Ni Siri Kuu - The Great Mystery

Ni Siri Kuu - The Great Mystery
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.

Jumapili, 15 Aprili 2018

NGUZO MOJAWAPO YA KUKUFANIKISHA KATIKA KILA OMBI UOMBALO



UAMUZI WA DHATI KUHUSU KUOMBA
Ili uweze kuomba vema na kufanikiwa katika kuomba kwako, pamoja na mambo mengine ni lazima uwe umefanya maamuzi ya kuomba. Maamuzi yanakuja kama matokeo ya sababu ya kutaka kuomba. Si mara nyingi sana watu wanaingia kwenye kuomba wakiwa wamefanya maamuzi, ni mara chache sana mtu anaweza kuingia kuomba akiwa amefanya maamuzi ya kuomba.
Unaweza kuwa na sababu za kuomba lakini usifanye maamuzi ya kuomba, hivyo ukaoma tu kwa sababu inakubidi uombe, ngoja niombe lakini hujafanya maamuzi ya kuomba. Mara nyingi hatuombi kwa sababu tumeamua kuomba, bali tunaomba kwa sababu imetulazimu kuomba, na kwa kuwa hakuna njia nyingine, au pamoj na njia nyingine ngoja pia niombe tu. 
Kwa nini ni lazima kufanya maamuzi wa dhati ndipo uombe
ü  Uamzi ndiyo siraha pekee ya mtu kuweza kuomba na kufika mwisho, au kuweza kufaidi uombaji anao uomba
ü  Utaelewa thamani ya kuomba ikiwa tu umeomba kwa maamuzi
ü  Utapata unachopata kwa uzuri halisi ikiwa utaomba kwa maamuzi
ü  Utajifunza zaidi katika uombaji wako ikiwa utaomba kwa maamuzi
   Ukioba bila kuamua kuomba,
§  hutaona thamani ya kuomba
§  hutapata kilicho katika kuomba
§  hutatambua nafasi yako katika kuomba
§  hutajua Mungu anahusikaje wakati  unapoomba
§  hutajua unaathili upande wa adui kiasi gani ,na
§  hutakuwa na msimamo katika kuomba
Uamuzi wa kuomba
Ni matokeo ya picha unayoiona ya jambo/mtu/kitu ambacho ni hitaji kwako. Picha hiyo ni ya imani, inayokuelekeza  umuhimu na thamani ya kuomba, matokeo ya kuomba, maelekezo ya kuomba, nguvu na mamlaka ya kuomba.
Uamuzi wa kuomba unakuja baada ya kuona umuhimu na thamani ya kuomba, tena ni pale unapokuwa umeona/unaona matokeo ya kuomba hupo utakapoomba, siyo imani ya kuamini tu bali unaona katika ufahamu hayo matokeo, tena ni hapo yanapokuja maelekezo ya kuomba, na katika hayo yote unahisi na kusikia nguvu ya kuomba na kuwa na mamlaka ya kiuombaji kuhusu hilo hitaji.
Namna ya kufanya maamuzi ya kuomba unapotaka kuombea jambo/mtu
Mambo haya  4 ni lazima uwe na uwezo wa kuyafanya au kuyapata ndipo utakapofanya Maamuzi
Ø   Tafuta kwanza ufahamu wa kiroho kuhusu jambo/eneo/mtu/kitu unachotaka kuombea
Danieli alifanya maamuzi ya kuomba; maamuzi hayo yalitokana na ufahamu alioupata kuhusu jambo analotaka kuomba, ufahamu ambao aliupata kwa kuvisoma vitabu vilivyoandika habari za kiroho kuhusu Yerusalemu. hapa maandiko hunena “katika mwaka wa kwanza wa kumiliki kwake, mimi Danieli, kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu miaka ambayo Neno la BWANA lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani miaka sabini, nikwamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na  majivu. (Danieli 9:2-3)”
Ø  Kutambua umuhimu na thamani ya kuomba
Maamuzi ya dhati yanategemea thamani unayoiona katika jambo unalotaka kulifanya, thamani hii inategemea msingi uliyonayo katika kuomba, na unaamini kuomba kwa asilimia ngapi, na tafisiri ulizonazo na shuhuda kuhusu kuomba. Unaweza ukawa una historia mbaya kuhusu mafanikio ya kiuombaji, yaani huna imani sana na mafanikio yanayopatikana katika uombaji. Mtu anayejua uombaji ni nini na uwezo wake huthamini sana kuomba na huona kuomba kuwa kitu cha thamani kwenye maisha yake kuliko chochote kile. Jambo hili linawezekana tu kwa mtu ambaye amefuatilia masuala ya kiuombaji, shuhuda mbalimbali kuhusu uombaji, ahadi za kiuombaji katika Neno la Mungu, mafanikio ya watu walioomba katika maandiko.
Twafahamu habari za Mwanamke Hanna, jinsi alivyofanya maamuzi ya kuomba, na kufanikiwa vema kupata alichotaka.  (1Samweli 1:10)  ukiendelea unaona matokeo ya kuomba kwake, na jinsi tena alivyozidi kuomba kama shukrani yake kwa Mungu. (sura ya 2)
Elisha akaomba kusema na Bwana kuhusu kumfumbua macho mjakazi wake ili aone ulinzi aliowawekea Bwana dhidi ya maadui waliokuwa wamewazunguka (2 Wafalme 6:17) Twafahamu habari ya Hezekia; “Basi Hezekia akajigeuza, akaelekeza uso wake ukutani, akamwomba BWANA, akasema, Ee BWANA. Ikawa, Neno la BWANA likamjia Isaya, kusema, Enenda ukamwambie Hezekia, BWANA, Mungu wa Daudi, baba yako, asema hivi, Mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka kumi na mitano. (Isaya 38:2,4,5)”
Ø  Matokeo unayoona wakati utakapokwisha kuomba
Hupaswi kuona matoke ya kuomba baada ya kumaliza kuomba, bali matokeo huwa yanaonekana kabla ya kuomba. “Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana. (Waebrania 11:1)”. Eliya alimwambia Ahabu kuwa nvua inakuja kabla hajaomba, alipoenda kuomba ilimgharimu kuomba mara saba, kama si maamuzi ya kuomba aliyokuwa ameyafanya ambayo yalitokana na kuona matokeo ya kuomba kabla hajaomba, angeishia njiani kwenye kuomba kwake.
Kuona matokeo ya kuomba hiyo ndiyo imani halisi. Maandiko hunena wazi kuwa “imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana”. Ni kusema kuwa, kuwa na uhakika, ni kuona kile kitu ambacho hakionekani bado kwa macho ya nyama. Imani inakupa uhakika wa kitu kabla ya wewe kukipata, imani inkuonyesha kitu ambacho hakionekani nje ya imani, ndiyo maana imani ni kwa vitu visivyoonekana tu basi. “Akasema nitawaficha uso wangu, nitaona mwisho wao utakuwaje; Maana, ni kizazi cha ukaidi mwingi, watoto wasio imani ndani yao. (Kumb 32:17)”
Imani si kuamini tu, bali ni kuona ambako ndiko kunakopaswa kukupe kuamini. Kuamini ni ile inayokuja baada ya kuwa na uhakika, uhakika ambao umekuja baada ya kuona ishara au hali au kitu au kidokezo kinachothibisha hilo jambo japo bado halijadhilika au halijatimia au halionekani wazi. Imani ni ule uhakika anaokuwa nao mtu ndani yake kuhusu jambo, hali, kitu, mtu n.k.
Kuwa na imani ndogo au kubwa ni kiwango cha uhakika ulionao juu ya hilo jambo/kitu katika kutenda kwake, kutimia kwake, kufanikiwa kwake n.k
Huo uhakika, ili uwepo, ni hadi mtu awe na hati milki ya uwezo, nguvu, mamlaka, neema na rehema ndani yake vilivyo vya Mungu. Ambavyo mara zote vinakuja kutokana na kumjua Mungu. Imani chanzo chake ni kusikia kusikia ambako huja kwa Neno la Kristo. Kusikia huko si tu kule kusikia Neno la Mungu, ni kusikia ambako kumekuja kama neno lakini Neno la imani. Neno lenyewe ambalo ni imani linaingia ndani yako ndipo unapokuwa na uhakika. Neno la Mungu ndiyo Kweli, hivyo huwezi kuwa na uhakika yaani ukweli kama si Neno la jambo hilo.
“Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba Yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao. (Waebrania 11:6)”
Kuwa na imani kunahusisha mambo mengi, moja kubwa ni kumjua Mungu, ambako kunatiwa nguvu na wema, maarifa, kiasi, saburi, utauwa, upendo. (2 Petro 1:5-7) - (9)
Ø  Maelekezo ya kuomba
Maelekezo ya kuomba yanakusukuma kufanya maamuzi, ambao unatokana na utayari unaoupata kwa kuwa unamaelekezo ya kuomba.
Kuomba ni safari, ambayo kuianza au kutoianza kunategemea uhakika wa safari (Imani), kunategemea Maelekezo ya safari, tena kunategemea umuhimu wa safari.
Maelekezo ya namna ya kuomba ni nyenzo muhimu katika kukusukuma kufanya maamuzi ya kuomba. Maelekezo kuwa nayo au kutokuwa nayo kunategemea na kiwango cha neno ulichonacho kuhusu jambo hilo, pia inatokana na kiwango cha uhitaji kinachoonekana ndani yako, tena inategemea mazoea uliyonayo kuhusu kuomba, tena inategemea kiwango cha imani uliyonayo katika Mungu, na zaidi sana inategemea uhusiano ulio nao na Roho Mtakatifu. Kuwa na maelekezo ni sawa na kupata utaratibu wa namna utakavyofanya kazi fulani, jambo hilo litakusukuma kuwa tayari kuifanya, kadhalika maelekezo kuhusu kuomba yanakusukuma kufanya maamuzi maana unajua kwa hakika unachotakiwa kufanya na mwisho wake utakuwa upi.
(Daniel 9:1-22)
Ø  Mamlaka, nguvu na kibali cha kuombea jambo hilo
Kuwa na kibali au mamlaka ya Mungu ndani yako inakusukuma kufanya maamzi ya kuombea jambo. Kama ndani yako husikii kuwa na mamlaka, utaombea jambo bila kufanya maamuzi, kwa sababu huwezi kufanya maamuzi kama ndani husikii kuwa na mamlaka au kibali cha jambo hilo. Yesu alisema, ni nani atakaye kujenga mnara, asiyeketi chini kwanza na kuhesabu gharama?, huwezi kufanya maamuzi ya kuomba  ikiwa hujisikii kuwa na uwezo wa kuombea jambo hilo na kufika mwisho.
Hivyo ili mtu uweze kufikia kufanya maamuzi katika kila hitaji unalotaka kuomba, ni lazima ujitahidi kuwa na hayo mambo manne. Ni vema sana mtu ukiwa nayo ya kudumu, si kwa ajili ya hitaji moja tu.
Msisitizo kuhusu maamuzi katika kuomba
Maamzi ni msingi muhimu sana, katika kufanikisha kuomba kwako. Ni mara chache sana kutokea kuomba ukiwa umefanya maamuzi kisha usifanikiwe katika kuomba kwako. Kati ya msingi unaowakwamisha wengi katika kuomba kwao ni kuomba kabla/bila kufanya maamzi ya kuomba. Huwezi kuona rahisi kuwa unaweza kuomba bila kufanya maamuzi, na unaweza kujiuliza tuna maana gani kusema kuwa mtu anaweza kuomba bila kufanya maamuzi. Lakini ni wazi na ni kweli na wengi wanaomba bila kufanya maamzi, maana ukienda kwenye ibada ya maombi, kisha ukaambiwa tunataka tuombee jambo furani, ukaomba kama Dakika 10, je! Utafuatilia kama lile jambo uliloliombea kwenye kipindi limefanikiwa au bado?, ni adimu sana kutokea kuuliza.
“Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisita-sita, roho yangu haina furaha naye.(Waebrania 10:38)”
Huwezi kusema wakati unaomba ulifanya maamuzi, maana kama ungekuwa umeombea jambo ulilolifanyia maamzi lazima kwenye kuomba kwako ungepata majibu hapo hapo, si jibu lile la suruhu ya jambo lakini hata ile tu kujua kuwa ni  nini kimefanyika na unategemea matokeo gani, na hapo utayangoja ili uyaone kwa hakika.
Kuna maombi machache sana kwenye maisha yako ambayo unaweza kuwa umeyaomba ukiwa umeyafanyia maamuzi. Na utagundua kuwa karibu kila jambo uliloombea kwa kufanya maamzi basi ulijibiwa/ulifanikiwa.
“kuomba kwake mwenye haki, kwafaa sana akiomba kwa bidii” (Yakobo 5:16b)
Maamuzi ya kuomba siyo yale ambayo mnafanya maamuzi kwa kusema tumeamua kuombea kitu fulani. Bali ni ile ya maamuzi ya kuomba kwa hakika bila kuchoka wala kukata tamamaa hadi upate unachotaka. Inakuja kutokana na uhakika wa njia hii ya kuomba kuwa ndiyo pekee itakayokufikisha katika hali au jambo unalolihitaji.
Mfano mtu anasema nimeamua niombee jambo hili kwa wiki mbili huku nikifunga ili jambo hili liishe.
Mfano halisi wa mtu aliyefanya maamuzi ya kuomba ni habakuki. Maandiko yanatueleza hivi “ Mimi nitasimama katika zamu yangu, nitajiweka juu ya mnara, nitaangalia ili nione atakaloniambia, na jinsi nitakavyojibu katika habari ya kulalamika kwangu. (Habakuki 2:1)”
Kadhalika Eliya, alifanya maamuzi ya kuomba, hapa maandiko hunena kwanza “Eliya alikuwa mwanadamu mwenye tabia moja na sisi, akaomba kwa bidii mvua isinyeshe, na nvua haikunyesha juu ya nchi muda wa miaka mitatu na miezi sita, akaomba tena, mbingu zikatoa mvua, nayo nchi ikazaa matunda yake. (Yakobo 5:17-18)”
Eliya, anatajwa kuwa ni mwanadamu mwenye sifa/tabia kama za kwetu, lakini katika uwepo wa maamuzi aliomba na kufanikiwa. Kilichomfanikisha ni kitu gani ni maamuzi, maana kama siyo maamuzi asingeomba kwa bidii. Na alipoomba mara ya kwanza na hakupata mafanikio angekata tamaa na kuacha, lakini kwa kuwa alishafanyia maamuzijambo analotaka kulifanya hivyo kuomba kwake haikuwa tu kuomba, bali kuomba hadi apate anachoomba.
Hapo juu tumesoma habari za Daniel, ambaye aliomba maombi yasiyokuwa ya kawaida na akafanikiwa, lakini kama ukitazama kilichomsaidia utaona kuwa, ni maamuzi aliyoyafanya ambayo yalikuwa yanatokana na ufahamu alioupata katika kuvisoma vitabu.
 Mwl. Goodluck Kazili (Ni Siri Kuu – The Great Mystery)

Kunihusu

Picha yangu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Tafuta katika Blogu Hii