KUHANI GOSPEL TEAM
(KGT-TANZANIA)
TAARIFA KUHUSU TIMU
01. UTANGULIZI
KGT ni kifupi cha Kuhani Gospel Team kwa kiswahili Timu ya Kikuhani ya Injili, inayojihusisha na huduma za kuujenga ufalme wa Mungu/mbinguni hapa Duniani, huduma hizo ni pamoja na Mikutano ya Injili, uinjilisti wa nyumba kwa nyumba na maeneo ya mkusanyiko, uimbaji,Maombi na maombezi, Semina za Neno la Mungu, Malezi kwa waamini/waliookoka, Ushauri, kusaidia huduma, kusaidiana na kanisa kulinda na kuweka uchaji wa Mungu katika nchi
02. TIMU YENYEWE
Timu hii inaundwa na watu wanaoshuhudiwa kuwa wameitwa na kuteuliwa na Mungu kumtumikia Yeye, haina dhehebu wala Dini kwa maana ya kubagua ila ni timuya Kikristo kwa maaana ya inayomwamini na kumfuata Kristo Yesu. Inashirikiana na makanisa yote Yenye msingi wa Kristo, Inashirikiana na vikundi vyote vyenye msingi wa Kristo, inashirikiana na Watu wote wafanyao huduma katika msingi wa Kristo, na inajitoa kutumika mahali popote, mazingira yoyote na kwa namna yeyote maadamu kibali Cha Roho mtakatifu kipo.
Timu ina wahudumu zaidi ya 70, ambao wanaishi maeneo tofautitofauti katika nchi. Mfumo wa timu unamruhusu mtu kuwa katika timu akiwa popote ndani au nje ya nchi.
Timu imeweka watumishi walio washauri, ambao ni wachungaji wa makania tofautitofauti, watu wenye huduma mbalimbali wanaoshuhudiwa kuwa wema na wenye wito na mzigo na kazi ya Mungu, ambao kwa nafasi na neema ya Mungu iliyo juu yao, wanaijenga timu na kuifanya isonge mbele katika kutekeleza wajibu wa kuujenga ufalme wa Mungu, ili pia kufikia maono ya timu.
03. KUMBUKUMBU
Timu hii ilianza 11/2013, ikiwa na wanatimu karibu 30 waliounganishwa pamoja na Roho Mtakatifu na kuweka msukumo wa uundaji wa timu, miongoni mwa watu hao walikuwa wameshiriki huduma mbalimbali hasa wakiwa kama wanafunzi.
Mwezi huo wa 11 kwa usimamizi wa Roho Mtakatifu, Timu hii iliundwa rasmi kwa Ushirika wa Roho Mtakatifu, na sasa watu hawa waliweka maadhimio na mipango ya namna ya kuendelea mbele na mfumo utakaotumika ili kuifanya timu hii itimize wajibu ambao Roho mtakatifu anahimiza ndani yao.
2014 mwezi wa 6, Baada ya kufanya Huduma Katika wilaya ya Mpwapwa, Timu ilipata kibali cha kuunda timu katika wilaya ya Mpwapwa, timu hiyo iliundwa na kuwa kanda kamili ya KGT. Hivyo timu sasa iliendeshwa kikanda, kanda ya Dodoma mjini na kanda ya Mpwapwa.
Mwezi wa 9/2014 kwa mara ya kwanza kwa pamoja Timu kwa umoja na ushiriki wa Kanda zote ilifanya huduma Galigali kijiji kilichopo mpwapwa karibu na mkoa wa iringa, katika Huduma hiyo Dodoma mjini iliwakilishwa na wahudumu 13, Mpwapwa iliwakilishwa na wahudumu 17. Katika huduma hiyo Timu ilishirikiana na Kanisa kuu Anglikana ving’hawe.
Mwezi wa 11/2014, Timu kwa kushirikiana na UKWATA Dodoma mjini, walifanya huduma Wilayani Kongwa, huduma ya mkutano na uinjilist wa nyumba kwa nyumba pamoja na Semina. Huduma hiyo iliyoratibiwa na umoja wa makanisa Kongwa ilifungua mlango wa Timu kuunda Kanda nyingine ya Kongwa. Hivyo kuifanya KGT kuwa na kanda Tatu.
04. MAONO YA KGT-TANZANIA
“Kumfanya kila mtu (katika mapenzi ya Mungu) amwamini, ampokee na kumjua Mungu wa pekee na kweli na Yesu Kristo aliyetumwa Duniani kwa ajili ya wokovu”
05. WAJIBU WA TIMU
Timu ina wajibu ambao ndio msingi wa kuundwa na kuwepo kwake, wajibu huo unagusa maeneo mawili:-
05.1. KWA MWANATIMU
“Kumsaidia kila mwanatimu kumtumikia Mungu kwa kiwango alichomkusudia”kwa maono haya, timu inawajibika kuangalia wito wa Mungu ndani ya kila mwanatimu na kumuandalia mazingira ya kutumika, ikiwa ni pamoja na kumwandaa ili kutumika sawasawa na mapenzi ya Mungu.
05.2. KWA WASIO WANATIMU
Kuwahubiri vema, ili wamwamini Yesu Kristo na kuupokea ufalme wa Mungu/mbinguni, kuwafundisha kumjua Mungu wa pekee na wa kweli na Yesu Kristo, kuwalea kwa Kusaidiana na Kanisa ili kutunza na kulinda wokovu walioupata ili wadumu katika Pendo la Mungu katika Ufalme wake.
06. KAULI MBIU
“Mjue Sana Mungu, Ili Uwe na Amani”
07. MSUKUMO NA MSIMAMO WA TIMU KWA WANATIMU
“Kumuabudu Mungu, uzima hadi mauti, mauti hadi uzima, uzima na mauti hadi milele na milele”
08. KUTUMIKA KATIKA TIMU
Timu ina namna ya kutumika wakati wa huduma katika namna mbili, kuna utumishi wa kudumu na utumishi wa huduma.
08.1. UTUMISHI WA KUDUMU
Huu ni utumishi ambao mtumishi anakuwa sehemu halisi ya timu na anawajibika katika mambo yote yanayoihusu timu wakati wote, anahusika katika kupanga, kuamua na kujishughulisha na timu wakati wote, pia anajulishwa kila jambo na kuhusihswa katika uendeshwaji wa timu. Hadi sasa timu ina watumishi/wahudumu wa kudumu 70 kwa Kanda Zote.
08.2. UTUMISHI WA HUDUMA
Huu ni utumishi ambao mtumishi anashiriki huduma tu, ziko nyakati ambazo timu huwa na huduma sehemu mbalimbali katika mikoa, wilaya, vijiji na mitaa. Kwa mtumishi anayetambuliwa au aliyepata kibali cha kutumika kwa njia hii, wakati unapofika wa huduma Timu inampa taarifa na namna ya kushiriki katika huduma, na kisha mtumishi huyo huungana na timu tayari kwa kufanya huduma, baada ya huduma mtumishi hahusishwi na uendeleaji na uwajibikaji wa timu. Hadi sasa timu ina watumishi wa Huduma zaidi ya 10.
09. MFUMO WA KGT
Timu ina mfamo wa uendeshaji unaoisaidia timu kuendelea mbele na kutimiza wajibu iliopewa na Mungu. Timu ina mfumo wa Kanda kimaeneo na zote hutumia mfumo mmoja katika uendeshaji wa timu ngazi ya kanda. Pia ina mfumo wa idara za utendaji kazi/huduma kulingana na karama na vipawa vya kutumika. Timu ina idara 6 zinazosimamia shughuli zote katika timu. Katika idala yuko/wako wasimamizi wa Idala hizo na waliosalia wote ni wajumbe wa Idala kulingana na Karama pamoja na kipawa alichonacho. Timu inajumuisha watu wa lika zote, katika kusimamia, suala la lika halihusiki sana, zaidi ni uwezo na jinsi karama inavyofanya kazi ndani ya mtu.
10. IDARA ZA KGT
10.1. KGT UTATU
Hii ni Idara ambayo ndani yake limo kundi la uombaji, uinjilist, malezi, ushauri na maelekezi. Idara hii huratibu shughuli zote na kuwajibika ipasavyo ili kutimiza mambo yanayoangukia kwenye idara hiyo kwa kila kudi kama yalivyo. Mfumo huu wa kiutendaji ni wa kanda zote, hata hiyvo Idara ina wasimamizi watatu kwa kila kanda na ni wazi kuwa timu ikiongezeka basi wasimamizi hao huongezwa.
10.2. KGT HAZINA
Hii ni idara inayosimamia Sadaka na upatikanaji wa mahitaji mbalimbali katika timu ili huduma zisikwame kwa uhitajiwa wa fedha na vitu. Idara hii inahusika na kuomba, kujua na kutekeleza upatikanaji wa mahitaji mbalimbali ya kuisaidia timu kuendesha huduma, pia idara inahusika na kuhifadhi, kutunza na kulinda ili timu iwe na hazina ya kutosha.
10.3. KGT HABARI NA MAWASILIANO
Hii ni idara inayoratibu masuala yote ya kutoa na kupokea habari/taarifa kutoka na kwenda mahali husika. Pia inahusika katika kufungua na kusimamia vyombo vinavyohusika na utoajia habari kama vile mitandao ya kijamii, redio, runinga na simu.
Idara hii inashirikiana na idara ya “KGT production”katika kuandaa matangazo, kuzalisha na kusambaza kazi za huduma ili kutimiza wajibu wa timu wa kuwafikia wengi kwa njia za kila namna.
10.4. KGT PRODUCTION
Idara hii inahusika na kuandaa matangazo, kuchukua kumbukumbu za huduma, kusambaza kazi za huduma kama vile tape, CD, DVD na machapisho. Pia Idara hii hushirikiana na idara maalumu kuweka mazingra mazri ya huduma.
10.5. KGT WORSHIP
Idara hii, inahusika na masuala yote ya uimbaji wakati wa huduma za timu na wakati mwingine wowote inapopaswa kuhudumu. Pia idara hii, inahusika kuibua, kuchochoe na kusimamia watu wenye wito wa kuimba wafanye vema katika wito huo, ikiwa ni pamoja na kuwaandaa na kuwaatengenezea mazingra ya kutumika kwa kiwango stahiki.
10.6. IDARA MAALUMU
Hii ni idara inayohusika na kuratibu shughuli zote zisizoangukia katika idala zilizotajwa, shughuli hizo ni pamoja na masuala ya kusaidiana, masuala ya chakula wakati wa huduma, kusimamia Muonekano wa wanatimu Hasa wakati wa huduma, kubuni vitu vinavyoendeleza timu kwa mtazamo wa kiroho na kimwili.
11. HUDUMA KATIKA TIMU
Timu hii kwa mujibu wa ufunuo wa kuundwa kwake na maono ya uendeshwaji wake, timu inajikita katika kufanya huduma zaidi na kuwaandaa watumishi. Hivyo huduma zilizo kuu ni kuwatangazia watu habari za ufalme wa Mungu, kwa njia ya kuwahubiri na kuwaombea, pia kuwafundisha ili wajue jinsi ufalme wa Mungu ulivyo kwa njia ya Semina. Kufanya ibada kama timu ikiwa ni kuendelea kuleana na kuimarika ili kuwa na uwezo wa kufanya huduma sawasawa na mapenzi ya Mungu.
Timu inajikita maeneo ya miji midogo na vijiji hasa maeneo ambayo Injili haijawafikia Vema. Katika hayo timu inafanya mikutano ya injili, na hupeleka semina kila mwaka katika maeneo yote iliyokwisha fanya huduma ya uinjilist nia ikiwa ni kuzaa matunda na kulea na syo kuzaa tu.
Ziko huduma zifanywazo na kanda, lakini pia zipo huduma za ngazi ya timu. Huduma za kanda zinafanyika katika eneo linaloizunguka kanda kwa upana wake, na huduma za ngazi ya timu zinafanyika eneo lolote.
12. MWISHO
Timu hii, ina nia ya kutumika kwelikweli kwa kadri neema ya Mungu inavyofunuliwa. Inalenga kupanuka kuimarika na kukua zaidi. Inaendelea kuomba ili kujua mapenzi ya Mungu kamili katika nchi na watu, kuendelea kuweka mfumo wa kutumika zaidi na kufikia ukomo mwema wa uimalikaji wa kila mtu katika ufalme wa Mungu. Timu inaendelea kusimama vema, kuhakikisha inatimiza wito huo kwa gharama yoyote, kwa maana hiyo, timu hailegei wala haichoki katika hali yoyote, katika mazingira yote ina imarika na itaimarika zaidi na zaidi. “KGT-TANZANIA, Mjue Sana Mungu Ili uwe na Amani”
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni