Ni Siri Kuu - The Great Mystery

Ni Siri Kuu - The Great Mystery
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, Baba, kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako.

Jumatatu, 29 Februari 2016

THAMANI YA MTU WA NDANI (NAFSI)

SK-Siri Kuu
 

THAMANI YA MTU WA NDANI (NAFSI)

Na Mwl; Goodluck Kazili

"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?. (Mathayo 16:26)
Hakuna kitu chenye thamani katika ulimwengu huu, kama nafsi ya mtu. Nafsi yako ndicho kitu chenye thamani kuliko chochote unachokijua katika ulimwengu huu, ndiyo sababu Yesu aliuliza au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake?. Je! ulimwengu mzima thamani yake inalingana na thamani ya nafsi yako? hapana haiwezi kufikia. Na hivyo hakuna chenye thamani kuliko nafsi yako.

Hata hivyo ajabu ni kwamba, mtu mwenyewe haithamani hiyo nafsi yake bali anathamini vitu ambavyo nafsi ilipewa ili kuvitumia. mfano mtu hataki kuokoka kwa madai kuwa atashindwa kuifaidi dunia na raha yake. Mtu kama huyu, tatzo lake ni ufahamu tu wa kutokujua thamani ya kila kimoja na matumizi yake na sababu ya kuwekwa hivyo vitu.

Hata hivyo, ni muhimu kujua kuwa kuna utu wa ndani na utu wa nje. tena utu wa nje uliumbwa kwa ajili ya utu wa ndani, kama tu nyenzo ambayo mtu wa ndani anapewa ili atumie kwa matumizi yake.


NI SIRI KUU

Na Mwl; Goodluck Kazili

"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)


"A work shop of Holy Sprit in man is mind"

"A work shop of devel in man is mind"

"A work shop of mind in man is brain"

If you fail to protect and control you're mind, you can not be you, you will be one of someone,

Jumatano, 24 Februari 2016

POWER OF VISION (NGUVU YA MAONO)


SK-Siri Kuu


 


POWER OF VISION (NGUVU YA MAONO)
Na Mwl; Goodluck Kazili 
“Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na chi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba, kwa kuwa ndivyoilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)
Dondoo muhimu za kujifunza kuhusu Maono (kwa ufupi)
Ø  Tafsiri ya maono
Ø  Maono kuhusu maisha
Ø  Nvugu ya maono
Ø  Namna ya kuwa na maono
Ø  Funguo za maono
Ø  Kiapo katika maono
Ø  Mipango ya maono
Ø  mwisho
TAFSIRI YA MAONO
Maono ni picha ya mbele kuhusu jambo/ kitu/hali/ inayopigwa na kudhihilishwa kabla, ili kutengeneza mazingra ya kufanikiwa kwake
Maono yanaeleza jambo lisilokuwapo bado kwa wakati uliopo sasa lakini lipo mbele, hivyo ile picha inayopigwa na kuletwa kwa mtu ili afanye jambo kwa ajili ya kufanikiwa kwake.
Hata hivyo maono yapo ya aina nyingi, lakini maana hiyo inagusa maono karibu ya namna zote. Katika somo hili, maono yanayolengwa ni yale yanayohusu maisha ya mtu.
MAONO KUHUSU MAISHA
Kila mtu katika maisha ana viengele 4 vinavyogusa maisha yake, vitu hivyo ni Yeye kuhusiana na Mungu, uchumi, afya na familia.
Hivyo, mtu analazimika kuwa na maono yanayogusa mambo hayo manne . kwa ulazima huo, binafsi ni lazima uwe na:-
1.       Maono ya Kiutumishi (spritual Vision)
2.       Maono ya kiuchumi (economical vision)
3.       Maono ya kifamilia (family vision)
4.       Maono ya kiafya (health vision)

Hata hivyo, haiwezekani hayo yote kuwa maono halisi ndani yako kisha ukayafanikisha vema. Unapaswa kuwa na maono makuu, ambayo huwa ni moja.  Unakuwa na maono ambayo ni makuu (main vision), kisha unakuwa una maono yaliyo chini ya maono makuu (sub vision).
Mfano mimi Goodluck Kazili maono yangu ni haya “Kumtumikia Mungu kwa kiwango cha juu cha kwanza, katika yote, kwa vyote, sawa na mapenzi yake” (to serve the LORD GOD to the best level of all, with all in His will). Kwangu haya ndiyo maono makuu (main vision), lakini chini yake nina maono mbali mbali ya kiuchumi, ya kiafya, na ya kifamilia. Mfano katika maono ya uchumi, nina picha (maono) ya kuwa na shule pamoja na chuo, tena nina picha (maono) ya kuwa na miradi kadhaa ya fedha, n.k.
Hivyo ninachofanya ni lazima haya maono yawe chini ya maono makuu ambayo ni ya kumtumikia Mungu. Hivyo, pamoja na kuwa nitamiliki chuo, shule, miradi, bado itakuwa sehemu ya utumishi wangu kwa Mungu ili kuwa wa juu na wa kwanza kwa vyote na katika vyote sawa na mapenzi yake Mungu.
NGUVU YA MAONO
Huwezi kufanikiwa vema katika jambo lolote kubwa usipokuwa na maono nalo. Maono yenyewe kama yalivyo ni nguvu, tena ni imani, tena ni ulinzi, tena kichocheo (catalyst), ni Zaidi ya jitihada unazoweza kuzifanya katika jambo lolote. Maano yanaelezea na yanalihakiki jambo kuanzia mwisho wake kuja mwanzo wake, hivyo unaona unakoenda na jinsi unavyofanikiwa hata kabla hujafanikiwa wala kufikia.
Ni muhimu kufahamu kuwa kazi ya akili ni kuutumia ubongo kutekeleza wazo au adhimio lolote lililo ndani ya mtu liwe baya au jema. Akili inatengeneza mbinu mbalimbali kwa kuutumia ubongo ili kufanikisha adhima yoyote ile iliyoadhimiwa na mtu. Hivyo ukiwa na maono, yale maono mbali na kuhifadhiwa sehemu nyingine kama moyoni, pia hukaa kwenye akili, hivyo akili wakati wote hutumia ubongo kufanya namna mbali mbali ili kutekeleza hilo ambalo ndiyo maono.
Pia kinyume chake ni kuwa kama hauna maono, unaifanya akili yako itekeleze kila jambo linalokuja ndani yake karibu kila siku. Mfano mtu akikusema vibaya, kama huna maono na kama hayana nguvu ndani yako, unaifanya akili yako kutwa nzima ishinde inatafuta namna ya kufanya ili kutekeleza hilo la huyo aliyekusema. Kama ni jambo ambalo akili itashindwa kupata suruhu, ina maana akili haitaridhika na itapelekea kuliwaza kila wakati na kukwama katika mambo mengine.
NAMNA YA KUWA NA MAONO
Huwezi kuwa na maono nje yako, hata Mungu hawezi kukuletea maono nje yako, ikimaanishwa kuwa ni lazima yawe maono ambayo kwa kweli ndiyo wewe, na ndivyo ulivyo. Kuna maono ya kuletewa na kuna maono ya kutengeneza wewe mwenyewe, na mara nyingi ukitengeneza maono wewe mwenyewe kwa namna ya kawaida utayaacha na huwa yatabadilika.
Mbali na yale ya kuletewa, wewe unaweza kuwa na maono ambayo yanazaliwa ndani yako. Hilo si jambo la kufikri ila linazaliwa kama wewe ulivyozaliwa. Maana kila mtu ndani yake kuna maono, ambayo mara mnyingi hayako wazi kwake, hivyo ni kazi ya kuyatambua na kuyajua.  Hii ni hatua ambayo mtu anaingia kwa makusudi na kwa dhamili hatua hii ni hatua ya ufunuo, Kimungu yaani unafunuliwa kilichoko ndani yako, hivyo unakitambua na kukielewa. (vision recognition and understanding)
Ili kutambua maono, ni lazima uwejifahamishe wewe mwenyewe kukuhusu, maana maono yako ndiyo wewe mwenyewe. Hivyo ukishaweza kujijua vema ulivyo, undani wako usiobadilika ambao ndiyo asili yenyewe hapo unaweza kutambua maono yaliyoko ndani yako. Na kwa kuwa tumetofautiana uwezo wa utambuzi, unweza kuomba usaidizi ili kutambua maono yako, ikiwa ni wewe mwenyewe kwa Mungu au mtu kukusaidia.
FUNGUO ZA MAONO          
Hapo kwenye maono, kuna vitu ambavyo vinashika hayo maono ambavyo ni lazima vijulikane na tena uwe navyo wakati wote ili viwe kwenye akili itumie ubongo wakati wote kuvitekeleza.
Nitumie mfano wangu:
Maono yangu ni “kumtumikia Mungu, kwa kiwango cha juu, cha kwanza, katika vyote na kwa vyote sawa na mapenzi yake” kwa kingereza “to serve the LORD GOD, to the best level of all with all to His will”
Katika maono haya, funguo zake ziko 5
1. Kumtumika Mungu (serving Lord God)
2. Kiwango cha juu na cha kwanza (best level)
3. Katika yote (of all)
4. Kwa vyote (with all)
5. Mapenzi yake (His will)
Kwa hiyo, huu unakuwa ndio msingi wangu wa maonowa vitu ninavyo paswa kuvitekeleza wakti wote

KIAPO/ COMMITMENT
Ili uweze kufanikiwa katika maono yako ni lazima uwe na kiapo juu yako mwenyewe.  Mfano mimi ili kufikia maono yangu kwa jinsi yalivyo na funguo zake, nimejiapia kuwa “Goodluck Kazili katika kila jambo ni lazima nimtumikie Mungu, tena kwa kiwango cha juu na cha kwanza, tena sawa na mapenzi yake”
Kama unavyojua kiapo ni kitu ambacho kikishakuwa ndani yako, huna uhuru wa kuchagua kutekeleza au kutokutekeleza. Hivyo kila wakati utajikuta unakumbuka ufanyapo jambo na kuliangalia kama liko sawa na maono yako tena kama linaongeza jambo kwenye maono yako
MPANGO MKAKATI (STRATEGIC PLAN)
Hii ni mipango tofautitofauti inayohusu maono na inayopaswa kutekelezwa ambayo kufanikiwa kwake ndio kufikiwa kwa maono. Hapa ndipo akili inapofanya kazi zaidi kufikia maono ambayo yako ndani yako.

MWISHO
Wakati wote kumbuka kuwa , kama huna maono utatumikia maono ya watu wenginge. Na ukweli ni kuwa hukuzaliwa ili utumikie maono ya watu wengine, lakini kama huna lazima utumikie tu, aidha kwa kujua au kwa kutokujua.
Pia maono yanakua, hivyo upana wa maono yako kwa sasa au ya kipindi flani hayatabaki na ukubwa au upana uleule. Maana kwa kadri wewe unavyokua ndivyo na Yeneyewe yanavyokua.
Maono makuu yanapaswa kuwa ya kumtumikia Mungu, na mengine yote kuwa madogo.
Mungu wa mbinguni akujalie kuwa na maono yanayoujenga ufalme wake.

Mwl. Goodluck kazili
Email: gkazili@yahoo.com
Phone: 0765 129 960
Blog:  Kazili.blogspot.com




Jumatano, 10 Februari 2016

FUNGUO ZA UTAWALA (KEY OF DOMAIN)

Na Mwl; Goodluck Kazili

"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

1. MAARIFA (Knowledge)
2. NGUVU ZA KIROHO (Spritual power)

Maarifa humuwezesha mtu kutawala, nguvu za roho humuwezesha mtu kutiisha

wakati Mungu anamuumba mtu, alikusudia mtu huyo aitawale nchi na vyote lakini pia na kuvitiisha (Mwanzo 1:26). huwezi kutawal bila kuwa na maarifa, kadhalika huwezi kutiishi kama huna ngvu

wakati wote anayetawala ni yule mwenye maarifa zaidi. Mungu alimpa mtu uwezo wa ziada kimaarifa zaidi ya viumbe wote, na kwa hayo maarifa anawatawala. Mwanadamu angepewa uwezo wa kimaarifa sawa na wanyama wengine basi asingeweza kuwatawala bali kingetumika kigezo cha pili cha kutiisha na hapo kwa vile mwanadamu asivyokuwa na nguvu basi simba, tembo, na wanyama wengine ndio wangetawala.

hivyo utawawala wowote ule unategemea maarifa na nguvu. Mtu asiyekuzidi maarifa hawezi kukutawala, labda kwa kigezo cha pili yaana nguvu. mfano kiongozi, huwaongoza au huwatawala watu kwa kutumia maarifa na nguvu ya sheria. hata kama utakuwa unamzidi maarifa bado anaweza akakutawala kwa kutumia nguvu ambayo inaweza ikawa ile halisi au ya kisheria.

unataka kutawala ni lazima uwe na maarifa zaidi na ngvu pia. lakini kwa vile tunavyopaswa kuenenda kwa roho hauhitaji nguvu za mwili bali za roho, maana ile kuwa na maarifa hukupa pia nguvu za mwili. maana maarifa ni sawa na nguvu (knowledge is equevalent to power) 

itaendelea....

SK-Siri Kuu by
Goodluck Kazili

Kunihusu

Picha yangu
"Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga. Naam, baba , kwa kuwa ndivyo ilivyopendeza mbele zako. (Ni Siri Kuu)

Tafuta katika Blogu Hii