapokaliwa na
watu, na hapo ndipo kusudi la Mungu hukamilika. Kwa kuwa ukamilisho wa kusudi
la Mungu ni pale nchi inapokawaliwa na watu, na kutawala kwa misingi ya Mungu.
Tanzania ina eneo lenye ukubwa wa kilomita za muraba laki
tisa elfu arobaini na tano na mia mbili na tatu (945,203), ni nchi ya 31 kwa
ukubwa wa eneo, katika eneo hilo aridhi ni asilimia 93.8 katika 100, na eneo la
maji ni asilimia 6.2 ya jumla ya eneo lote. Idadi ya watu kwa mujibu wa sense
zilizowahi kufanyika sense ya kwanza mwaka wa 1967= milioni 12 laki 3 elfu 13
mia 469,( 12,313,469) sense ya pili mwaka wa 1978= milioni 17 laki 5 elfu 12
mia 610,(17,512,610) sense ya tatu mwaka wa 1988= milioni 23 elfu 95 mia 885
(23,095,885) sense ya nne mwaka wa 2002= milioni 34 laki 4 elfu 43 mia 603
(34,443,603).
Sense ya tano ya 2012 inakadiliwa
kuwa na watu milioni 45,798,475, kadilio la miaka ijayo, kufikia mwaka 2020 inakadiliwa kuwa 57, 102,896. Kwa idadi hiyo inaonesha kuwa
nchi ya 30 kwa idadi ya watu. Kwa kila eneo la kilomita mbili linakaliwa na
watu 46, msongamano huu, unaiweka kuwa nchi ya 124 kwa msongamano wa watu, ndio
nchi kubwa zaidi Afrika ya Mashariki.
Tanzani inajulikana kama nchi
masikini sana Duniani, katika viwango vya kimataifa, japo katika uhalisia
Tanzania si nchi masikini, bali ni Taifa masikini. Kwa maana utajiri ulio
kwenye aridhi ya Tanzania ni zaidi ya utajiri ulio kwenye mataifa
yanayohesabika kuwa nchi tajiri.
Kabla ya ukoloni hatukuwa na
taifa la Tanzania, wala Tanganyika, isipokuwa kulikuwa na koo, pamoja na
makabila mbalimbali yaliyokuwa na utawala wao, hivyo hatukuwa na jamii moja
ya Tanganyika wala Tanzania kwa kuwa haikuwepo
mipaka halisi ya nchi kiutawala. Mnamo mwaka wa 1884, katika nchi ya ujerumani
iliyoko uraya, ulifanyika mkutano wa kuigawa afrikana ili kuiweka chini ya
utawala (ukoloni). Wakati huo ndipo mipaka ilipochorwa na Tanganyika ikawa
taifa na nchi yenye mipaka halisi, iliyotambuliwa na umoja wa mataifa baadae.
Wakati huo ndio ulikuwa mwanzo wa kuja kwa habari za Kristo, kwa njia ya
umisheni, ulikuwa unafanywa na wazungu. Hata hivyo, jamb la kuleta habari njema kama maandiko
yalivyokuwa yametangulia kusema, bado ilionekana kuwa ni tatizo kwa kuwa
ilihusisha masuala ya utawala wa kinyonyaji yaani ukoloni.
NAFASI YA SELIKARI MBELE ZA MUNGU
Selikari kwa maana ya utawala, ni
chombo kilichowekwa/kinachowekwa na Mungu kwa kusudi la kusimamia/kuhudumia
watu wake katika mambo yote ya mwili. Selikali siyo mtu bali ni
mamlaka(authority) ambayo ipo kwa ajiri ya kutekeleza mambo makuu matatu. Kujenga uchumi imara kwa watu wake, kuwa na siasa safi, na kutoa huduma zote za kijamii
KUJENGA UCHUMI IMARA:
Uchumi wa nchi na watu wake anayehusika kuujenga ni selikali, hili ni
jambo moja mhimu linalotambulisha utendaji wa selikali (mamlaka). Japo kuna
vitu ambavyo huisaidia selikali kujenga uchumi imara kwa watu, hata hivyo vitu
vyote ni wajibu wa selikali kuwa navyo, isipokuwa tu maliasili ambazo ziko nje
ya uwezo wa mwanadamu. Uchumi wa nchi uko kwenye nchi, ikimaanisha kuwa uchumi
wan chi uko kwenye aridhi. Lakini hatuwezi kutaja uchumi bila watu.
Maana ya uchumi, ni kuzalisha na kutumia
lasilimari zilizoko ili kukidhi mahitaji yaliyopo, lasilimari hizo ni kama zile
za asili na zisizo za asili, lakini hata hivyo zisizo za asili hutokana na zile
za asili.
UFAHAMU
WA KIROHO JUU YA UCHUMI
Hapo mwanzo hapakuwepo na uchumi,
kama tuuonavyo leo, lakini mara ya kwanza kabisa Mungu alimwagiza Adamu kuilima
aridhi na kuitunza, huo ulikuwa mwanzo wa uchumi katika kitabu cha “Mwanzo
1:28-31”. Pia watoto wa Adamu, Kaini na Habiri, walikuwa wakifanya kazi
zilizotambulisha nafasi yao na uchumi wao.
Dhambi inaonekana kuwa tatizo la
uchumi, kama vile lilivyo tatizo la uzima wa milele “Mwanzo 3:17” dhambi
iliathili aridhi, na hauwezi kuwa na uchumi bila kuwa na aridhi ukiwa kama
taifa au nchi. Wakati Mungu alipoilaani aridhi, kwa sababu ya dhambi ilikuwa na
tafsiri ya kuulaani uchumi, kwa kuwa maisha ya mtu kwenye mwili yalitegemea
sana ardhi “Akamwambia Adamu, kwa kuwa umeisikiliza
sauti ya mke wako, ukala matunda ya mti ambao nalikuagiza, nikisema usiyale;
ardhi imelaaniwa kwa ajiri yako; kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za
maisha yako, michongoma na miiba itakuzalia, nawe utakula mboga za kondeni; kwa
jasho la uso wako utakula chakula, hata utakapoirudia aridhi, ambayo katika
hiyo ulitwaliwa; kwa maana u mavumbi
wewe nawe mavumbini utarudi.
Laana hii vipengele vyake vyote vinagusa uchumi tu, kwa kuwa kipengele cha
kifo hakikuwa laana bali yalikuwa matokeo ya kuvunja sheria, na aliambiwa
mapema kuwa akila hayo matunda hakika atakufa.
Dhambi iliharibu suala la uchumi,
kuwepo kwa dhambi kulifanya suala la uchimi kuwa tatizo, kwa maana ya kuwa
ilifanya mtu ahangaike ili kuwa na uchumi mzuri, hali njema ya uchumi
tunayoiona kwa baadhi ya watu, na kwa baadhi ya nchi/mataifa, ni kidogo sana
ukilinganisha na ilivyokuwa imekusudiwa, kabla ya dhambi kuvuruga.
Lakini hata hivyo, kwa maana
halisi ya uchumi tuijuayo leo, inaonesha kuwa uchumi uliletwa na dhambi, maana
ya sasa ya uchumi “ ni kutumia malighafi zisizotosheleza ili kukidhi mahitaji
ya mwanadamu” hivyo kama kuna utoshelevu basi suala la uchumi tusingekuwa nalo,
lakini kwa sababu ya upungufu uliopo, tunalazimika kuwa na wazo la kusuruhisha
tatizo na kuzalisha na kutumia lasilimali kidogo zilizopo ili kutimiza mahitaji
yaliyoko, Na tunajua kuwa bila dhambi huo upungufu usingekuwepo.
Adamu ni mzaliwa wa kwanza, nje
ya nafasi ya Yesu, na kwa kuwa yeye ni lango la wanadamu wote na mataifa yote,
hivyo wote huhesabiwa kuwa wametenda dhambi ileile aliyoitenda Adamu. Jambo
hili ni kwa sababu ya, kila mtu hupita kwenye lango lilelile la Adamu, hivyo
kinachosababisha tuhesabiwe kuwa tumetenda dhambi si kutenda dhambi kwenyewe
bali mahali tunapopita na kutokea
tunapokuja duniani ndipo panapofanya tuhesabiwe dhambi.
Baraka kuu ya hapa duniani ni
uchumi imara, wala siyo wokovu, kwa kuwa wokovu haupo kama Baraka, bali ni
neema ambayo ipo kwa kila mtu. Lakini suala la uchumi si neema ambayo imewekwa
kwa kila mtu, bali ni maarifa, ujuzi na ufahamu wa namna ya kuujenga ili uwe
imara, ndicho kigezo kikuu. Ukisoma maandiko, kuanzia kitabu cha mwanzo, habari
za Ibrahimu hadi kufika kwenye agano jipya, mafundisho na Baraka zilizoamriwa
nyingi ni za uchumi, hata hivyo agano la kale lote lemetaja Baraka kuu mbili,
nayo ni ya uchumi na afya tu. Agano jipya limetaja wokovu pekee kwa wingi sana
na msisitizo uko kwanye wokovu uletao
uzima.
Mfano Mungu alimuahidi ibrahimu
kumrithisha kizazi chake nchi ya kanani, ambayo imejaa maziwa na asali, lakini
ni ukweli kuwa nchi ya kanaani haina hivyo vitu kwa kiwango tunachosoma kwenye
maandiko, hii ni kwa sababu kilichokuwa kinaelezwa ilikuwa zaidi ya maziwa haya
tuyajuayo kwa jinsi ya mwili. Kwa kuwa lugha ya roho huweza kutumia kitu
kiletacho taswira tu kwenye ulimwengu wa mwili, kwa mfano Mungu alipozungumza
suala la maziwa, ni hakika kuwa alitaja vitu vyote vijulikanavyo kuwa bora na
hasa vyakula, pia ilipotajwa asali ilimaanisha vitu vyote vilivyo vitamu kwa
aina yake kuwa vitakuwa vimejaa katika nchi ya Kanaani.
Hata hivyo kuna uhalisia wa sasa
katika vitu hivyo vilivyotajwa katika nchi ya Kanaani ambayo sasa ni Israel.
Kwa maelezo haya bado inaonesha kuwa jambo kubwa lilikuwa la uchumi, hata
kilichosababisha wao kwenda Misri ilikuwa haja ya uchumi na hata
kilichowakwamisha kutokutoka Misri ni uchumi uliokuwa umeunganisha na miungu ya
misri.
Ukisoma maandiko kwenye agano la kale hakuna mahali
ambapo uzima wa milele umetajwa, kama
tuujuavyo leo, hata kwa wale waliopata kuelewa, walichojua kuwa wakisha kufa
watalala pamoja na ndugu zao, wala hapakuwa na ufahamu juu ya siku ya mwisho,
hadi kufikia wakati wa nabii Amosi karibu mwaka 750 K.k.
Amri 10 za Mungu na sheri zaidi
ya 420 walizopewa wana wa Israel, karibu zote zilikuwa zinagusa hali ya uchumi
wao. Hii ina maana kuwa zilikuwa za kujenga uhusiano mwema na Mungu ambapo
matokeo yake ilikuwa kupata uchumi mzuri pamoja na afya, tofauti na sasa ambapo
matokeo makubwa ni uzima wa milele.
Ukiangalia vema, utagundua kuwa,
walipovuja sheria hizo, hali yao ya uchumi na afya ilileta shida, kwa maana ya
kuwa uhusiano wao na Mungu ulipokuwa mubaya, basi matokeo yalikuwa kwenye
uchumi na afya zao. Na hapa utagundua kuwa , suala la dhambi haliachani na
uchimi pamoja na afya ya mtu. Baraka za afya na uchumi zimetajwa kwenye
“Kumbukumbu la torati 28:1….”
Uchumi wa mtu, una misingi yake
katika roho au una mlango wake ambao
hujulikana kama agano, hutofautiana na ngazi ya Taifa japo taifa na uchumi wake
huanzia kwa mtu, mwisho huwa kuna uchumi wa mataifa. Ni mhimu kuelewa mgawanyo
huu wa makundi matatu yanayopokea uchumi kutokana na mfumo wa ulimwengu wa roho.
Kwenye ulimwengu wa roho, uchumi
hukaa ndani ya mtu, ila kuna muda unaoamriwa juu ya mtu huyo na uchumi ulio juu
au ndani yake. Hata hivyo majira yapo kwa kila mtu kulingana na uhusiano wake
ulivyo katiaka ulimwengu wa roho. Mfano, ndoto ya Farao“Mwanzo 41:1….” Haikuwa
inagusa uchumi wa misri pekee bali hata ule wa kanaani. Lakini kilichofanyika
ni kuwa Farao alikuwa na uchumi ndani
yake, lakini Baraka yake ilikuwa Kanaani ambyo ilikuwa ndani ya Yusufu. Yusufu
alikuwa na maarifa juu yauchumi, pia alikuwa na Baraka ya uchumi, ndio maana
alipoingia kwa Potifa, maandiko yanasema Mungu alimfanikisha Potifa mambo yake
kwa mkono wa Yusufu. Lakini Yusufu mwenyewe hakuwa na uchumi, ila akifika
mahali penye uchumi basi Baraka yake ilikuwa inauchanua ule uchumi.
Jambo hili ni mhimu sana kwa kuwa
wako watumishi wengi ambao wana Baraka za uchumi, lakin wao hawana uchumi, si
ajabu mtu kumuombea awe na uchumi imara, na akafanikiwa kwa maombi na namna
alizopewa na mtumishi huyo, lakini unaweza kumkuta mtumishi huyo ana hali
mbaya. Kwa hili kinachofanyika Mungu anamuunganisha na watu wenye uchumi, ili
Yeye aachilie Baraka yake na atakapofanikiwa basi haitakuwa kwa ajiri ya huyo
mtu peke yake bali pia itakuwa kwa ajiri ya huyo mtumishi.
Mali zilizopatikana baada ya Yusufu
kuingia misri zilikuwa kwa ajiri ya misri na watu wa nyumbani mwa Yusufu. Hata
katika habari ya watumishi waliowekwa na Mungu kuwahudumia watu katika Israeli,
Mungu aliweka utaratibu huu, Kiongozi alipewa Baraka, ambazo akiziachilia
kwako, unafanikiwa katika mambo yako, ambapo sasa itakubidi kuchukua sehemu ya
mafanikio yako na umpe huyo kiongozi/mtumishi, na huo ndio ujira wa Mungu
katika Baraka anazozitoa.
Mfano mwingine, nabii Eliya
wakati wa njaa, alimtaka Yule mwanamke amtengenezee mikate, lakini Yule mama
alitaka kulalamika kwa kuwa alikuwa ameishiwa, Eliya akamshrutisha amalizie
unga huo uliobaki, baada ya mama Yule kufanya Kama alivyoagizwa, matokeo yake
ilikuwa kupata chakula tele,Kwa kuwa chombo kile kilijazwa mara dufu. Hapa
tunaomna kuwa Eliya alikuwa Na Baraka, Ni mhimu kujua mahali ambapo au mtu
ambaye ana Baraka zako, Kama marekani walivyogundua kuwa Baraka yao iko
Israeli, wakafanya kuwafadhili na kuwatunza kwa uwezo wao wote na sasa ndio
nchi pekee yenye uchumi imara duniani.
Uchumi wa Taifa
Uchumi huu wa taifa huwa na msingi
wa mtu/familia, uchumi huu una misingi ya kwenye aridhi na kisha humalizikia
kwa watu. Mfano Israeli walikuwa wakitembea Na Baraka za uchumi, hivyo nchi ya
kanaani haikuwa na Baraka hiyo wasipokmuwepo wana wa Israel, ndio maana hata
kama mtu ataitumia ile aridhi, haitatoa mazao, lakini ikitumiwa na mtu wa uzao
wa Israel hutoa mazao sana.
Uchumi wa dunia
Ni uchumi ambao chanzo chake
huanzia kwenye mtu/familia kasha huja taifa ndipo tunapopata uchumi wa dunia,
uchumi huu hutegemea Baraka zilizoko kwenye mataifa. Mfano halisi ni Baraka
aliyopewa Ibrahimu juu ya mataifa, “Mwanzo 22:18”, alifanya agano na Mungu
lililokuwa linagusa maisha ya uzao wake na mataifa. Wakati ibrahimu alipewa
haki ya kuwa Baraka kwa uzao wake na mataifa, Daudi alipewa ufalme Isaya 11:1,
wakati Yakobo alipewa haki ya taifa, ndio maana hadi leo tuna taifa la Israel
ambalo ni jina lake.
Kwa maelezo haya yanaonesha wazi
kuwa Israel kama taifa na nchi ina dhamana kubwa katika uchumi, utawala na
taifa katika dunia.
Tangu hapo mwanzo Mungu
alipoilani aridhi, hakukuwa kana namana ya kusitawi uchumi mpaka kwa Baraka
maalumu, na jambo hili lilianza kwa Ibrahimu, na Mungu aliunganisha hali ya
mafanikio ya watu na mataifa kwa Ibrahimu, “Na katika
uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umeitii sauti yangu
Mwanzo 23:18”. Na katika
ukweli huu, unagundua kuwa hakuna taifa lisilomkiri Ibrahimu ua Yesu kwa
aganola Ibrahimu lenye uchumi imara. Hata hivyo yako mengine yawezayo kutokea
ili kukamulisha maandiko yanayotaja siku za mwisho, ambapo wale wasio wa Kristo
watapata nguvu za Kiuchumi, na kuitawala dunia. Mafano mataifa yanayoanza
kupata nguvu nje ya kumkubali Kiristo ni moja ya alama ya kutimiza ufunuo huu.
Wakati Yesu alipokuja duniani,
kulifanyika mabadiliko ya aina tata
Uchumi, ufalme ambapo ndani yake
tunapata wokovu, na taifa. Na katika kuutazama ukweli huu utagundua kuwa kabla
ya Yesu kuzaliwa mataifa/falme zilizokuwa zinatawala dunia hakuna inayojulikana
kwa sasa, kwa kuwa yalitokea mabadiliko makubwa sana kwenye maeneo hayo matatu
mhimu katika dunia. Mfano, falme kama z aroma, uyunani na uajemi, babeli,
zilizokuja kufuatiwa na Iraq hazina nguvu hata kidogo. Ujio wa Yesu ulifunga
mlango wa ustawi ambapo ilikuwa tangu kwa Adamu, Wakati huo Yesu alichukua hiyo
nafasi akafanyika kuwa mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote wa walio hai na walio
kufa.
Utagundua kuwa nchi karibu zote
zina mafanikio yatokanayo na misingi ya Kiroho, mfano nji ya malekani ina
mafanikio makubwa kwa sababu ya Israel, hata
ulaya pia ina mafanikio kwa sababu ya kumabariki ibrahimu, na wakati
wanapopunguzi zile Baraka hata uchumi wao unayumba, na marekani kwa kuwa anajua
hili, ndiye aliyebaki na msimamo juu ya Israeli na ikiwa atalegeza msimamo wake
basi huu ndio utakuwa mwisho wa kustawi kwake, amtaifa yaliyobaki nai yale
yanayoembea kwa Baraka za ishimael kwa kuwa naye alipewa Baraka hizo japo
hazikuwa kubwa kama za Isaka. Mfano mataifa ya uarabuni yote yanauchumi
unaoelekeana na Baraka za Ishimaeli, na ndio maana hawawezi kuwa sawa na
mataifa mengine yasiyo kuwa na Baraka hizo wala walio chini ya Isaka “mwanzo 21:8….”
Hivyo ugonvi wa mataifa
yanayopokea Baraka kupitia kwa ibrahimu, nay ale ya Ishimaeli hayako kwenye
uchumi ila yako kwenye ufalme. Kwa kuwa tofauti za imani, hazina uhusiano na
uchumi ila ni mambo ya kifalme au utawala, hivyo unagundua kuwa lango la
Ibrahimu kwa upande wa uchumi ni kubwa,na ndio msisitizo mkubwa ulio kwenye
agano, msisitizo wa agano jipya upo kwenye ufalme- uzima wa milele.
Hapa unakumbuka kuwa matazamo wa
watu waliookoka na kushika tu agano jipya, huzingatia na msisitizo wao uko
kwenye habari za ufale-uzima wa milele, sualala uchimi hawahangaiki nalo, lakini Mungu aliviweka vyote kwa maana nzuri
sana, kwa kuwa wokovu ni kwa ajiri ya roho, uchumi ni kwa ajiri ya mwili. Na
kwa kuwa hapo mwanzo kwenye agano la kale msisitzo war oho haukuwepo sana zaidi
ulikuwa wa mwili, ndio maana Baraka zote ambazo zimetajwa kwenye maandiko
zinahusu uchumi na afya tu, wakati wa agano jipya msismitizo ulikuwa kwenye roho, mwili
umeonekana kuwa adui, ndio maana ukisoma barua za Paulo, amezunguzia sana kuwa
mwlil ni Adui Warumi sura ya 6 hadi ya
8. Pia kwenye Mathayo 6:31 “bali utafuteni kwanza ufalme wake(mbinguni) nahaki
yake; na hayo yte mtazidishiwa”
Wapo waonao kuwa ni bora kuwa na
uchimi kwanza kasha wokovu ndipo ufuate, wakiamini kuwa usipokuwa na uchumi bsi
hata suala la wokovu litakusumbua. Na wengine wanaona bora kuwa na wokovu
kwanza kwa kuwa huo uchumi hata ukiukosa bado una tumaini la uzima wa milele.
Lakini tukiyatazama hayo maneno ya Yesu, yanatupa uhakika kuwa ndani ya ufalme
kua uchimi pia , kwa kuwa aliposema na mengine mtazidishiwa alimaanisha na uchumi. Lakini p[ia katika mfano alioutoa wa
lazalo, unaonesha kluwa unaweza kuwa na uzima bado uchumi usiwe nao wakati
uwapo duniani, pia unaweza kuwa na
uchumi lakini uzima usiwe nao.
Hata hivyo suala la wokovu na
uchimi kwa nchi zinazoendelea, bado ni changamoto kubwa, kwa kuwa hata sehemu
kubwa ya mahubiri na mafundisho yao yanahusu uchumi, na muujiza wao mkubwa ni
wa uchumi na afya. Hata hivyo ukweli wa mambo ni kuwa wengi wao maarifa ya
uchumi hawana lakin suala la uzima na afya kwa ujumla lina kipaumbele sana.
Mafano kama utasikia tangazo la mkutano wa injili kwa hakika vittajwa vitu
viwili, yaani wokovu na uponyaji wa magonjwa, hii ni kwa sababu mafanikio
katika uchumi ni kidogo sana hata katika sala zao, angalau kuna mafanikio
katika maombi ya magonjwa japo hata hivyo wengi wao wamekuwa wakihusianisha na
nguvu za giza. Lakini hapo yako matabaka mawili, kuna wale waishio mjini na
hasa angalau wenye mafanikio ya kiuchumi, ambao ni daraja la wafanyabiashara,
wasomi, wafanya kazi, hawa wao hupendelea mahubiri na mafundisho yanayohusu
habari za uchumi, mfanokatika wanafunzi wengi wao hupenda mafundisho na
mahubiri yanayowapa msaada wa namana ya kufanikiwa katika masomo na uchumi kwa
ujumla, habari za wokovu na maarifa ya roho kwao ni changamoto.
Kwa ngazi ya taifa, ni kweli kuwa
kila taifa linakipaumbele chake katika masuala ya roho, vivyo hivyo kila
mtumishi anakipaumbele chake. Na ukivichunguza utagundua kuwa vipo vinavyolalia
upande wa agano la kale, na vingine viko upande wa agano jipya,
Mfano
Afrika kuna vipaumbele kama
wokovu na uchumi, msisitizo wa kenye wokovu uko kwenye uzima wa milele pamoja
na afya ya mwili, pia kupata mafaniko ya kiuchumi.
Amerika na ulaya kuna vipaumbele
kama kuabudu, hii ni kwa sababu wao hawana shida sana ya kiuchumi wala kiafya,
hivyo kwa upande wa Mungu ni watu wenye kupenda kuabudu kuliko kuomba na kutaka
msaada wa Mungu. Kusema hivi haimaanishi kuwa wao hawaombi, isipokuwa mkazo wao
hauko kwenye mambo ya uchumi na afya.
Mashariki ya kati hasa Israel,
kuna vipaumbele viwili, ufalme na ibada, huko ndiko kuna mambo ya kifalme
pamoja na moyo wa ibada.
Uarabuni na asia, kuna vipaumbale
vya wokovu na kuabudu.
Vipaumbele hivi vyote vina chanzo
na sababu zake, mfano kwa upande wa Amerika na ulaya si mahali ambapo mtu anaweza
kuwahubiria habari za kuwa na uchumi na afya kwa kuwa wamejaliwa katika hayo.
Sawa na upande wa Israeli, habari za utawala kwake ni mhimu sana kuliko vyote
kwa kuwa, wao ndio saa ya dunia, hivyo kila mabadiliko yanayotokea kwao
yanaigusa dunia.
Kutokana na maelezo yote hayo
juu ya uchumi ni wazi kuwa suala la uchumi lina misingi yake zaidi ya vile
linavyotazamwa kwa baadhi yetu. Kwa kuwa hakuna mahali popote ambapo uchumi
umehusianisha na shetani, bli uchumi huhusianishwa na dhambi. Hivyo katiuka kuomba
juu ya uchumi ni mhimu kujua misingi iliyojengwa kabla imesimamia kwenye nini,
sulemani aliomba hekima akapewa na utajiri. Kama hakuna hekima basi ni ngumu
sana kuwa na utajiri. Kwa kuwa mataifa mengi yalipofanikiwa kiuchumi walimsahau
Mungu kabisa, uchumi uliwalewesha wakaona kuwa ndio kila kitu.
Hivyo katika kuombea nchi yetu,
ni mhimu tushugulike na dhambi pamoja na hekima ya utawala, hapo tunaweza
kufanikiwa katika kunusuru hali ya nchi yetu kwa upande wa uchumi.
Katika suala la utawala, ni jambo
mhimu sana katika selikali, nchi isipokuwa na viongozi wazuri ni hakika kuwa
haiwezi kuendelea, kwa kuwa suala la maendeleo linagusa uongozi pamoja na mfumo
ulioko. Kwa hali hii, tukitaka amani iwepo katika nchi, ni lazima tushugulike
na uongozi pamoja na lango lake ambalo huwa kwenye mawazo na imani.
Suala la uongozi lina uhusiano
mkubwa na suala la familia na marafiki, kwa kuwa kuna uongozi wa wito, na ule
wa kujiita au kuitwa na marafiki, dini, au familia. Hata hivyo ni mhimu kujua
kuwa suala la uongozi si Baraka bali ni mfumo na mtu aliyewekwa kuwa kiongozi.
Kwa mfano kiongozi wa kwanza wa
Israeli katika habari ya wafalme alikuwa Sauli, katika utawala wake, kitu
kinachoitwa utii hakuwa nacho, na mtu asiye na utii, ina maana hana hekima ya
kutosha, na kama hana hekima ya kutosha, basi huyo lazima atakosea. Na kosa la
kiongozi wan nchi ni pigo kwa nchi.
Nafasi ya uongozi ni mhimu sana
katiaka nchi, kuliko kiongozi mwenyewe, kwa kuwa kiongozi ni mtu tu, lakini ile
nafasi anayopewa inamfanya awe zaidi ya mtu. Hivyo jambo kuwa si kiongozi bali
ni ile nafasi ya kiongozi na kitu ambacho imebeba. Hata hivyo ni mhimu kujua
kuwa kiongozi hafanyi yaliyo yake, bali hufanya ya Yule aliyempa nafasi ya
kukaa kwenye hiyo nafasi. Hakuna mtu awezaye kutimiza kiu na haja ya mioyo ya
watanzania wanaokaribia milioni 47 kwa akili na hekima yake, bila msaada wa
roho. Pia ni jambo bay asana kama hakuna maaono yoyote, tunaweza kulaumu mfumo
uliopo kila siku lakini kama hakuna maono ya Mungu juu ya nchi basi, hakuna
jambo tuwezalo kulifanya. Hivyo kwetu waombaji ni mhimu kuwa na maono ya juu ya
nchi, kasha tusimamie hayo.
Hivyo katika yote yako mambo
makuu matatu, moja ni maono, mbili ni nafasi yenyewe ya utawala kwa lugha
nyingine tunaweza kusema kiti chenyewe, na tatu ni mtu mwenyewe yaani kiongozi
mwenyewe.
Mfano mzuri unaogusa kiongozi
mwenyewe na nafasi yake kwa watu wake ni huu wa mfalme Daudi
“Ndipo moyo wake Daudi ukamchoma baada ya kuwahesabu hao watu.
Naye Daudi akamwambia BWANA, nimekosa sana kwa haya niliyoyafanya; lakini sasa
Ee BWANA, nakusihi uondoilee mbali uovu wa mtumishi wako; kwani nimefanya
upumbavu kabisa. Na Daudi alipoondoka asubuhi, neon la BWANA likamjia nbii
Gadi, mwonaji wake Daudi, kusema, Nenda, nenda ukanene na Daudi, BWANA asema
hivi, nakuwekea mambo matatu; katika haya uchague moja, nikutendee hilo. Basi
Gadi akamwendea Daudi, akamweleza, akamwambia, basi, miaka ya njaa ikujilie
katika nchi yako? Au miezi mitatu ukimbie mbele ya adui zako, huku
wakikufuatia? Au siku tatu iwe tauni katika nchi yako? Fanya shauli sasa,
ufikiri ni jawabu gani nimrudishie aliyenituma. Naye Daudi akamwambia Gadi,
nimeingia katika mashaka sana; basi sasa natuanguke katika mkono wa BWANA; kwa
kuwa rehema zake ni nyingi; wala nisianguke katika mkono ya wanadamu . basi BWANA akawaletea
tauni tangu asubuhi hata wakati ulioamriwa; nao wakafa watu kutoka Dani mpaka
beer-sheba sabini elfu Samweli 24:10-16”
ni hakika kuwa ukisoma maneno haya,
unaweza usitamani nchi yetu kuwa kwenye nafasi hiyo mbele za Mungu, ukitazama
yanayofanya na baadhi ya viongozi. Kwa kuwa kama kosa la kiongozi linaweza
kusababisha uchungu wa msiba kiasi hicho, ina maana kwa uongozi wetu basi wat
wangeisha. Ni bora kuwa hivi kuliko kuwa na nafasi kubwa mbele za Mungu, bila
kushugulikia nafasi ya kiongozi na kiongozi mwenyewe.
WAJIBU WA SELIKALI KATIKA MAMBO YA KIJAMII MBELE ZA MUNGU
Huduma zote za jamii kama vile, hospitali, umeme, maji,
shule, soko, n.k ni wajibu wa selikali, lakini hata hivyo mambo haya
yameunganishwa na uchumi, kwa kuwa uchumi usipokuwa mzuri basi huduma hizi
hazitatolewa vyema.Hivyo mambo makuu mawili yanalifanya hili liwe sawa.
WAJIBU WA KANISA JUU YA SELIKALI
UHUSIANO
WA LANGO HILI LA KANISA NA NCHI PAMOJA NA TAIFA:
Kama ilivyoelezwa mwanzo kuwa lango la kanisa kuhusianishwa
na nchi na taifa ni kuwa: mpango wa kwanza kabisa wa Mungu ilikuwa nchi na
taifa vitawaliwe kwa sheria za mbinguni au za ulimwengu wa roho. Na wakati
mwanadamu alipokuwa kwenye bustani ya
edeni namna iliyokuwa inamuongoza ilikuwa namna ya roho. Lakini ulipotokea uasi
ulipindua ile namna ya roho iliyokuwa imewekwa kumuongoza mwanadamu na
kuchukuliwa na namna ya mwili. Lengo la Mungu kuweka namna ya roho ni kwa kuwa
vitu vya roho viko imara na ni vya uhakika, na kwa kuwa Mungu ni roho basi
ilikuwa ni lazima mwanadamu aongozwe na namna ya roho na Mungu alikuwa
amemfunika na namna ya roho inayotosha kuongoza dunia.
Kwa kuwa dhambi
ilitokea na kuvuruga mfumo huo, mwanadamu alikuwa anaishi kwa kuongozwa na namna
ya dunia na wara siyo ya Mungu, isipokuwa kwa wachache waliopata neema ya
kumuelekea Mungu aliwapa namna hiyo ya roho. Mfano Henoko.
Ilipofika wakati wa Ibrahimu Mungu alipoingia Agano na
Ibrahimu baada ya kuona kuwa Ibrahimu atamuelekea Mungu. Baada ya miaka mia nne
Mungu alianza kutekeleza Agano lake. Alimtumia Musa kutekeleza mambo ya agano
lake na Ibrahimu, lakini wakati huo bado hata wana wa Israeli walikuwa
wanatawaliwa na namna ilele ya mwili. Na kwa kuwa ili uishi na Mungu ni razima
uongozwe na taratibu za Mungu ambazo ni za urimwengu wa roho, Mungu alimchukua
Musa na kumueleza utaratibu mpya wa maisha yao wanayotakiwa kuishi na wara si
kama zamani. Walipewa amri kumi na sheria ndogondogo zilizoikamilisha utaratibu
wanaotakiwa kuishi, ikumbukwe sheria hizi zilikuwa zimetoka kwenye ulimwangu wa
roho wa Mungu Baba Mwenyezi, kwa kuwa hakuna sheri itokayo kwa Mungu isiyo ya
ulimwengu wa roho( Warumi 7:14).
Hapo Mungu alitaka kuwatengenezea maisha aliyokuwa
ameyakusudia tangu mwanzo kwenye bustani ya Edeni kabla ya uasi. Baadae wakati
wa nabii samweli Wana wa Isreli
walikataa kuwa chini ya utawara wa Mungu badara yake wawe na mfalme
atakayewaongoza, ambaye watakuwa wanamuona na kuenda naye vitani kama
ilivyokuwa kwa mataifa mengine.
Mungu aliwakubalia na akafanya ule Mlango aliokuwa
anautumia katika kuwaongoza akauweka juu ya namna hiyo ya utawara waliyoitaka
ya kuwa na mfalme mwanadamu. Mlango huo ulikuwa kanisa, na uliwekwa kuwa
kiongozi wa selikari ya mwili waliyoitaka, hivyo japo kuwa alikuwepo kiongozi
wa mambo ya mwili, lakini bado Mungu aliweka kiongozi katika lango lile la
kanisa kuwaongoza watu na mfalme wao (1 Cor 6:4).
Na ni ukweli kuwa hukuna mfalme aliyewekwa katika Israeli na asipewe kiongozi
yaani nabii wa kumuongoza, hata kama angekuwa imara kiasi gani lakini bado
kwenye lango la kanisa kuna kiongozi aliyewekwa kuwaongoza wote. Hata wakati wa
Daudi japo alionekana kuwa imara sana mbele za Mungu, lakini hiyo ilikuwa
nafasi ya kifalme , kwenye nafasi ya kanisa manabii walikuwepo kama Mwongozo,(2Samweli
24:10-19)
Maelezo hayo
yanaonesha kuwa kusimama kwa nchi na taifa kunategemea pia namna kanisa
lilivyosimama.
Kanisa ni mwangalizi na kiongozi wa selikali na watu wake,
na tunaposema selikali na watu wake inamaanisha kuwa kanisa linaiongoza selikali kufanya sawasawa
na mapenzi ya Mungu ili Mungu asiadhibu nchi hiyo na taifa hilo.
Pia kanisa ndiyo kiongozi wa viogozi wa selikali, mwenye
wajibu wa kuwafanya watimize mapenzi ya Mungu katika nchi na taifa kwenye lango
hilo la uongozi katika mwili.(1 Cor 11:16).
Nabii Danieli aliyekuwa amewekwa kusimama kwenye lango la
kanisa alipoona mambo hayako sawa aliingilia kati na kuomba maombi mazito ya
kuepusha hasira ya Bwana isiipate nchi na taifa lake, (Danieli 9:3-19), pia
Ezekieli alipewa kazi ya kufanya ili kufuta uovu wa nchi na taifa lake kwa kuwa
yeye alikuwa kwenye lango la kanisa (Ezekieli 4:4-9).
Roho Mtakatifu akujaze zaidi ya ulichosoma na kujifunza
kwa msaada zaidi niandikie kwenye email: gkazili@yahoo.com, au tuma ujumbe no 0765-129960
Mwl. Goodluck Kazili
Labels:
KUOMBEA NCHI
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
UTATU MTAKATIFU NA KUSUDI KWA MTU (MUNGU BABA, MUNGU MWANA, MUNGU ROHO MTAKATIFU)
UTATU
MTAKATIFU NA KUSUDI KWA MTU
(MUNGU BABA, MUNGU MWANA, MUNGU ROHO MTAKATIFU)
DONDOO:
UTANGULIZI
SEHEMU YA KWANZA
Ø NAFASI
YA MUNGU BABA KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
Ø NAFASI
YA MUNGU MWANA KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
Ø NAFASI
YA ROHO MTAKATIFU KATIKA DUNIA/MWANADAMU/MTU
SEHEMU YA PILI
NYAKATIA TATU MHIMU
Ø KUUMBWA
ULIMWENGU
Ø BAADA
YA UUMBAJI AGANO JIPYA
Ø UJIO
WA KRISTO: AGANO JIPYA
SEHEMU YA TATU
UGAWAJI WA MADALAKA
Ø KUTOKA
KWA MUNGU HADI KWA YESU KRISTO
Ø KUTOKA
KWA YESU KRISTO HADI KWA ROHO MTAKATIFU
SEHEMU YA NNE
MAMLAKA NA UHUSIANO BAADA YA UGAWAJI MADALAKA
Ø MAMLAKA
YA MUNGU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAMU
Ø MAMLAKA
YA YESU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAUMU
Ø MAMLKA
YA ROHO MTAKATIFU NA UHUSIANO WAKE NA MWANADAMU
SEHEMU YA TANO
UMHIMU NA ULAZIMA WA KUJUA NA KUFUATA UTARATIBU HUU
Ø KUSUDI
LA MUNGU KWA MWANADAMU
Ø UTILIMILIVU
WA KUSUDI
Ø HITIMISHO
SEHEMU YA NNE
MAMLAKA NA UHUSIANO BAADA YA
UGAWAJI MADALAKA
Ni mhimu kufahamu kuwa utendaji
kazi wa Mungu umebadilika sana kulingana na vipindi ambavyo vimepita. Hali hiyo
inapelekea mfumo pia wa mwanadamu kutakiwa kubadilika katika uhusiano wake na
Mungu. Kitu kilichowakwamisha wayahudi hadi leo wengi wao wasimwamini Kreisto
ni kutokujua mabadiliko ya utendaji kazi wa Mungu na uhusiano wake na wanadamu.
Japo maandiko yalikuwa yametangulia kueleza wazi kuwa kutakuwa na mabadiliko:
Yeremia 31:3
Hakika Mungu ni mmoja lakini
mwenye nafsi tatu za utendaji kazi, kusema mwenye nafsi tatu ni mhimu kuelewa
kazi ya nafsi ni kupambanua na kufanya maamuzi. Hivyo kwa ufupi na tafsiri ya
karibu tunaweza kusema kuwa Mungu anapambanua na kufanya maamuzi katika maeneo
matatu au kwa namana tatu. Hivyo kwetu wanadamu husema yuko Mungu Baba, Mungu
mwanaNeno, na Mugnu Roho Mtakatifu: kwa maana wako watatu washuhudia[mbinfuni, Baba, na Neno,
na Roho Mtakatifu, na watatu hawa ni umoja. Kisha wako watatu washuhudiao
duniani], Roho, na maji, na damu na watatu hawa hupatana kwa habari moja,
(1Yohana 5:8-9a)
Hata hivyo ni mhimu kujua kuwa,
utenfaji kazi huo, ambao umebadilika katika vipindi maalumu ambavyo vina maana
kubwa kwetu.
Ukisoma kwenye maandiko
matakatifu utakutana na wakati ambao Mungu alikasilishwa na akaamua kumupa
mamlaka malaika ya kuwaongoza wana wa Israel; kutoka
32: 34: basi sasa uende ukawaongaze watu
hawa mpaka mahali paloe ambapo nimekwambia habari zake; tazama Malaika wangu
atakutangulia; pamoja na hayo siku nitakayowajilia nitawapatiliza kawa ajili ya
dhambi yao.
Hata hivyo tuna wakati wa
kujiuliza kwa nini Mungu hakuwapa Mwana ndiye awaongoze; hakika yake ni kuwa muda wa
Mungu kujifunua kupia Mwana ilikuwa bado, pia ni wazi kuwa nafasi ya taifa moja
hakukuwa na ulazima wa kujifunua kupitia mwana wakati ulimwengu mzima ulikuwa
na shida, hivyo kwao malaika alitosha, hata hivyo ukiendelea kusoma unaona kuwa
Musa alikataa kwenda na malaika.
Na jambo hili ndilo ambalo
limefanyika kwa wayahudi japo si kwa kukataa kwenda na Yesu ila kwa kutokujua
kuwa utendaji kazi katika dunia hauko tena chini ya nafsi ya Mungu Baba bali
Mungu mwana.
Ilipofika kipindi Fulani cha
wakati kama unabii ulivyokuwa umeonyesha Mungu alihamisha mamlaka yake ya
kuisimamia dunia na kuweka chini ya Nafsi yake iliyo mwana yaani nafsi ya pili
ya utendaji kazi ambayo ni Mwana;
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa Tumepewa motto
mwanamume na uweza wa kifalme utakuwa bagani mwake; naye ataitwa jina lake,
Msahuri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani (Isaya
9:6). Pia kaitka Mathayo 1:21Naye atazaa
mwana , nawe utamwita jina lake Yesu, maana ndiye atakayewaokoa watu wake na
dhambi zao, Hayo yamekuwa ili litimie neon lililonenwa na Bwna kwa ujumbe wa
nabii akisema, Tazama bikra atachukua mimba naye atazaa mwana; Nao watamwita
jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.
Ugawaji wa mamlaka hii ulikuwa na
maana kubwa sana, hasa kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu, kwa maana ya kuwa
Mungu aliamua aitoe nafsi yake ambayo ni mwana ili aifanye kuwa upatanisho kwa
dhambi kati ya wanadamu na Mungu. Hii humaanisha kuwa Mungu hatamtazama
mwanadamu tena moja kwa moja isipokuwa ataitazama nafsi yake/mwana kisha ndani
yake atamuona mwanadamu. Na kwa kuwa katika nafsi hiyo ilitolewa damu ambayo
huwasafisha dhambi zao, hivyo Mungu hataiona dhambi kwa kuwa watakuwa
wametakaswa.
Haikutosha tu kuzaliwa kwa Yesu
na kuwapa msingi wa namana ya kuishi maisha mpya yaani ya Kikristo, bali
walitakiwa wakae nae ili kupata msaada zaidi wa kuendelea kuufahamisha
ulimwengu hiyo namna mpya na ukombaozi ulioletwa na Mungu kwa wanadamu kupitia
nafsi Yake. Na kwa kuwa kazi ya nafsi ya pili yaani mwana ilikuwa kutoa damu na
maji kwa ajili ya ukombozi na utakaso wa dhambi, kazi ya kuendelea kushuhudia
ukombozi hou haikuwa ndani ya nafsi mwana balili ilikuwa ndani ya uwezo wa
nafsi Roho Mtakatifu; hivyo baada ya nafsi Mwana kumaliza kazi yake ilikuwa ni
lazima nafsi nyingine ije kwa ajili ya ukamilisho.
Hapa huwa kuna changamoto kubwa
kwa kuwa watu wengi wanaishia kwenye nafsi ya pili yaani mwana; wakijua kuwa
baada ya kuokoka, kubatizwa na kutakaswa kwa damu ya Yesu hudhani kuwa mambo
tayari, na wakati mwingine hufikri wanaweza kuyaishi hayo maisha ya utakatifu
walioupata kupitia kwa mwana. Kumbe ni lazima kumalizia na hatu nyingine mhimu
sana ya nafsi ya tatu yaani Roho Mtakatifu kwa kuwa huyo nidye kila kitu baada
ya mtu kuokoka, kubatizwa na kutakaswa.
Maandiko yameweka wazi mambo haya
japo watu hawayazingatii, na ndio maana wanakwama sana katika huduma zao, imani
yao, na hata katika kutunza wokovu hou walioupata.
Ukisoma habari za Yesu ni baada
tu ya kubatizwa alichukuliwa na Roho kwenda kujaribiwa nyikani. Kwa hali ya
kawaida kulikuwa na haja gani ya Yesu kuchukuliwa na Roho Mtakatifu; (Math
4:1). Baada ya Yesu kukaribia kuyondoka
kwenda mbinguni aliwaambia wanafunzi/ mitume; Lakini mtapokea nguvu, akisha kuwajilia juu
yenu Roho Mtakatifu;nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika
Uyahudi wote, na Samaria na hata mwisho wa nchi, (matendo 1:8)
Hawa hawakuwa na sifa ya kuwa
mashahidi wa Yesu kabla Roho mtakatifu hajawajilia, ni mhimu kujiuliza vema
maana hawa wanafunzi walikuwa wamekaa na Yesu mda wa miaka mitatu na nusu
akiwafundisha tena wakitembea naye na wakihubiri
na kufanya ishara na maajabu mengi, lakini bado kuondoka kwa Yesu
walikuwa hawana sifa za kuwa mashahidi wake hadi Roho mtakatifu atakapowajilia.
Ukijiuliza unagundua kuwa kazi hiyo
haikuwa ya Yesu/Mwana bali ilikuwa imewekwa ndani ya Roho Mtakatifu.
Kwa uelewa zaidi kuna wakati
wanafunzi wa Yesu hawakuwa wanapendezwa na taarifa za kuwa Yesu ataondoka,
kisha Yesu akawaambia; Lakini mimi nawaambia iliyokweli; yawafaa ninyi mimi
niondoke, kwa maana mimi nisipoondoka, huyo msaidizi hatakuja kwenu, bali mimi
nikienda zangu, nitampeleka kwenu,(Yohana 16:8). Hapa unaona kuwa
kumbew Roho Mtakatifu yupo, lakini hajapewa hiyo kazi, na Yesu anasema
nitampeleka kwenu halafu ukiendelea kusoma zinatajwa kazi atakazozifanya ambazo
amepewa mamlaka haimaanishi ndizo kazi anazoziweza tu ila kwa duniani amekuja
kufanya hizo; Naye
akisha kuja huyo natauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki,
na hukumu, (Yh 16:9).
Ukipendezwa na somo hili na unahitaji mwenelezo wake tuma email gkazili@yahoo.com au tuma ujumbe no ya simu 0752165609 au 0716050663.
Labels:
SK-Siri Kuu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Jisajili kwenye:
Maoni (Atom)
Kunihusu
- Ni Siri Kuu - The Great Mystery
- "Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
.png)